Tuesday, January 11, 2011

 HALMASHAURI ZAAGIZWA KUTENGA MAENEO YA MITI

Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Mji Mkoani Iringa zimeagizwa kutenga maeneo makubwa ya kupanda miti kwa faida ya Halmashauri husika na mkoa kwa ujumla kutokana na mkoa kuwa na hali nzuri ya hewa.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Georgina Bundala wakati akisoma hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika uzinduzi wa siku ya upandaji miti kimkoa uliofanyika katika Halmashauri ya mji wa Njombe.

Bundala amesema “nachukua nafasi hii kuziagiza Halmashauri zote za Mkoa huu zitenge maeneo makubwa kwa ajili ya kupanda miti kwa ajili ya faida ya Halmashauri husika”. Amesema mkoa wa Iringa una hali ya hewa nzuri inayofaa kwa zao la miti na kuwataka wananchi kutunza vizuri upendeleo huo mkoa uliojaaliwa na Mwenyezi Mungu ili kupiga hatua ya maendeleo.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Ludewa ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya njombe amesema kuwa mkoa wa Iringa una eneo kubwa la Misitu ya asili na ya kupanwa. Amefafanua kuwa Mkoa unamisitu ya hifadhi zaidi ya 64 yenye eneo la hekta zaidi ya 325,650. Vilevile amesema misitu ya kupandwa inaukubwa zaidi hekta 110,283 na kufafanua kuwa misitu hiyo ni pamoja na ile Halmashauri, vijiji, watu binafsi, makampuni na vikundi.

Wananchi wakiwa wamejiandaa vilivyo kushiriki zoezi zima la upandaji miti

Aidha, alichukua nafasi hiyo kuwataka wananchi kuendelea na zoezi la kuotesha miche na kuipanda, kuhifadhi ardhi kwa madhumuni ya kuzuia mmomonyoko wa ardhi, kuhifadhi misita ya asili na kuhifadhi vinazo vya maji.

Amesema uongozi wa mkoa umeamua siku ya upandaji miti kimkoa ifanyike tarehe 10 Januari, 2011 kwa kuwa hali ya hewa inaruhusu kwa zoezi hilo kwa mkoa mzima hivyo hauwezi kusubiri mpaka mwezi Aprili. Siku ya upandaji miti mwaka huu inaongozwa na ujumbe usemao MISITU NI UHAI; PANDA MITI KWANZA NDIPO UKATE MTI”.
“Ujumbe huu unatuasa tupande miti mingi sana na tukate mti mmoja na tukifanya hivyo tutafanikiwa kuhifadhi mazingira ya nchi yetu” amesema Bundala.

Akielezea takwimu amesema kuwa Mkoa wa Iringa ulipanda miti zaidi ya 6,603,296 katika Halmashauri zake katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari 2001 hadi Januari 2010. “Upandaji miti ni jambo muhimu sana, lakini muhimu zaidi ni kuitunza miti iliyopandwa. Haina maana kutumia nguvu zetu kuotesha na kupanda miti na kisha kuicha miti hiyo iungue moto au kuliwa na mifugo inayochungwa katika maeneo yaliyopandwa miti” Alisisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Aliagiza kuilinda miti hiyo kwa nguvu zote na pia ifanyike sensa ya miti ili kuwa na takwimu sahihi zinazoonyesha idadi ya miti iliyopona na iliyopo mashambani.

Shughuli  hii ya kupanda miti hufanyika kila mwaka hapa nchini kwa kuwashirikisha wananchi wa maeneo mbalimbali. Kwa kawaida siku ya upandaji miti kitaifa kila mwaka ilikuwa inafanyika tarehe mosi ya Mwezi Januari  lakini kuanzia mwaka jana 2010 shughuli ya upandaji miti  Kitaifa inafanyika Mwezi wa Aprili.



Tuesday, January 4, 2011




THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
PRIME MINISTER’S OFFICE
MINISTRY OF REGIONAL ADMINISTRATION AND
LOCAL GOVERNMENT


IRINGA REGION                                                         Regional Commissioner’s Office
Telephone no.  2702191                                                                                   
                                                                                                         P.O.Box 858
Fax no.   2702082                                                                            IRINGA

                                 
                                                                        1st January, 2011

Invitation for Tenders
For

Construction of Iringa Regional Commissioner’s Conference Facility – Phase I

Tender No. RAS/003/2010 – 2011/W/10


1.          This Invitation for Tenders follows the General Procurement Notice for these Projects which appeared in the Daily News Paper Issue No. ISSN 0856– 3812 NO. 10148  dated  30th August , 2010

2.     The Government of Tanzania has set aside funds for the operation of the Regional   
       Administrative Secretary - Iringa during the financial year 2010/2011. It is intended   
       that part of the proceeds of the fund will be used to cover eligible payment under the
       contract for Construction of Iringa Regional Commissioner’s Conference Facility –   
       Phase I

3.   The Regional Administrative Secretary - Iringa now invites sealed tenders from eligible
          “Nationalcontractors registered in Class Five and above for Construction of Iringa   
           Regional Commissioner’s Conference Facility – Phase I

            
  1. Tendering will be conducted through the National Competitive Tendering procedures specified in the Public Procurement (Goods, Works, Non Consultant Service and Disposal of Public Assets by Tender) Regulations, 2005 – Government

Notice No. 97 and is open to national Tenderers only as defined in the Regulations unless otherwise stated in the Tender Data Sheet.
5.      Interested eligible Tenderers may obtain further information from and inspect the Tendering Documents at the office of the Regional Tender Board Secretary, Regional Administrative Secretary, from 7.30a.m. to 3.30 p.m on Mondays to Fridays inclusive except on public holidays.
      P. O. Box 858,
          IRINGA

6.      A complete set of Tendering Document(s) in English language and additional sets may be purchased by interested Tenderers on the submission of a written application to the address given under paragraph 8 below and upon payment of a non-refundable fee of Fifty Thousands Shillings Only (Tshs. 50,000.00). Payment should be by Cash payable to the Regional Secretariat Cashier.

7.      All tenders must be accompanied by a tender securing declaration in the format provided in the tendering documents.

  1. All tenders in one original plus two (2) copies properly filled in, and enclosed in plain envelopes must be delivered to the Regional Administrative Secretary,
    P. O. Box 858
    , Iringa
    at or before 10.00p.m on Monday 31st January, 2011.
    Tenders will be opened promptly thereafter in public and in the presence of Tenderers’ representatives who choose to attend in the opening at the Regional Commissioner’s Conference Hall.

9.      Late tenders, portion of tenders, electronic tenders, tenders not received, tenders not opened and not read out in public at the tender opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstance.



Regional Administrative Secretary
IRINGA

Saturday, January 1, 2011

HOSPITALI YA MKOA IRINGA YAPONGEZWA

Hospitali ya Mkoa wa Iringa imepongezwa kwa kutoa huduma nzuri kwa wagonjwa wanaohudhuria hospitali hiyo kwa matibabu.

Pongezi hizo zimetolewa na Mbunge wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Ritta Semotto Kabati alipofanya ziara fupi ya kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika wodi ya akina mama na wodi ya watoto leo kwa lengo la kuwapa pole, na kuwatakia heri ya mwaka mpya 2011.
Mhe. Ritta Kabati, Mbunge wa CCM viti maalum (kulia) akimkabidhi baadhi ya zawadi
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Dkt. Oscar Gabone
katika viwanja vya Hospitali hiyo leo

Mhe. Kabati amesema “naipongeza hospitali ya mkoa wa Iringa kwa kutoa huduma nzuri na bora jambo linalowafanya wagonjwa kuridhika na huduma inayotolewa”. Ameongeza kuwa ametembelea hospitali mbalimbali lakini katika suala la usafi hospitali ya mkoa ipo juu.

Mhe. Kabati amesema lengo la kufanya ziara hiyo fupi ni kuwafariji na kuwatia moyo akina mama na watoto na kuwapa zawadi mbalimbali ikiwa ni pongezi zake kwa kufanikiwa kuuona mwaka mpya wa 2011.  “Nawapa pole sana wagonjwa wote na nawatakia afya njema kwani kuugua si kufa na pia naomba wote tuuanze huu mwaka mpya kwa furaha na uwajibikaji ili kuweza kujiletea maendeleo”.

Sikujua Filango, mama aliyejifungua mtoto saa tisa usiku wa tarehe 01.01.2011 ameelezea kurithishwa na huduma za hospitalini hapo tangu alipowasili hadi alipojifungua.

Akielezea changamoto zinazoikabili hospitali ya mkoa, Katibu wa Hospitali, Dotto Zambalesi amesema kuwa hospitali hiyo inakabiliwa na upungufu wa watumishi wenye taaluma stahiki akidai waliopo kuwa ni wachache hatimae kuwa na jukumu zito kidogo kwa wataalamu waliopo kuweza kuziba pengo la watumishi wanaopungua. Aidha changamoto nyingine ameiongelea kuwa ni ufinyu wa bajeti jambo linalokwamisha ufanisi katika baadhi ya shughuli.

Mhe. Rita Kabati Mbunge viti maalum CCM (katikati) akiwa na
mama Felisha (kushoto) na mama ambaye mtoto hajampatia jina (kulia)
baada ya kuwakabidhi zawadi alipotembelea wodi ya akina mama leo

Akitoa shukrani zake kwa ziara hiyo mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Oscar Gabone amemshukuru Mhe. Mbunge na msafara wake na zawadi walizozitoa katika wodi ya akina mama na wodi ya watoto na kueleza matumaini yake kuwa ziara ijayo itahusisha zawadi za akina baba pia.

Katika ziara hiyo Mbunge huyo aliambatana na akina mamawa UWT mkoa na wilaya na baadhi ya waheshimiwa madiwani na kutoa zawadi za sabuni, maziwa, juice na biskuti pamoja na vitu vingine.


Baadhi ya wajumbe katika ziara ya Mhe. Kabati wakibadilishana mawazo na viongozi wa Hospitali ya Mkoa
WANANCHI WATAKIWA KUTAFAKARI CHANGAMOTO ZA KIJAMII

Serikali mkoani Iringa imetoa wito kwa waumini na wananchi kutafakari changamoto zilizojitokeza katika jamii na kusababisha uvunjaji wa amani na mshikamano katika kuukaribisha mwaka mpya 2011.

Kauli hiyo imetolewa na kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kanali Issa Machibya katika hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bibi. Evarista Kalalu katika mkesha mkubwa wa kitaifa uliofanyika katika uwanja wa Samora uliopo katika Manispaa ya Iringa.



       Askofu Dkt. Oderdenburg Mdegela akiteta jambo la Mwakilishi wa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bibi. Evarista Kalalu. 
Bibi Kalalu amesema “natoa wito kwa waumini na wananchi wote kwamba tunapoukaribisha mwaka mpya, kila mmoja wetu atafakari ni mambo gain au changamoto zipi zilizojitokeza katika jamii na kusababisha uvunjifu wa amani na mshikamano wetu”. Amezitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na rushwa, mauaji ya walemavu wa ngozi (Albino), ubakaji, utoaji mamba, mauaji ya vikongwe na mauaji ya watu yanayoendelea kujitokeza.

Aidha, amesema kuwa changamoto hizo zimesababishwa na mmomonyoko wa maadili katika jamii na kusisitiza kuwa waumini wa dini zote na madhehebu yote kuweka nguvu katika kuliombea taifa liepukane na mmomonyoko wa maadili. Amewataka kila mmoja kuwa mwalimu wa kutenda matendo mema yenye kumpendeza Mungu na kuendelea kudumisha amani iliyopo.

Vilevile amewataka waumini wote kuwaombea viongozi wa taifa kwa Mungu ili hekima, busara na ujasiri wa kutawala kwa moyo wa uadilifu. Ameongeza kuwa kila mwanajamii kwa nafasi yake awajibike katika kuleta maendeleo yake binafsi, kudumisha amani, mshikamano na maadili mema katika jami nzima.

Katika neno la utangulizi lililotolewa na Mhashamu Baba Askofu Dr.Oderdenburg Mdegela amesema dhumuni la mkesha huo ni kuiombea nchi ili iwe na amani, “tumekuja kuomba na kutembea pamoja ili nchi iwe na amani”. Amesema kuwa toba ni msingi wa kumkaribia Mungu na Mungu huleta mabadiliko katika familia, kazi, biashara na Taifa. Amesema kuwa mkesha huo ni mafuriko na utamfunika kila mtu katika kutenda mema. Aidha, aliwashukuru wale wote waliohusika kuruhusu uhuru wa kuabudu nchini pasipo kuvunja sheria.

Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Iringa wakipokea
baraka kavika uwanja wa Samora mkesha wa mwaka 2011



...MAISHA BORA YANATOKANA NA KUFANYA KAZI KWA JUHUDI NA MAARIFA!

Wananchi wamekumbushwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili kujiletea maisha bora na si kutegemea kuwa maisha mazuri yanateremka kutoka juu.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bibi Evarista Kalalu katika hafla fupi ya kukabidhi mkopo wa zana za kilimo trekta kubwa manane na ndogo 25 uliotolewa na Idodi SACCOS iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Idodi SACCOS zilizopo katika Kata ya Idodi, Tarafa ya Idodi katika  Halmashauri ya Iringa.
Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bibi. Evarista Kalalu akikabidhi mkopo wa Trekta

Bibi Kalalu amesema kuwa maisha rahasi kwa jamii yanatengenezwa kwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa na si kukaa na kusubiri muujiza kutoka juu. Ameongeza kuwa vijana wengi wamekimbilia maisha wanayodhani ni rahisi hasa mijini na kujikuta wanaharibikiwa na kupoteza muelekeo hivyo kuagiza vijana washawishiwe kutokimbilia maisha hayo na wajiingize katika kilimo na vyama vya ushirika wa akiba na mikopo (SACCOS). Ametanabaisha kuwa usalama wa Tarafa ya Idodi na Mkoa wa Iringa utatokana na kushawishiwa huko kwa vijana kufanya kazi mbalimbali na si kupoteza muda na muelekeo katika maisha.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Iringa ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi amefafanua madhumuni ya kuanzisha vyama vya ushirika vya akiba na mikopo (SACCOS) mwanzoni mwa miaka ya 2000 kuwa ni mkakati wa serikali kuwakomboa wananchi wake. Amesema “nguvu za wananchi zikiwekwa pamoja kwa malengo mahususi unakuwa ni mtaji mkubwa sana” hivyo kuwataka wananchi wengi zaidi kujiunga katika vyama vya akiba na mikopo ili kuunganisha nguvu zao. Amesema “wanaidodi wengine wasio wanachama wawe tayari kujifunza na kujiunga kutoka SACCOS”.

Alichukua nafasi hiyo kuzitaka kata nyingine kubuni bidhaa nyingine isiyopatikana katika Kata ya Idodi ili kuongeza wigo wa utoaji huduma katika Tarafa mzima ya Idodi jambo litakalodumisha ushirikiano na udugu.  

Afisa Kilimo, Mifugo na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Lucy Nyallu amesema kuwa kilimo cha kisasa hakitegemei kubahatisha bali kinategemea matumizi sahihi ya mbolea, uchaguzi wa mbegu bora na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa kilimo.

Mwenyekiti wa SACCOS hiyo Ngoola Mwangosi amezitaja changamoto zinazoikabili SACCOS hiyo kuwa ni pamoja na wadau wa mikopo ya stakabadhi mazao kutotoa mikopo ya kukopesha kwa wakati, na baadhi ya wanancha kutorejesha mikopo kwa wakati. Ameitaja changamoto nyingine kuwa ni wananchama kutokuwa na zana za kisasa za kilimo na kusababisha uzalishaji duni.

Chama cha ushirika wa akiba na mikopo (Idodi SACCOS DYK) kilisajiliwa rasmi Disemba, 2004 kikiwa na wanachama 178 na vikundi vya wajasiliamali sita kikiwa na hisa zenye thamani ya Tsh. 3,600,000, akiba Tsh. 107,286,400 na amana Tsh. 7,200,000.