Thursday, November 3, 2011

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU 

TAWALA ZA MIKOA ZA SERIKALI ZA MITAA






OFISI YA MKUU WA MKOA WA IRINGA



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU KIMKOA NA MAPOKEZI YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU TAREHE 7-11/11/2011


IMETOLEWA NA;    
MHE. DR. CHRISTINE G. ISHENGOMA (Mb.)
          MKUU WA MKOA WA IRINGA



Sanduku la Posta: 858, IRINGA
Simu: 255 026 2702715/2702021/2702191
Fax:   255 026 2702082
Barua pepe: rasiringa@pmoralg.go.tz


Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa:
Tarehe 7 hadi 9 Novemba, 2011 tutakuwa na maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru kimkoa ambayo yatafanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Hayati Samora uliopo katika Manispaa ya Iringa. Maadhimisho haya ni maalum kwa ajili ya kufanya tathmini ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kijamii tulizofanya kimkoa kwa kipindi cha miaka 50.

Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa:
Wakati wa maadhimisho haya ambapo kutakuwa na maonesho mbalimbali ya shughuli za maendeleo tunazofanya hapa Mkoani, burudani ya ngoma, sanaa, michezo na hotuba mbalimbali za viongozi katika ngazi za Vijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa tunapaswa kufanya tathmini kuona wapi tumetoka, wapi tulipo na wapi tunakwenda. Hii itatusaidia kujiwekea malengo mapya ambayo yataongeza kasi ya maendeleo katika Mkoa wetu kama kauli mbiu ya Maadhimisho haya inavyosema “TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE”.

Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa;
Maadhimisho haya ya miaka 50 ya UHURU yanakwenda sambamba na mapokezi ya Mwenge wa Uhuru ambao utapokelewa hapa Mkoani Iringa tarehe 09 Novemba, 2011 katika Tarafa ya Wanging’ombe iliyopo katika Wilaya ya Njombe (Mwenge utapokelewa toka Mkoa wa Mbeya) na tutaukabidhi Mkoa wa Ruvuma tarehe 11 Novemba, 2011.

Ukiwa hapa Mkoani, Mwenge wa Uhuru utafungua miradi minne  (4), kuweka mawe ya msingi miradi minne (4) kuzinduliwa mradi mmoja (1) jumla miradi tisa (9) yenye jumla ya thamani ya Tshs. Tshs. 486,833,845/=  Pamoja na kufungua miradi hiyo kutakuwa na mikesha ya Mwenge katika viwanja vya Samora katika Manispaa ya Iringa tarehe 9 na Uwanja wa Sabasaba tarehe 10 katika Halmashauri ya Mji wa Njombe.
Wakiwa Manispaa ya Iringa, wakimbiza Mwenge watapata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya shughuli mbalimbali ya miaka 50 ya Uhuru.
TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE.

Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa:
Shughuli hizi mbili ni za kihistoria, kwa sababu kila mmoja wetu atapata fursa ya kushuhudia mafanikio tuliyofikia. Hivyo, ninawaomba mjitokeze kwa wingi kuanzia tarehe 7 hadi 11 Novemba, 2011 kwenye maonesho tutakayofanya katika uwanja wa Samora na kwenye mapokezi ya Mwenge wa Uhuru ili tuweze kwa pamoja kuiandika historia ya Mkoa wetu vizuri kwa manufaa yetu wenyewe na vizazi vijavyo.


ASANTENI KWA KUNISIKILIZA

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE.