Wednesday, August 28, 2013

MATUKIO KATIKA PICHA YA SIKU YA FAMILIA NA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI MAHALA PA KAZI

                                          Wadau wakiwa wanafuatilia semina

                             Wadau wa semina wakifuatilia mafunzo

                                                    Wasanii nao hawakuwa nyuma

                                         Wafuatiliaji wakifuatilia wa Senina

                                                             Muda wa maakuli

                                                        Dkt. Paul Luvanda akitoa mada

                          Scolastica Mlawi akihamasisha watumishi kujimwaga katika muziki

                                                               Muda wa muziki


                                     Ndani ya ukumbi wa SIASA ni KILIMO




                 Washiriki wa siku ya Familia na Mapambano dhidi ya Ukimwi Mahala Pa kazi


                                                 Ndani ya ukumbi muda wa maakuli


                                 Mtoa mada akiwasilisha mada yake


        Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Mipango na Uratibu- Nuhu Mwasumilwe akifunga Semina



RS IRINGA PIMENI AFYA




Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa wametakiwa kupima afya zao ili kujitambua na kuchukua hatua dhidi ya maambukizi ya VVU na ukimwi kwa lengo la kuwa na afya njema na kuongeza ufanisi wa kazi.
                            Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Utawala, Scolastica Mlawi

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Utawala na Rasilimali watu, Scolastica Mlawi wakati wa kufungua semina ya siku ya familia na mapambano dhidi ya ukimwi mahala pa kazi kwa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Siasa ni Kilimo wilayani Iringa. 

Dkt. Christine amesema “ni vema kila mtumishi apime afya yake ili ajitambue na kuchukua hatua zinazostahili kwa kuwa huduma za kuzuia maambukizi mapya kwa watu ambao hawana maambukizi pia wale wenye maambukizi wasipate maambukizi mengine zinatolewa katika zahanati, vituo vya afya na hospitali za serikali, taasisi na mashirika binafsi”. Amesema kuwa wateja wanaotembelea vituo vya kutolea huduma za afya wakiwa wanaumwa magonjwa mengine aukusindikiza wagonjwa wanashauriwa kupima VVU. Amesema kuwa huduma hiyo imesaidia sana kuwafanya watu wengi kujua hali za afya zao kuhusiana na maambukizi ya VVU na kuchukua hatua.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inawajali sana watumishi wake hasa wanaoishi na VVU. Amesema “serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuwajali watumishi wake inatekeleza Waraka Na. 6 wa Mwaka 2006 kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ambao unamtaka kila mwajiri katika Wizara, Taasisi, Mashirika na Idara za Serikali  kuwasaidia watumishi wanaoishi na V.V.U. kwa kuwapa fedha kidogo kwa ajili chakula na nauli wakati wa kwenda kupata huduma za matibabu”.

Ameendelea kusema kuwa watumishi wamekuwa wakishauriwa kupima afya zao na kutoa elimu ya kuzuia maambukizi mapya. Katika kuonesha msisitizo, ametoa rai tena kwa watumishi kupima afya zao ili wanapogundulika kuwa na maambukizi ya V.V.U. waweze kupata huduma ya ushauri, vipimo, dawa, matibabu kwa magonjwa nyemelezi na mlo kamili.

Akiongelea malengo ya semina hiyo kwa watumishi, Afisa Tawala mwandamizi katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Neema Mwaipopo amesema kuwa lengo ni kuelimishana na kukumbushana kujikinga na maambukizi mapya ya ukimwi kwa ambao bado hawajapata na kwa ambao wamepata kujikinga na maambukizi mapya. Amesema kuwa lengo jingine ni kuwahamasisha watumishi kwenda kupima na watakaokutwa wameathirika watoe taarifa kwa mwajiri ili waweze kunufaika na msaada wa huduma kwa mujibu wa Waraka Na. 6 wa Mwaka 2006 kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma ambao unamtaka kila mwajiri kuwasaidia watumishi wanaoishi na V.V.U.

Neema amesema kuwa suala la unyanyapaa halipo kutokana na watumishi kupatiwa elimu ya mara kwa mara. Amesema kuwa utaratibu wa kutoa elimu kupitia semina, vikao na mikutano mbalimbali ni endelevu katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa.

Siku ya familia na mapambano dhidi ya ukumwi katika ofisi ya mkuu wa mkoa imeongozwa na kaulimbiu isemayo Iringa bila maambukizi mapya, unyanyapaa na vifo vitokanavyo na ukimwi inawezekana. 
=30=

Monday, August 26, 2013

PICHA ZA MATUKIO YA MKUTANO WA AMANI ULIOANDALIWA NA JUMUIYA YA WAISLAMU WA AHMADIYYA

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (katikati) Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry (kushoto) na Mstahiki Meya wa manispaa ya Iringa Aman Mwamwingi (kulia)

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (katikati) Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry (kushoto) na Mstahiki Meya wa manispaa ya Iringa Aman Mwamwingi (kulia) na Kamanda wa Polisi Mkoa, Afande Mungi
 
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dkt Leticia Warioba (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu (katikati) na kiongozi wa Jumuiya ya Ahmadiyya 

 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Dkt Leticia Warioba (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Evarista Kalalu (katikati) na kiongozi wa Jumuiya ya Ahmadiyya

 Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Gerald Guninita (kushoto)

 Wadau wa amani wakifuatilia mkutano

 Wadau wa amani wakifuatilia mkutano

 Wadau wa amani wakifuatilia mkutano

 Wadau wa amani wakifuatilia mkutano

 Wadau wa amani wakifuatilia mkutano

Ustaadh Rafik akisoma shairi kuhusu Amani

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma akisoma Hotuba



   Amir na mbashiri mkuu wa Jumuiya ya waislamu waahmadiyya Tanznaia, Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry

     Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu akitoa mchango wake kuhusu Amani

              Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi akichangia kuhusu amani

                   Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo akichangia mkutanoni.

                      Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evarista Kalalu akichangia mada

                Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita akichangia mkutanoni

Ag. RAS IRINGA ATAKA WADAU WOTE KUSHIRIKI KULINDA AMANI





Ushirikiano wa wananchi wote na wadau unahitajika katika kuhakikisha serikali inatimiza jukumu lake la kulinda na kusimamia amani na uslama nchini. 

          Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu

              Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi

           Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo


              Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evarista Kalalu
 
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu alipokuwa akichangia katika mkutano wa amani mkoa wa Iringa uliyoandaliwa na Jumuiya ya waislamu wa Ahmadiyya na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa. 

Wamoja amesema “serikali inalojukumu la kuhakikisha kuwa amani na usalama kwa watu wote, lakini katika kutekeleza hilo unahitajika ushirikiano wetu sote”. Amesema kuwa wananchi na wadau wote hawana budi kushirikiana katika kuhakikisha kuwa amani inadumishwa nchini. Amesema kuwa upendo ni nguzo mihumu katika kudumisha amani. Amesema amani haiwezi kuwepo kama hakuna upendo, na kushauri kuwa viongozi wote wajitahidi kuhubiri upendo ili kujihakikishia uendelevu wa amani.

Katika mchango wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhan Mungi amesema kuwaamani haiwezi kutafsiriwa kwa tafsiri moja pekee, bali inatafsiriwa kwa sifa zake. Amezitaja sifa hizo kuwa ni ukosefu wa vurugu na migogoro. Sifa nyingine amezitaja kuwa ni pamoja na ukosefu wa vurugu na uadui. Nyingine ni ukosefu wa chuki na ugomvi. 

Mungi amesema kuwa amani ya kweli inazo tabia sinazoonekana. Amezitaja tabia hizo kuwa ni kujali, kuheshimu, haki kwa watu wengine. Amesema kuwa tabia nyingine ni ukarimu na uvumilivu kwa imani ya watu wengine.

Amesema kuwa amani haishikiki bali ipo katika akili na roho na inapimika kwa kutokuwepo kwa vurugu. 

Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo amesema kuwa amani ni kichocheo kikubwa cha maendeleo nchini. Amesema kuwa ili jamii iweze kuwa na maendeleo ni lazima watu na makundi yote waweze kutii mamlaka zilizopo kisheria kwa sababu mamlaka zote zinatoka kwa Mungu. 

Evarista Kalalu amewataka wadau wote wa amani kujiuliza wamefanya nini katika kuhakikisha amani iliyopo inadumu na kuwa endelevu. “Tanzania hatuna mahali pa kukimbilia iwapo tutaamua kuvunja amani iliyopo. Wote wasio na amani wanakimbilia kwetu, hivyo sisi tutakimbilia kwa nani?” alihoji Mkuu wa Wilaya ya Mufindi. 

Amesema kuwa ni ukweli usiofichika kuwa katika jamii tunayoishi wapo watu wasiopenda amani hivyo ni jukumu letu kuwaripoti katika mamlaka husika. “Si kila mtu anaweza kuchukua hatua, hivyo tunahitaji kuwalinda wale wote wenye mamlaka za kuchukua hatua” alisisitiza Evarista. 
=30=