Wednesday, October 19, 2011

WELLINGTON HARRISON TURNER GONDWE-Jr


Wellington Harrison Turner Gondwe, alizaliwa tarehe 11 Oktoba, 1987 mjini Morogoro.

Alibatizwa mwaka 1990 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Usharika wa Bugando na alipata Kipaimara mwaka 2001 katika Usharika huohuo.

Alijiunga na shule ya msingi Mlimani mwaka 1994 na kuhitimu darasa la Saba katika Shule ya Msingi ya Lake mwaka 2002.
Aidha, alijiunga na Shule ya Sekondari ya Murutunguru iliyopo Wilayani Ukerewe mwaka 2003 hadi Juni, 2004.

Baada ya hapo alihamia katika Shule ya Sekondari ya Thaqaafa Julai, 2004- 2006. Kutokana na ugonjwa hakuweza kufanya mitihani yake ya kidato cha Nne iliyotarajiwa kuanza 22 Oktoba, 2006.

Wellington alianza kuugua Malaria kali tarehe 3 Oktoba, 2006. Aidha, alilazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando tarehe 10 Oktoba, 2006.

Pamoja na jitihada za Madaktari za kunusuru maisha yake kushindikana na roho kushindana na mauti, alifariki tarehe 20 Oktoba, 2006 saa 12 kamili jioni.

BWANA alitoa na BWANA ametwaa jina lake lihimidiwe.


WATUMISHI WA UMMA NA HUDUMA BORA


Watumishi wa Umma wamekumbushwa kuendelea kutoa huduma bora kwa jamii na kuhakikisha jamii inaridhika na huduma hiyo pamoja na changamoto zilizopo.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alipokuwa akiongea na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. George Masaju (kulia) akiongea na wafanyakazi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Iringa hawapo pichani na Kaimu mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bw. Aseri Msangi (kushoto)
Masaju amesema “tunatambua kuwa sisi ni watumishi wa Umma na tuna maadili yetu ya kazi kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 na mabadiliko yake Na. 17 ya mwaka 2007”. Amesema kwa msingi huo wa utumishi wetu wa Umma “sote kwa pamoja lazima huduma zetu tuzitoe kwa ubora na kwa viwango vya kuridhisha kwa Umma”.
Amesema “nawajibika kuwakumbusha wajibu wetu sote kwa Serikali na tukumbuke kuwa sisi ndio watendaji wa kuwasaidia viongozi wetu wa juu”.
Aidha, amewakumbusha kuwa wafanyakazi katika ngazi za mikoa na Halmashauri ndio walio karibu zaidi na wananchi hivyo wanawajibika kufanya kazi kwa uwezo wao na viwango kwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema utoaji wa huduma bora kwa wananchi unasaidia katika kuondoa kero na kupunguza malalamiko ya wananchi dhidi ya Serikali yao.
Akisisitiza dhana ya ubora wa huduma kwa wananchi, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa ubora huo ujikite katika utoaji wa maamuzi sahihi na yanayotolewa katika muda muafaka.
Ametolea mfano wa huduma zikitolewa vizuri katika idara ya polisi na mahakama kutasaidia kupunguza uhalifu.
Vilevile, amesisitiza kuwa jukumu la kudhibiti uhalifu nchini si la idara ya polisi na mahakama pekee bali ni jukumu linalohitaji msukumo wa pamoja baina ya mamlaka zinazohusika na wananchi kwa umoja wao.