Wednesday, June 25, 2014

PICHA ZA MWENGE IRINGA DC

IRINGA DC

PICHA ZA MWENGE KILOLO

KILOLO

IRINGA DC YAKOPESHA VIJANA MIL 34



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Halmashauri ya wilaya ya Iringa imetoa mikopo ya zaidi ya shilingi milioni 34 kwa ajili ya kuviwezesha vikundi vya vijana vinavyojihusisha na ujasiliamali ili kuongeza mtaji na kujiletea maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Iringa, Dkt. Leticia Warioba katika risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyosomwa na Afisa Utumishi Mkuu wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Iringa iliyosomwa katika eneo la Isimani tarafani wilayani Iringa.
Dkt. Warioba amesema “katika kipindi cha mwaka 2013/2014 halmashauri ya wilaya imetoa mikopo yenye jumla ya shilingi 34,500,000 kwa vikundi 18 vya ujasiliamali vya vijana”. Amesema kuwa halmashauri hiyo ina vikundi 177 vya vijana vyenye jumla ya wanachama 1,358 kati yao wanaume 825 na wanawake 531.
Akiongelea mikopo kwa vikundi vya wanawake, mkuu wa wilaya ya Iringa amesema “katika kipindi cha mwaka 2013/2014 halmashauri imetoa mikopo yenye jumla ya shilingi 74,950,000 kwa vikundi 50 vya ujasiliamali vya wanawake.
Kuhusu ujumbe wa Mwenge wa Uhuru, mkuu wa wilaya amesema kuwa ujumbe uliobebwa mwaka huu 2014 “katiba ni sheria kuu ya nchi” chini ya kauli mbiu isemayo ‘jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba mpya’.
Amesema kuwa katika kutekeleza ujumbe huo wananchi na viongozi wa serikali, vyama vya siasa na madhehebu ya dini wameshiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata katiba mpya kwa kupiga kura ya maoni kupitia mabaraza ya katiba yaliyoundwa katika halmashauri ya wilaya ya Iringa. Amesema kuwa wananchi wote walishiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata katiba mpya. Amesema kuwa pamoja na wananchi kushiriki kupitia makundi mbalimbali serikali imeendelea kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura ya maoni ili kupata katiba mpya.
=30=








MAPOKEZI YA MWENGE IRINGA

KILOLO

KILOLO YAKABILIANA NA DAWA ZA KULEVYA NA RUSHWA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa- KILOLO
Wilaya ya kilolo imeendelea kukabiliana na mapambano dhidi ya dawa za kulevya na rushwa kwa lengo la kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na afya na maisha bora.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya kilolo Gerald Guninita katika risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Kikwete iliyosomwa na Katibu Tawala Wilaya ya Kilolo, Yusuph Msawanga mjini Kilolo.
Gininita amesema kuwa matumizi ya dawa za kulevya ni moja kati ya changamoto zinazolikabili taifa katika kipindi hiki. Amesema kuwa wilaya ya Kilolo katika kupambana na dawa za kulevya inatekeleza kaulimbiu isemayo “furahia afya siyo dawa za kulevya”. Amesema kuwa wananchi wamekuwa wakielimishwa kwa njia mtambuka athari za dawa za kulevya kiafya, kijamii na kiuchumi. Amesema kuwa wilaya yake imeemdela kufanya uhamasishaji kwa vijana kuanzisha shughuli za kiuchumi.
Akiongelea mapambano dhidi ya rushwa, Guninita amesema kuwa wilaya ya Kilolo kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inatekeleza kaulimbiu isemayo “palipo na rushwa hakuna maendeleo”. Utekelezaji huo ameutaja kuwa ni kutoa elimu kwa umma pamoja na kuzindua club za wapinga rushwa katika shule za sekondari (33) na shule za msingi (15). Mkakati mweingine ameutaja kuwa ni kufanya tafiti ndogo ndogo zenye matokeo ya haraka katika kutambua mianya ya rushwa ili zisaidie kukabiliana na tatizo la rushwa. Ameutaja mkakati mwingine kuwa ni kupokea taarifa za malalamiko kuhusu vitendo vya rushwa na kuzifanyia kazi kwa mujibu wa sheria.
=30=

MWENGE KUTEKELEZA MIRADI YA BIL. 3.1



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mwenge wa Uhuru kutekeleza miradi ya maendeleo yenye zaidi ya shilingi bilioni 3.1 katika siku nne za kukimbizwa kwake mkoani Iringa.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipowasilisha taarifa ya mkoa wa Iringa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa kupokea Mwenge wa Uhuru kutoka mkoa wa Morogoro leo.
Dkt. Ishengoma amesema Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Iringa utaweka mawe ya msingi, utakagua, utazindua na kufungua jumla ya miradi ya maendeleo 42 yote ikiwa na thamani ya shillingi 3,109,958,020”.
Amesema kuwa kati ya fedha hizo serikali kuu imechangia shilingi 1,329,471,899, halmashauri za wilaya na manispaa shilingi 946,005,221. Amesema kuwa michango ya wananchi ni shilingi 500,877,000 na shilingi 333,603,900 ni michango ya wadau wa maendeleo.
Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa mkoani Iringa utakimbizwa katika halmashauri nne za Kilolo, Iringa, Manispaa ya Iringa na Mufindi. Amesema kuwa Mwenge huo utakimbizwa umbali wa kilometa 1,159 na kukabidhiwa mkoani Njombe tarehe 28 Juni, 2014.

Akiongelea ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2014, Dkt. Ishengoma ameutaja ujumbe huo kuwa ni “katiba ni sheria kuu ya nchi” wenye kaulimbiu ‘jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba mpya’.
Akiongelea mchanganuo wa miradi hiyo, mkuu wa mkoa wa Iringa amesema kuwa jumla ya miradi 10 itafunguliwa, miradi 16 itazinduliwa, miradi 7 itawekwa mawe ya msingi na miradi 9 itakaguliwa. Ameitaja miradi hiyo kuwa inatokana na sekta za kilimo, ufugaji, maji, maliasili, ujenzi na barabara, afya, elimu na maendeleo ya jamii.
=30=



IRINGA WATAKIWA KUJITOKEZA KUUPOKEA MWENGE

Na. Dajali Mgidange, IRINGA
Wananchi wametakiwa kujitokeza kwa winngi kuulaki Mwenge wa Uhuru katika maeneo mbalimbali utakayokimbizwa mkoani Iringa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru mkoani Iringa mwaka 2014 ofisini kwake leo.
Dkt. Ishengoma amesema kuwa ni vizuri wananchi wakajitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru pindi utakapopita katika maeneo yao. Amesema “ninawasihi wananchi kuendela kudumisha amani na utulivu wakati wote ambapo Mwenge wa Uhuru utakuwa ukikimbizwa katika mkoa wetu na hata baada ya kuhitimisha mbio hizo katika mkoa wetu”.
Akiongelea uhamasishaji katika halmashauri, Mkuu wa Mkoa amesema “ninapenda kutumia fursa hii kuviomba vyombo vya habari na ninyi waandishi wa habari kuwahamasishwa wananchi katika halmashauri zote za Mkoa wa Iringa kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru katika maeneo yote ambako utapita, kushiriki katika mikesha ya Mwenge pamoja na kupokea ujumbe wa Mwenge wa Uhuru wa mwaka huu 2014”.
Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Mkoa wa Iringa utakagua, kuweka mawe ya msingi, kufungua na kuzindua jumla ya miradi ya maendeleo 42 yenye thamani ya Tsh. 3,109,958,020/=. Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utatoa ujumbe katika maeneo yote ambako utakimbizwa. Ameitaja miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru kuwa ni miradi ya barabara, elimu, afya, kilimo na ufugaji. Miradi mengine ameitaja kuwa ni miradi ya vijana na wanawake na hifadhi ya mazingira.
Mwenge wa Uhuru mwaka 2014 unaongozwa na ujumbe usemao “katiba ni sheria kuu ya nchi’’ wenye kauli mbiu isemayo ’ jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba mpya’.
=30=

Monday, June 23, 2014

IRINGA WATAKIWA KUKIMBIZA MWENGE KWA UTULIVU



Na. Dajari Mgidange, IRINGA

Wananchi wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru katika maeneo mbalimbali utakayokimbizwa mkoani Iringa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru mkoani Iringa mwaka 2014 ofisini kwake leo.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma

Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Iringa
Dkt. Ishengoma amesema kuwa ni vizuri wananchi wakajitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru pindi utakapopita katika maeneo yao. Amesema “ninawasihi wananchi kuendela kudumisha amani na utulivu wakati wote ambapo Mwenge wa Uhuru utakuwa ukikimbizwa katika mkoa wetu na hata baada ya kuhitimisha mbio hizo katika mkoa wetu”.
Akiongelea uhamasishaji katika halmashauri, Mkuu wa Mkoa amesema “ninapenda kutumia fursa hii kuviomba vyombo vya habari na ninyi waandishi wa habari kuwahamasishwa wananchi katika halmashauri zote za Mkoa wa Iringa kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru katika maeneo yote ambako utapita, kushiriki katika mikesha ya Mwenge pamoja na kupokea ujumbe wa Mwenge wa Uhuru wa mwaka huu 2014”.
Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Mkoa wa Iringa utakagua, kuweka mawe ya msingi, kufungua na kuzindua jumla ya miradi ya maendeleo 42 yenye thamani ya Tsh. 3,109,958,020/=. Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utatoa ujumbe katika maeneo yote ambako utakimbizwa. Ameitaja miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru kuwa ni miradi ya barabara, elimu, afya, kilimo na ufugaji. Miradi mengine ameitaja kuwa ni miradi ya vijana na wanawake na hifadhi ya mazingira.
Mwenge wa Uhuru mwaka 2014 unaongozwa na ujumbe usemao “katiba ni sheria kuu ya nchi’’ wenye kauli mbiu isemayo ’ jitokeze kupiga kura ya maoni tupate katiba mpya’.
=30=