Sunday, January 21, 2018

MATUKIO KATIKA PICHA UFUNGUZI MICHEZO YA TAASISI MKOA WA IRINGA

TIMU YA RAS IRINGA WAPOTEANA UWANJANI BAADA YA KICHAPO CHA 5-0 TOKA TANROADS



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  
Timu ya mpira wa miguu ya RAS Iringa imechapwa magoli 5-0 na  wakala wa Barabara (TANROADS) katika mechi ya ufunguzi iliyoshuhudiwa na mamia wa wakazi wa Manispaa ya Iringa wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela.

Mechi hiyo iliyochezwa katika dimba la chuo cha Ualimu Kleruu kilichopo manispaa ya Iringa ilianza kwa kasi ndogo huku kila timu ikosoma mchezo wa mwezake. Hadi kipinci cha kwanza kinaisha timu ya RAS IRINGA ilikuwa nyuma kwa goli Moja. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kidogo. 
 
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akisalimiana na Peter Nyakigera
Jitihada za RAS IRINGA kurudisha goli zilionekana wazi kabla ya juhudi hizo kufifishwa baada ya golikipa wao namba moja Mashaka Mwanage kuumia mkono wa kuume na kushindwa kuendelea na mchezo. Pigo hilo kwa RAS IRINGA lilifungulia mvua ya magoli hadi kufikia magoli matano.

Tangu awali TANROADS walionekana kukamia mechi hiyo huku wakiwa na kikundi cha washangiliaji mahili. Muda wote wa mchezo meneja wa TANROADS Mhandisi Daniel Kindole alikuwa akifuatilia kwa makini mechi hiyo.

Baada ya kipeng cha mwisho watumishi wa RAS walionekana kuondoka mmoja mmoja kwa njia yake jambo lililotafsiriwa na wachambuzi wa masuala ya soka kuwa ni kuvurugwa na kichapo hicho.
=30=

WATUMISHI WANAOSHIRIKI MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU MKOANI IRINGA WATAKIWA KUCHEZA KWA NIDHAMU



Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Watumishi wa taasisi mbalimbali mkoani Iringa wametakiwa kucheza kwa nidhamu na kuepuka ugomvi katika mashindano ya mpira wa miguu yanayoendelea mkoani Iringa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika hotuba yake ya ufunguzi wa mchezo wa mpira wa miguu kwa taasisi za mkoa wa Iringa iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela katika uwanja wa chuo cha ualimu Kleruu kilichopo Manispaa ya Iringa jana.
 
Mkuu wa Wilaya y Iringa, Richard Kasesela
Masenza aliwataka wachezaji hao kucheza kwa nidhamu na kuepuka kuchochea ugovi. Alisema kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni burudani na unajenga urafiki hivyo, mashindano hayo yatumike kutoa burudani na kujenga urafiki miongoni mwa wanamichezo hao. 

Aliongeza kuwa mashindano hayo yatumike kujenga uzalendo kwa watumishi wa umma na watumishi wa taasisi zisizo za kiserikali mkoani Iringa. Aidha, aliwataka wanamichezo hao kutengeneza mtandao utakaowaunganisha kama wanamichezo na watumishi wa taasisi mbalimbali.

Katika salamu za afisa michezo Mkoa wa Iringa, Kenneth Komba kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, alisema kuwa michezo hiyo ni wazo la mkuu wa Mkoa wa Iringa kutaka kuwaunganisha watumishi wa taasisi za Mkoa wa Iringa kupitia mchezo wa mpira wa miguu. Alisema kuwa hadi kufikia jana jumla ya taasisi 21 zilikuwa zimejitokeza kushiriki mashindano hayo.

Wakati huohuo, mechi ya ufunguzi, timu ya Timu ya RAS Iringa ilikubali kichapo cha magoli 5 bila kutoka TANROADS.

Mashindano ya mpira wa miguu kwa taasisi za Mkoa wa Iringa ni mashindanao ya kwanza ya aina yake kufanyika mkoani hapa yakikabiliwa na changamoto ya udhanimi.
=30=