Friday, September 2, 2011


KARIBUNI KATIKA BLOG YA WANAFUNZI WOTE POPOTE TANZANIA (MATUKIO NA WANAVYUO)

Kwanza tunapenda kuwasalimu sana Ndugu walimu na wanafunzi na wadau wote mliopo popote nchini Tanzania na Duniani kwa ujumla, Kwa heshima na Taadhima tunapenda kuwatambukisha kwenu Blog mpya kabisa inayo kwenda kwa jina la MATUKIO NA WANAVYUO ambapo lengo kubwa ni kuwakutanisha wanavyuo wote Nchi nzima na kubadilishana mawazo pia kujua nini kinaendelea kila wakati kupitia mtandao huu, Hatuna mengi sana ya kuandika hapa kwa maana mtandao wenu unajieleza vizuri kabisa, pia mtandao huu ni wanavyuo wote waliopo vyuoni sasa na wale walio maliza pia ni wa watanzania wote kwa ujumla kwa maana kuna mambo yanayo wahusu na muhimu. Tunawaomba mpitie kila kona ya mtandao huu na kutoa maoni kama yapo nini kiongezwe ama kuboreshwa zaidi, Tunawakumbusha tena mtandao huu ni wako. sisi tunaongoza tuu kwa mawasiliano zaidi tutumie Barua pepe kupitia
( twanavyuo@live.com)
tunatanguliza  shukrani zetu pia atakae pata taarifa hii ampe na mwenzake
Asanteni sana.
Matukio na wanavyuo Crew

KUTEMBELEA MTANDAO HUU BOFYA HAPA
http://www.tzwanavyuo.blogspot.com/

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,
Dkt. Christine Ishengoma


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt. Christine G. Ishengoma (Pichani)ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Ruvuma kufanya ukaguzi wa kina katika magari yote yanayotumika kusafirisha abiria katika wilaya zote.
Katika agizo hilo, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, amesisitiza juu ya umuhimu wa kuyachunguza, kuyakagua na kuyazuia magari yote yenye hitilafu za kiufundi yasifanye kazi ya kusafirisha abiria na mizigo.
Lengo la agizo hilo ni kudhibiti matukio ya ajali ambazo zinaweza kugharimu maisha ya wananchi pindi ajali zinapotokea. Hii inafuatia tukio la hivi karibuni ambapo gari la abiria linalofanya shughuli zake kati ya Mbinga na Mbamba-bay kupata ajali na kusababisha vifo vya watu sita na wengine kujeruhiwa. Ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Chunya ikiihusisha gari lenye namba T.270 BDG.
Katika ajali hiyo, gari hilo lilikuwa limepakia abiria na mizigo miongoni mwake yalikuwa mafuta ya Diesel na Petrol, hivyo baada ya ajali kutokea, mafuta yalishika moto na kusababisha vifo hivyo.
Ili kutekeleza agizo hilo, Jeshi la Polisi Mkoa litatakiwa kukagua na kuwazuia wenye magari ya abiria kubeba mizigo ya mafuta ya diesel/petrol katika magari yao, kudhibiti na kuzuia gari kubeba abiria wengi zaidi ya uwezo wake na mwisho kuyazuia magari yote yasiyo na sifa na vigezo vya kubeba abiria kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria ya usalama barabani.
Mwisho, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wote waliopoteza ndugu zao kufuatia vifo hivyo na aidha, anawatakia pole na kuwafariji abiria wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo na amesisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote waliosababisha ajali hiyo kutokea.
Imetolewa na:
Revocatus A. Kassimba,
Afisa Habari,
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,
RUVUMA.