Wednesday, October 19, 2011

WELLINGTON HARRISON TURNER GONDWE-Jr


Wellington Harrison Turner Gondwe, alizaliwa tarehe 11 Oktoba, 1987 mjini Morogoro.

Alibatizwa mwaka 1990 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Usharika wa Bugando na alipata Kipaimara mwaka 2001 katika Usharika huohuo.

Alijiunga na shule ya msingi Mlimani mwaka 1994 na kuhitimu darasa la Saba katika Shule ya Msingi ya Lake mwaka 2002.
Aidha, alijiunga na Shule ya Sekondari ya Murutunguru iliyopo Wilayani Ukerewe mwaka 2003 hadi Juni, 2004.

Baada ya hapo alihamia katika Shule ya Sekondari ya Thaqaafa Julai, 2004- 2006. Kutokana na ugonjwa hakuweza kufanya mitihani yake ya kidato cha Nne iliyotarajiwa kuanza 22 Oktoba, 2006.

Wellington alianza kuugua Malaria kali tarehe 3 Oktoba, 2006. Aidha, alilazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando tarehe 10 Oktoba, 2006.

Pamoja na jitihada za Madaktari za kunusuru maisha yake kushindikana na roho kushindana na mauti, alifariki tarehe 20 Oktoba, 2006 saa 12 kamili jioni.

BWANA alitoa na BWANA ametwaa jina lake lihimidiwe.


No comments:

Post a Comment