Sunday, December 29, 2013

IRINGA YAVUKA LENGO LA BRN KATIKA ELIMU








Mkoa wa Iringa imevuka lengo la matokeo makubwa sasa (BRN) kwa zaidi ya asilimia 60 kwa kiwango cha ufaulu kwa mtokeo ya kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013 ukishika nafasi ya tatu kitaifa.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kikao cha kamati ya uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga kidato cha kwanza mkoa wa Iringa mwaka 2014, Wamoja Ayubu katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao cha kamati ya uchaguzi mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.


 Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Wamoja Ayubu (kulia) akifungua kikao (kushoto) ni Afisa Elimu Mkoa wa Iringa Mwalimu Joseph Mnyikambi

Wamoja amesema “kiwango cha ufaulu ni kizuri sana na mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya tatu kati ya mikoa 25 ya Tanzania bara. Pia kiwango cha ufaulu kimepanda kwa Halmashauri zote. Kwa hiyo, nachukua nafasi hii kuzipongeza Halmashauri zote kwa kuvuka lengo la matokeo makubwa sasa ambalo ni asilimia 60 kwa mwaka 2013”. Amesema kuwa mwaka 2013 mkoa wa Iringa ulikuwa na watahiniwa 23,148 waliosajiliwa kufanya mtihani wakiwemo wavulana 10,752 na wasichana 12,396. Amesema miongoni mwao watahiniwa 22,922 wavulana wakiwa 10,630 na wasichana 12,292 sawa na asilimia 99 walifanya mtihani.

Akiongelea ufaulu, Wamoja ambaye pia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa amesema kuwa watahiniwa 14,956 (wavulana 7,042 na wasichana 7,914) ndio waliofaulu kwa kupata alama kati ya 100-250 sawa na asilimia 65.25. Aidha, amekieleza kikao hicho kuwa ni wakati muafaka kuweka mikakati ya kuongeza ufaulu zaidi hadi kufikia asilimia 70 ambalo ni lengo la matokeo makubwa sasa kwa mwaka 2014.

Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013 mkoa wa Iringa, Afisa elimu mkoa wa Iringa, Mwalimu Joseph Mnyikambi  amesema kuwa katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika tarehe 11-12 Septemba, 2013 shule za msingi 449 kati ya shule 482 ndizo zilizokuwa na watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi.

Mwalimu Mnyikambi amesema kuwa mahudhurio katika siku za mitihani yameongezeka kutoka asilimia 98.3 mwaka 2012 hadi asilimia 99 mwaka 2013 likiwa ni ongezeko la asilimia 0.7 . Amesema kuwa kiwango cha kumaliza elimu ya msingi kimeongezeka kutoka asilimia 82 (2012) hadi asilimia 84 (2013) ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 2.

Afisa Elimu Mkoa wa Iringa amezitaja shule 10 bora za serikali na binafsi kimkoa kutoka kila Halmashauri kwenye mabano kuwa ni:- Sipto, Ummusalaama, Ukombozi, St. Dominic Savio, Star, Wilolesi, St. Charles (zote za Manispaa ya Iringa) nyingine ni Brooke Bondi na Southern Highland (Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi) na Mapinduzi (Manispaa ya Iringa). 

Akiongelea mwongozo wa uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2014, Mwalimu Mnyikambi amesema kuwa nafasi zilizotengwa kwa shule za vipaji maalum kwa mkoa wa Iringa ni Mzumbe (6), Kibaha (7) kwa wavulana na Kilakala (8) na Msalato (5) kwa wasichana. Nafasi za shule za bweni zilizotengwa kwa mkoa wa Iringa ni Malangali (12) na Songea (9) kwa wavulana na Sekondari ya wasichana ya Iringa (9) na Mgugu (8) wasichana. Shule za ufundi ni Ifunda (15), Iyunga (10) wavulana na Tanga (2) wasichana.

=30=

Tuesday, December 17, 2013

PICHA ZA MATUKIO YA ZIARA YA KIMAMAMA WA KIKUNDI CHA SONGAMBELE KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA AMANI

Msafara wa kinamama wa kikundi cha Songambele walipowasili katika kituo cha kulelea watoto yatima cha AMANI, Wilayani Kilolo na kupokelewa na Mkuu wa Mkituo Mama Erica Mwakalebela (mwenye gauni la bluu)

Msafara wa kinamama wa kikundi cha Songambele walipowasili katika kituo cha kulelea watoto yatima cha AMANI, Wilayani Kilolo na kupokelewa na Mkuu wa Mkituo Mama Erica Mwakalebela (mwenye gauni la bluu)



Kinamama wa kikundi cha Songambele wakijihudumia chai baada ya kuwasili katika kituo cha Amani


Kinamama wa kikundi cha Songambele wakijihudumia chai baada ya kuwasili katika kituo cha Amani


Kinamama wa kikundi cha Songambele wakijihudumia chai baada ya kuwasili katika kituo cha Amani



Kinamama wa kikundi cha Songambele wakijihudumia chai baada ya kuwasili katika kituo cha Amani

Kinamama wa kikundi cha Songambele wakijihudumia chai baada ya kuwasili katika kituo cha Amani


Wanakikundi cha Songambele wakianza ziara ya kutembelea kituo cha Amani


Wanakikundi cha Songambele wakianza ziara ya kutembelea kituo cha Amani


Wanakikundi cha Songambele wakielekea kukagua stoo ya kituo cha Amani


Wanakikundi cha Songambele wakitembelea mashamba ya kituo cha Amani


                                                    Jiko la kituo cha Amani


Wakinamama wa Songambele wakicheza ngoma ya Kihehe maarufu kama KIDUO baada ya kuingia katika ukumbi wa Krefeld

Walimu wa Useremala katika kituo cha Amani wakiwa ndani ya Karakana kwa ajili ya kuwapokea kinamama wa Songambele walipotembelea Karakana hiyo


Mkuu wa kituo cha Amani Mama Erica Mwakalebela (katikati) akiwa katika karakana ya kituo cha Amani



Kinamama wa Songambele wakikagua Karakana ya Ushonaji katika kituo cha Amani

Wakinamama wa Songambele pamoja na walimu wa Karakana ya kituo cha Amani wakikagua mashamba ya kituo cha Amani

Kinamama wa Songambele wakikagua Karakana ya Ushonaji katika kituo cha Amani

Wakinamama wa Songambele muda mfupi baada ya kuingia katika ukumbi wa Krefeld kituoni Amani


Mama Baraka (kushoto) na Mama Stide (kulia) wakifuatilia burudani ya ngoma wa watoto wa kituo cha Amani hawapo pichani

Mama Baraka (kushoto) na Mama Stide (katikati) na Dkt. Maria wakifuatilia burudani ya ngoma wa watoto wa kituo cha Amani hawapo pichani

Wakinamama wa Songambele wakicheza ngoma ya Kihehe maarufu kama KIDUO baada ya kuingia katika ukumbi wa Krefeld


Wakinamama wa Songambele wakicheza ngoma ya Kihehe maarufu kama KIDUO baada ya kuingia katika ukumbi wa Krefeld


Mama Stide (kushoto) Dkt. Maria (katikati) na Mama Kifyasi (kulia) wakifuatilia Taarifa fupi ya kituo cha Amani toka kwa Mkuu wa kituo Mama Erica Mwakalebela hayupo pichani



Kinamama wa Songambele wakifuatilia Taarifa fupi ya kituo cha Amani toka kwa Mkuu wa kituo Mama Erica Mwakalebela hayupo pichani

Watoto wa kituo cha Amani wakiingia ukumbini kuburudisha kwa ngoma

Watoto wa kituo cha Amani wakitoa burudani


Walimu wa kituo cha Amani wakifuatilia burudani toka kwa watoto wa kituo hicho


Mama Mwalongo akiongea na watoto wa kituo cha Amani




Mama Mlawa akijitambulisha


Mama Mandela akijitambulisha

           Walimu wa kituo cha Amani wakifuatilia burudani toka kwa watoto wa kituo hicho


                                        Mama Mwalongo kijitambulisha




Baadhi ya zawadi toka kwa wanakikundi cha Songambele walizowapatia watoto wa kituo cha Amani



Baadhi ya zawadi toka kwa wanakikundi cha Songambele walizowapatia watoto wa kituo cha Amani

Baadhi ya zawadi toka kwa wanakikundi cha Songambele walizowapatia watoto wa kituo cha Amani


Baadhi ya zawadi toka kwa wanakikundi cha Songambele walizowapatia watoto wa kituo cha Amani


Mkuu wa kituo cha Amani, Mama Erica Mwakalebela akiwashukuru kinamama wa Songambele mmoja baada ya mwingine




Watoto wa Amani wakisaidiwa kunawa mikono kwa ajili ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na kinamama wa Songambele


Mwenyekiti wa kikundi cha Songambele, Mama Rehema Dunga (kushoto) na Mama Mandela (kulia) wakifanya maandalizi ya chakula



Mwenyekiti wa kikundi cha Songambele, Mama Rehema Dunga (kushoto) na Mama Mandela (katikati) na Dkt. Maria (kulia) wakifanya maandalizi ya chakula

Mwenyekiti wa kikundi cha Songambele, Mama Rehema Dunga akitoa baadhi ya maelekezo kwa ajili ya maandalizi ya chakula



                Kinamama wa kikundi cha Songambele wakiandaa sahani kwa ajili ya chakula



Maji na Juice








Kituo cha Amani


 



Watoto wa kituo cha Amani wakiwa katika foleni ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na kikundi cha Songambele


Watoto wa kituo cha Amani wakiwa katika foleni ya chakula cha mchana kilichoandaliwa na kikundi cha Songambele




Walimu wa kituo cha Amani wakipata chakula cha mchana kilichoandaliwa na kikundi cha Songambele



Walimu wa kituo cha Amani wakipata chakula cha mchana kilichoandaliwa na kikundi cha Songambele

Mama Mandela akibadilishana mawazo na mlezi wa kituo cha Amani





                             Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja

Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja


                              Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja





                           Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja






    Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja


    Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja





    Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja na walimu wa kituo cha Amani


    Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja baadhi ya watoto wa kituo cha Amani na walimu wao


                      Kinamama wa Songambele wakiwa katika pozi la pamoja




                 Mwenyekiti wa kikundi cha kimamama Songambele, Mama Erica Dunga


Kinamama wa Songambele wakiwa katika picha ya pamoja baadhi ya watoto wa kituo cha Amani na walimu wao


                          Kinamama wa Songambele wakiwa katika pozi la pamoja


                                                Wakati wa kupongezana




Mama Mlawa (kushoto) na Mama Mwalongo (kushoto) wakifurahia jambo


Mwenyekiti wa Songambele Mama Dunga na Makamu Mwenyekiti Mama Chonya akifurahia jambo