Sunday, March 16, 2014

MAN U 0-3 LIVERPOOL

STEVEN GERRARD & LUIS SUARES akunaga!

STEVEN GERRARD hakunaga!

STEVEN GERRARD hakunaga!

MARTIN & LUIS hakunaga!

ONGEZEKO LA WATU IRINGA WAONGEZA MAHITAJI YA ARDHI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Ongezeko kubwa la idadi ya watu katika manispaa ya Iringa linaenda sambamba na ongezeko la shughuli kuichumi hatimae kusababisha kuongezeka kwa mahitaji na matumizi ya ardhi.
 
Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa, Immaculate Senje
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa, Immaculate Senje alipokuwa akiwasilisha mada ya Mpango kamambe wa mji wa Iringa (Iringa Master Plan) 2015-2035 katika mkutano wa wadau wa maandalizi ya Mpango Kamambe wa Mji wa Iringa uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari ya Lugalo.

Senje amelitaja ongezeko la idadi ya watu katika mji wa Iringa linaloenda sambamba na ongezeko la shughuli za kiuchumi linasababisha kuongezeka kwa mahitaji na tumizi ya ardhi. Amesema ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya matumizi ya ardhi upo umuhimu wa kuwa na mwongozo unaotoa dira ya ukuaji wa mji ambao ni endelevu.

Akiongelea matumizi ya ardhi, Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa amesema kuwa mji wa Iringa kama ilivyo miji mingine nchini unayo maeneo ya makazi yaliyopangwa na kupimwa pamoja nay ale yanayoenelezwa kiholela. Amesema kuwa eneo la makazi lililopangwa wakati wa ukoloni liko katika makundi matatu ambayo ni ujazo wa chini, ujazo wa kati na ujazo wa juu.

Akiongelea maeneo ambayo yameendelezwa kiholela, ameyataja maeneo hayo kuwa yanapatikana katika kata za Mwangata, Ruaha, Mkwawa, Mtwivila, Kihesa na Nduli. Amesema kuwa yapo maeneo ya vijiji vilivyoingia katika Manispaa siku za karibuni kama Kigonzile, Nduli, Mgongo, Mkoga na kitongoji cha Ulonge kuwa yana makazi yaliyotawanyika.

Akielezea matarajio yake baada ya mkutano, Senje amesema kuwa masuala muhimu, kero na changamoto zinazowakabili wakazi wa Iringa zitaibuliwa na kuwa msingi mkuu utakaoongoza uandaaji wa Mpango Kamambe utakaokidhi mahitaji ya wakazi wa Manispaa ya Iringa.
=30=

SERIKALI KUTENGENEZA MASTER PLAN KWA KUSHIRIKISHA WADAU



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Serikali imedhamiria kuona mji wa Iringa unakuwa na kuwa na maendeleo endelevu kwa ustawi wa kwa kuandaa mipango shirikishi kwa wananchi.
 
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita
Kauli hiyoimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa wadau wa maandalizi ya mpango kamambe wa mji wa Iringa (Iringa Master Plan) iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita.

Dkt. Ishengoma amesema “lengo kuu la kuandaa mpango kamambe ni kuwezesha ukuaji wa mji ambao ni endelevu katika Nyanja za kiafya, usalama, mpangilio mzuri, muonekano mzuri na ustawi wa jamii”. Amesema kuwa katika kufanikisha mpango huo, ushirikishaji mipango iliyopita na inayoendelea ya kisera katika ngazi mbalimbali za utendaji utazingatiwa.

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa mpango kamambe husimamia uendeshaji wa mji kwa muda wa miaka 20. Amesema kuwa mpango huo unaweza kufanyiwa mapitio baada ya miaka mitano (5). Akiongelea umuhimu wa mpango amesema kuwa mpango hutoa mwongozo wa matumizi mbalimbali kwa ujumla kulingana na mahitaji ya jamii husika. Ameyataja matumizi hayo kuwa ni makazi, biashara, viwanda, kilimo, ufugaji na matumizi mengineyo.

Akiongelea Sheria ya Mipango Miji namba 8 ya mwaka 2007 na Sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 na Sheria nyinginezo, hifadhi ya mazingira husimamiwa na mamlaka ya upangaji kwa kushirikiana na wadau wa mji husika.
=30=

UCHAGUZI WA JIMBO LA KALENGA KUFANYIKA KWA AMANI NA UTULIVU



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka wananchi wa jimbo la Kalenga kujitokeza kwa wingi kupiga kura za kumchagua mbunge wa jimbo hilo.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma
Kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma ameitoa alipoongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuelezea hali halisi katika jimbo la uchaguzi la Kalenga na kuwataka wananchi wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi kumchagua mbunge katika uchaguzi utakaofanyika tarehe 16/03/2014.

Akiongelea ulinzi na usalama, Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama katika Mkoa wa Iringa amewahakikishia wananchi kuwa ulinzi utakuwepo wa kutosha na vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kuhakikisha amani na usalama kwa wananchi katika kipindi chote cha kupiga kura na wakati wa kutoa matokeo.

Dkt. Ishengoma amesema kuwa maandalizi yamekamilika na vifaa vyote vinavyohitajika vimefika katika vituo vya kupigia kura. Amesema kuwa vituo vyote vitakuwa wazi kuanzia asubuhi hadi jioni kwa muda uliopangwa.
=30=