Wednesday, October 31, 2012




Aga Khan Health Services Resumes Delivery Services at Iringa Primary medical Center.
Aga Khan Health services Iringa has resumed delivery services and has registered its first delivery today morning.

Speaking with Daily news in an exclusive interview the Joining Hands Initiative project manager Anitah Muruve said that both the mother and the baby are in good condition. She said the delivery services have been established under Joining Hands: Improving Maternal, Newborn and Child Health (JHI) Project which is a Canadian International Development Agency (CIDA) funded initiative that aims to contribute to improved reproductive and maternal, newborn and child health (MNCH) in fifteen districts across five target regions in Tanzania.
 Kerstin Scheffler with her new new baby (cetre)

Kerstin Scheffler with her new new baby (cetre)

Maruve said that the project is focusing on improving quality of and access to maternal, newborn and child health services; increasing utilization of MNCH service at primary care level.

The project manager added that the project objectives are improving maternal, newborn and child health practices through behaviour change communication (BCC) and health promotion (HP)  and enhancing knowledge transfer and exchange on maternal, newborn and child health  through a strong public private partnership (PPP) approach under which the project is being implemented. The delivery services are open to the public. 

The Aga Khan Health Services Tanzania will continue to establish deliveries in its other health facilities in Mwanza, Dodoma, Mbeya and Morogoro regions.
Speaking on the services received, the mother of the new born baby Kerstin Scheffler said she has enjoyed and appreciate the services offered throughout she has been at the centre.

Veronica James, The Iringa Aga Khan hospital, Manager said her centre is keeping on improving her services in order to offer better health care services to the people. She further, calls upon people to go for better maternal and child health.

The project has got three phases as project implementation planning (PIP), inception and implementation.
=30=
MTOTO WA KWANZA AZALIWA HOSPITALI YA AGA KHAN-IRINGA


Hospitali ya Aga Khan imefanikia kuanzisha huduma ya kuboresha afya ya mama mjamzito na mtoto kwa kupitia mradi wake wa Tuunganishe mikono pamoja na mwanamke wa kwanza mjamzito amefanikiwa kujifungua salama asubuhi ya leo.

Baba mzazi wa mtoto aliyezaliwa leo hospitali ya Aga Khan Said Gallos Mlewa (kushoto) akiwa na familia yake.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kukabidhi zawadi kwa niaba ya jamuiya ya Aga Khan mkoa wa Iringa, Meneja wa hospitali ya Aga Khan-Iringa, Veronica James amesema “leo imekuwa ni siku ya furaha sana kwa hospitali ya Aga Khan na kwa wananchi wa manispaa ya Iringa na vitongoji vyake kutokana na huduma za kujifungua kwa mama mjamzito wa kwanza hospitalini hapa”.

Akielezea malengo ya mradi wa Tuunganishe nikono pamoja Veronica amesema kuwa mradi huo unalenga kuwasogezea wananchi huduma karibu na kwa ubora unaotakiwa kwa kupunguza foleni kwa wanawake wajawazito katika vituo vingine vinavyotoa huduma ya mama wajawazito na kujifungua kwa lengo la kuwapunguzia hadha wajawazito hao.

Meneja wa hospitali ya Aga Khan iringa amesema kuwa mradi huo unalenga kuongeza kiwango na matumizi ya huduma ya afya ya mama mjamzito na watoto nchini. Amesema kuwa mradi huo pia unalenga kuboresha kiwango cha upatikanaji wa huduma ya afya ya mama mjamzito na watoto. Malengo mengine ameyataja kuwa ni pamoja na kuboresha huduma ya afya yam ma mjamzito na watoto katika jamii na kushirikiana na kujifunza kuhusu afya ya mama mjamzito na watoto.

Akielezea furaha yake mama mzazi Kerstin Scheffler (38) amesema kuwa amefurahishwa na huduma katika hospitali hiyo kwa kipindi chote alichokuwa hospitalini hapo kutoka kwa madaktari na wauguzi. Mama huyo aliyejifungua mtoto wake wa tatu leo na kupewa jina la Malaika Lina ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuzitumia huduma za afya ya mama mjamzito na mtoto katika hospitali hiyo ili waweze kunufaika vizuri.
Katika maelezo yake ya jumla Daktari mfawidhi wa hospitali ya Aga Khan Iringa, Dkt. Jumaa Mbete amesema mama huyo amejifungua salama majira ya saa 3:25 asubuhi hospitali hapo na mtoto akiwa na uzito wa kilo 3.3.

Dkt. Mbete amesema kuwa lengo la hospitali yake ni kusaidiana na serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuimarisha huduma ya afya ya mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano nchini.

Akiongelea gharama, Daktari mfawidhi amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakihofia gharama katika hospitali yake jambo ambalo si kweli. Amesema kuwa gharama ni ndogo sana akitolea mfano wa gharama kwa mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano kuwa huduma ni bure. Amesema kuwa katika hospitali hiyo huduma hiyo hutolewa kwa masaa 24 na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza na kunufaika na huduma hiyo.

Mradi wa Tuunganishe mikono pamoja ni mradi wa miaka mitatu ukiendeshwa katika mikoa ya iringa, Dodoma, Mwanza, Mbeya na Morogoro na mashika yanayotekeleza mradi huo Mfuko wa Aga Khan, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, shirika la misaada ya maendeleo la Canada na chuo kikuu cha Aga Khan.

Wednesday, October 24, 2012


Obama and Romney in final push

 
Barack Obama (left) and Mitt Romney in Boca Raton, Florida 22 October 2012 
Europe did not get a mention in the third presidential debate on foreign policy

US President Barack Obama had the best lines, but perhaps Republican presidential challenger Mitt Romney had the best night.

Not in the sense that he won the debate - it was a draw if you have to judge these things that way.
But Mr Romney pivoted to President Peaceful and stomped on any suggestion he would take America into new foreign wars.
He didn't make any of the errors he had made in the past or say anything demonstrably silly. He said he would keep to Mr Obama's policy of withdrawing troops from Afghanistan by 2014 and agreed that sanctions against Iran were working. As one tweeter put it, his policy seemed to be "speak louder, and carry the same stick".
But Mr Obama was firm - and funny. He undermined Mr Romney's alarm that America had fewer ships than in 1916 by saying that it had fewer bayonets and horses as well. He said the 1980s were calling because they wanted their foreign policy back.
He didn't play the indignant and offended president, which I had expected him to do, but he did set out his achievements calmly and clearly.
Both men repeatedly tried to talk about the economy, which they know is of more concern to most Americans than what happens abroad.
The debate was depressing in that foreign policy seemed pretty much to equal the Middle East. Israel must have been mentioned dozens of times.
China got a brief look-in, in the last quarter of an hour, but mainly as a trade rival. I didn't hear Europe mentioned at all.
This final debate probably won't shift the opinion polls, but it saw a marked change in emphasis in Mr Romney's foreign policy.
That is a danger for him, in that it resurrects the old flip-flopping charge. But it also suggests a new confidence, that he has to convince people he is safe enough to entrust with the presidency.

From BBC NEWS

Tuesday, October 23, 2012

MKOA WA IRINGA WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA RUBADA




Mkuu wa Mkoa wa Iringa ametoa wito kwa viongozi wa mkoa wake kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mamlaka ya uendelezaji wa bonde la mto Rufiji (RUBADA) ili kuwawezesha kuratibu na kusimamia vizuri mipango kabanbe ya kuendeleza shughuliza kilimo kwa ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT).

Katika hotuba ya ufunguzi wa kikao cha viongozi na wataalamu wa mkoa wa Iringa kuhusu uendelezaji wa SAGCOT uliofanyika katika ukumbi wa VETA mjini Iringa iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Christine Ishengoma.

Mgeni rasmi Gerald Guninita ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Kilolo (katikati) akisoma hotuba wakati wa ufunguzi wa kikao cha viongozi na wataalamu wa mkoa wa Iringa kuhusu uendelezaji wa SAGCOT


wajumbe wa kikao cha viongozi na wataalamu wa mkoa wa Iringa kuhusu uendelezaji wa wa SAGCOT 


Amesema RUBADA imepewa majukumu ya kusimamia na kuratibu mipango ya SAGCOT ili malengo ya mipango hiyo yaweze kutekelezwa vizuri na kuinua hali ya wananchi nchini. Amesema katika kufanikisha hili RUBADA inatafuta na kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji wa kilimo chenye tija na viwanda kwa lengo la kuleta mapinduzi ya kijani. Amesema katika hilo RUBADA kwa kushirikiana na wilaya husika itaandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji ili maeneo ya uwekezaji yabainishwe na kutengwa kwa ajili ya wawekezaji watakayoyaendeleza pamoja na wakulima wadogo wadogo wanaoyazunguka maeneo ya miradi hiyo.

Guninita amesema kwa kuzingatia kazi nzuri inayofanywa na RUBADA katika kutekeleza mipango hiyo, ushirikiano wa viongozi na wataalamu hao ni chachu katika ufanikishaji wa malengo hayo. Ameelezea matarajio yake kwa viongozi na wataalamu hao baada ya kikao hicho kuwa watakuwa mabalozi wazuri wa kuwaelimisha wananchi katika maeneo yao ili wawe washiriki wazuri katika kutekeleza mpango huo.

Akiwasilisha mpango wa SAGCOT Mkurugenzi Mkuu wa uendeshaji wa bonde la Rufiji, Aloyce Masanja amesema kuwa hakuna nchi iliyofanikiwa duniani kuichumi na kuondokana na umasikini pasipo mapinduzi ya kilimo na viwanda. Akiongelea takwimu, amesema kuwa asilimia 65 ya malighafi za viwanda zinatokana na kilimo wakati asilimia zaidi ya 55 ya mfumuko wa bei huchangiwa na mazao ya kilimo. Amesema katika hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo ni asilimia 23 pekee ndiyo zimetumika.
Akiongelea tofauti kati ya kilimo kwanza na sera nyingine zilizopita, Masanja amesema kuwa mipango na jitihada za zamani ziliibuliwa, kupangwa na kutekelezwa na serikali na mashirika yake pasipo kuwahusisha wadau wengine kikamilifu. Amesema tofauti na mipango ya awali kilimo kwanza ni mtazamo mpana wa mabadiliko ya kisekta na uzoefu uliopatikana kutokana na mipango iliyotekelezwa hapo awali na sasa kilimo kwanza kimeshirikisha wadau wote.   

Mkurugenzi Mkuu wa uendeshaji wa bonde la Rufiji ameyataja malengo ya SAGCOT kuwa ni kutatua matatizo yanayoikabili sekta ya kilimo hasa upatikanaji wa mitaji, vyama vya wakulima, miundombinu ya kilimo, uharibifu wa mazingira, ukosefu wa masoko, uwekezaji mdogo katika kilimo na uboreshaji wa sera zinazohusu kilimo. Amesema malengo mengine ni kuwahamasisha wakulima wadogo na kuwaunganisha katika vikundi na kuwafanya walime kilimo cha kibiashara.

Masanja amesema kuwa RUBADA imekuwa pia ikiwapa kipaumbele vijana katika shughuli mbalimbali za kujiongezea kipato. Amesema “kila tunapoanzisha miradi ya RUBADA tunakuwa tukianzisha kambi za vijana ambapo tunawafundisha mbinu bora za kilimo na matumizi ya dhana za kilimo” amesisitiza Masanja.

=30=









Sunday, October 7, 2012

MAONESHO YA ASALI DAR














SENJE AHIMIZA VIFUNGASHIO KATIKA BIDHAA





Halmashauri nchini zimeshauriwa kulipa kipaumbele suala la vifungashio katika mazao ya nyuki ili kutoa taarifa sahihi kwa mlaji.

Ushauri huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Immaculte Senje alipokuwa alitoa tathmini yake juu ya changamoto wanazokabiliana nazo katika kufikisha asali sokoni muda mfupi baada ya kutembelea mabanda ya Halmashauri katika maonesho ya kitaifa ya mazao ya nyuki yajulikanayo kama ‘Dar es Salaam Honey Exhibition’ yanayoendelea katika uwanja wa maonesho ya biashara ya Mwl. Julius Nyerere, barabara ya kilwa.

Senje amesema kuwa mabanda mengi aliyotembelea yanakabiliwa na changamoto ya vifungashio. Amesema “nadhani umefika wakati kwa Halmashauri zetu kulipa uzito suala la vifungashio katika mazao ya nyuki ili kuweza kuendana na uhalisia wa soko”. Amesema umuhimu wa vifungashio katika mazao ya nyuki hasa asali, unamuwezesha mlaji kupata taarifa kamili juu ya bidhaa anayoitumia na kiwango cha ubora wake.
Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji Makao Makuu, Al-Haji M. Batenga alipotembelea banda la Manispaa ya Iringa katika Maonesho ya Asali

Mjasiliamali Msafiri Chengula kutoka kikundi cha Anamed chenye mizinga zaidi ya 200 katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa amesema kuwa changamoto wanayoipata ni uuzaji asali kwa njia ya lejaleja, jambo linalowasababishia tatizo katika kuhifadhi fedha na kuzipangia matumizi sababu fedha hizo hazikai. Amesema kuwa uchomaji misiti umekuwa ukiathili sana utengenezaji wa asali sababu nyuki wamekuwa wakikimbia au kuungua. Changamoto nyingine ameitaja kuwa ni tabia ya wizi wa asali katika kipindi cha uvunaji ambacho kwa wilaya ya Iringa amekitaja kuwa ni kati ya miezi ya Mei hadi Julai kutokana na ukame hali inayowalazimisha walinaji kuhamia msituni wakati huo.

Changamoto ya vifungashio pia linaikumba Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa mujibu wa Afisa Misitu wa Msaidizi, Enock Changime, amesema “sehemu ya kuhifadhia asili asali ili iweze kuingia sokoni kwa maana ya vifungashio ni tatizo kwa sababu vifungshio vingi vinatoka nchi ya Kenya”.

Changime amesema kuwa changomoto nyingine ni udogo wa mwamko wa jamii katika suala la ufugaji nyuki. Amesema manispaa ya Iringa imekuwa ikihamasisha  jamii kujiunga katika vikundi na kuvipa mafunzo juu ya ufugaji nyuki sambamba na na misaada ya mizinga ya kuanzia ufugaji huo. 

Amesema kutikana na changamoto ya uhaba wa wataalamu, Manispaa ya Iringa imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na sna na Halmashauri ya wilaya ya Iringa katika kuunganisha nguvu ya rasilimali wataalamu ili kuweza kukuza sekta ya nyuki katika halmashauri hizo.

Akiongelea umuhimu wa vifungashio katika kukuza soko la bidhaa nchini, Kaimu Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano kutoka Wakala wa Vipimo nchini Irene John amesema ili bidhaa iweze kutambulika ndani na nje ya nchi suala la vifungishio sahihi ni muhimu sana. Amesema kuwa ni vema kuyapa uzito unaoshahili mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa ufungashaji bidhaa za mazao ya nyuki, ameyataja mambo hayo kuwa ni masharti kuwa ni kuandika maelezo na kiasi cha ufungashaji. Mengine ameyataja kuwa ni uzuiaji wa ufungashaji wenye udanganyifu na uthibiti wa vipimo.

Maonesho ya kitaifa ya mazao ya nyuki yalianza katika uwanja wa maonesho ya biashara wa Mwl. Julius Nyerere tarehe 4-7 Oktoba, 2012 na yalitanguliwa na kongamano la kitaifa la wadau wa sekya ya asali kutokana na agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda.
=30=