Tuesday, July 23, 2013

SALAMU ZA RC IRINGA KATIKA MAZISHI YA MWANAJESHI ALIYEFARIKI DARFUR -SUDAN



Salamu za Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine G. Ishengoma (Mb.) katika mazishi ya CPL Osward Paulo Chaula amesema yafuatayo:
 

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine G. Ishengoma (Mb.) akitoa salamu za Mkoa wa Iringa

 Wanajeshi wakitoa heshima zao kwa marehemu CPL. Osward Paulo Chaula

Kwa masikitiko makubwa kwa niaba ya wananchi wa mkoa wa Iringa, napenda kutoa poke kwa familia ya Paulo Chaula kwa kufiwa na kijana wetu askari CPL.Osward Paulo Chaula, ambaye alikuwa akishiriki ulinzi wa amani nchini Darfur, Sudan.
Tukio hilo lilitokea tarehe 13 Julai, 2013.

Mkoa wa Iringa na Taifa kwa ujumla, tunakiri kwamba tumeondokewa na kijana wetu shujaa, mzalendona mchapa kazi ambaye umauti umemkumba akiwa kazini. askari huyu alikuwa tegemeo kubwa kwa Taifa letu la Tanznaia. Tunaahidi tutayaenzi yale yote mazuri aliyotuachia watanzania.
kutokana na tukio hilo, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilolo zinatoa pole ya Tshs. 500,000/= kwa familia ya Paulo Chaula.
=30=
MATUKIO KATIKA PICHA YA MAZISHI YA MWANAJESHI ALIYEFARIKI DARFUR NCHINI SUDAN 

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt Christine G. Ishengoma (Mb.) akisaini kitabu cha wageni katika mazishi ya CPL.Osward Paulo Chaula

 Baadhi ya waombolezaji wakipita kutoa heshima zao za mwisho mbele ya mwili wa marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Waombolezaji wakiomboleza kifo cha CPL.Osward Paulo Chaula

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akiaga mwili wa marehemu

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe. Gerald Guninita akiaga mwili wa marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa akiaga mwili wa marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakiaga mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wenzake wa Jeshi la Wananchi wakibeba jeneza lenye mwili wamarehemu wa CPL.Osward Paulo Chaula
Wanajeshi vijana wa JWTZ wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula

Mwili wa CPL.Osward Paulo Chaula ukipelekwa makaburini

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akiweka udongo katika kaburi alimolala marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi Scolastica Mlawi akiweka udongo katika kaburi alimolala marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Waombolezaji wakiomboleza kifo cha CPL.Osward Paulo Chaula

Wapiganaji wa JWTZ wakiendelea na taratibu za kijeshi katika mazishi

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akiweka Shada la ua katika kaburi alimolala marehemu CPL.Osward Paulo Chaula

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb.) akikabidhi rambirambi kwa familia ya marehemu CPL.Osward Paulo Chaula