Monday, September 19, 2011

 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mteule Mhe. Dkt. Christine Ishengoma anatarajiwa kuwasili kesho katika kituo chake kipya cha kazi (Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa) .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa watu wote na kubandikwa katika mbao za matangazo katika Ofisi hiyo kutoka Sehemu ya Utawala inasema kuwa mteule huyo atawasili majira ya saa tano asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki.

Aidha, watumishi wote katika Ofisi hiyo wametakiwa kujitokeza muda huo ili kumlaki.

Mtandao wa www.dennisgondwe.blogspot.com unamtakia kila la kheri katika kituo chake kipya ukiamini KAZI KWANZA KATIKA KUIJENGA IRINGA YENYE NEEMA TELE