Sunday, August 26, 2012

VYOMBA VYA HABARI VYATAKIWA KUENDELEA KUHAMASISHA SENSA




Vyombo vya habari Mkoani Iringa vimeshauriwa kuendelea kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ili liweze kufanikiwa katika Mkoa wa Iringa na taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma muda mfupi baada ya kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi lililoanza usiku wa Kuamkia leo nchini kote.
Dkt. Christine amesema kuwa zoezi hilo vimeanza vizuri na mdadisi ameonekana kubobea katika kazi hiyo. Aidha, amewamwagia sifa wakufunzi na wadadasi kwa jinsi walivyoonesha juhudi katika kufundisha na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu uelewa wa zoezi zima la Sensa ya Watu na Makazi.
 Dr. Christine Gabriel Ishengoma, Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa Mkoa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Sensa ya Mkoa amevipongeza vyombo vya habari vya Mkoa wa Iringa kwa weledi katika kuhamasisha zoezi hili. Amesema uhamasishaji ni muhimu sana katika kutoa hamasa kwa kazi ya Sensa ili asitokee mtu ambaye atakuwa hakupata taarifa na elimu juu ya umuhimu wa Sensa na kuhesabiwa. Aidha, ametoa wito kwa vyombo hivyo kuendelea na uhamasishaji huo kwa kipindi cha wiki nzima ili kulifanikisha zoezi hili katika Mkoa wa Iringa. “kufanikiwa kwa zoezi hili Mkoani Iringa sit u kutakuwa na manufaa kwa Mkoa wetu, bali kwa nchi nzima na jambo hili litafikiwa pale tu wananchi wote watakapokuwa wameelewa umuhimu wa zoezi hili na kushiriki katika kulifanikisha” alisisitiza Dkt. Christine.

Akiongelea matukio yasiyo ya kawaida katika zoezi hili, Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa Mkoa wa Iringa amesema kuwa zoezi hilo limeanza katika hali ya utulivu mkubwa na hakuna tukio lolote lisilo la kawaida lililotokea na kuripotiwa. Aidha, amewata wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa makarani wa Sensa pindi watakapopita katika maeneo yao na kujibu kwa usahihi maswali watakayokuwa wakiulizwa.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka, akitoa maoni yake baada ya kuhesabiwa asubuhi ya leo amesema kuwa kazi ya kuhesabu na kuhesabiwa ni jukumu la kila mtanzania pasipo kujali mipaka ya aina yoyote. Amesema kila mtanzania anayo haki ya kuhesabiwa katika Sensa hii ili kuhakikisha Serikali yake inapata taarifa sahihi kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo kwa wananchi wake.
Mpaka amesema “miongoni mwa michango ya wananchi katika jitihada za kujiletea maendelea kwa kushirikiana na Serikali yao ni pamoja na kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka huu”. Amesema zipo njia mbalimbali za kushiriki katika shughuli za maendeleo katika kipindi hiki kutoa taarifa sahihi ni jukumu namba moja ili kuiwezesha Serikali kupata takwimu sahihi. 

Sensa ya Watu na Makazi inafanyika kwa mara ya tano nchini ikiongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Sensa kwa Maendeleo, jiandae kuhesabiwa’ ipo katika siku yake ya kwanza nchini kote na itaendelea kwa siku saba ili kuhakikisha kila mwananchi anahesabiwa mara moja tu.
=30=

SENSA YAANZA VIZURI MUFINDI



Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi Wilayani Mufindi limeanza kwa hali ya utulivu mkubwa na wananchi wameendelea kutoa ushirikiano mkubwa katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa.

Akiongea katika mahojiano maalumu na na gazeti la Uhuru, Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa wilaya ya Mufindi, Evarista Kalalu amesema kuwa katika siku ya kwanza ya Sensa ya Watu na Makazi Wilayani Mufindi, “kwa kweli zoezi hili lilianza saa sita kamili usiku katika maeneo ambayo si ya makazi ya kudumu, kazi ilifanyika katika Mji wa Mafinga katika maeneo ya stendi, nyumba za kulala wageni na maeneo yanapopaki magari makubwa ya mizigo. Aidha, zoezi kama hilo lilifanyika pia katika maeneo ya Nyololo, Igowole, Kibao, Malangali, Ihowanza, Mgololo na Usokami hadi asubuhi saa kumi na moja kazi hiyo ilikuwa imekamilika kwa mafanikio makubwa”. Amesema kuwa leo asubuhi pamoja na kuanza zoezi kwenye makazi ya watu, wagonjwa waliolazwa kwenye vituo vyote vya huduma wamehesabiwa asubuhi na zoezi linaendelea kwenye makazi ya kudumu ya watu.

Akiongelea tathmini yake, amesema kuwa kazi ya kuhesabu watu inaendelea vizuri sana na muitikio wa watu ni mkubwa sana katika zoezi hilo. Amesema ukubwa wa muitikio wa watu katika wilaya yake unatokana uhamasishaji mkubwa unaoendelea kufanyika na kiu kubwa waliyonayo wananchi ya kushirikiana na Serikali katika kujiletea maendeleo.

Evarista ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi amesema kuwa ili zoezi hilo liweze kufanikiwa kwa asilimia 100, viongozi na jamii kwa ujumla hawana budi kuendelea kutoa hamasa na elimu ili wananchi wote waweze kushiriki kikamilifu katika upatikanaji wa takwimu hizo muhimu kwa mustakabali wa taifa. Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa makarani wa Sensa wanaoendelea kupita katika kaya zao kukusanya taarifa mbalimbali. Amesema wananchi watakapo jibu kwa usahihi maswali watakayoulizwa na makarani wa Sensa watakuwa wametimiza wajibu wao wa kushiriki katika kupanga mipango ya maendeleo yao kwa namna moja ama nyingine.

Katika mahojiano kwa njia ya simu na Mratibu wa Sensa Mkoa wa Iringa, Fabian Fundi amesema, “kwa ujumla zoezi hili linaenda vizuri na tulianza saa sita usiku na kuendelea nalo hadi alfajiri. Na asubuhi hii tumeanza kuhesabu kaya binafsi ambazo ni makazi ya kudumu ya watu”. Amesema kuwa kamati ya Sensa Mkoa haijapata taarifa wala matukio yasiyo ya kawaida wala kupokea simu yoyote kutoka kwa makarani kutaarifu kuwa kuna mtu au kaya iliyogoma kuhesabiwa, hii ni dalili nzuri kuwa zoezi hili litakuwa la mafanikio katika Mkoa wa Iringa.

Sensa ya Watu na Makazi inafanyika kwa mara ya tano nchini kote ikiongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Sensa kwa Maendeleo: Jiandae kuhesabiwa’ ipo katika siku yake ya kwanza na itaendelea kwa siku saba ili kuhakikisha kila mwananchi anahesabiwa mara moja tu.
=30=

VYOMBO VYA HABARI IRINGA VYATAKIWA KUENDELEA KUHAMASISHA SENSA



Vyombo vya habari Mkoani Iringa vimeshauriwa kuendelea kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ili liweze kufanikiwa katika Mkoa wa Iringa na taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma muda mfupi baada ya kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi lililoanza usiku wa Kuamkia leo nchini kote.
Dkt. Christine amesema kuwa zoezi hilo vimeanza vizuri na mdadisi ameonekana kubobea katika kazi hiyo. Aidha, amewamwagia sifa wakufunzi na wadadasi kwa jinsi walivyoonesha juhudi katika kufundisha na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu uelewa wa zoezi zima la Sensa ya Watu na Makazi.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Sensa ya Mkoa amevipongeza vyombo vya habari vya Mkoa wa Iringa kwa weledi katika kuhamasisha zoezi hili. Amesema uhamasishaji ni muhimu sana katika kutoa hamasa kwa kazi ya Sensa ili asitokee mtu ambaye atakuwa hakupata taarifa na elimu juu ya umuhimu wa Sensa na kuhesabiwa. Aidha, ametoa wito kwa vyombo hivyo kuendelea na uhamasishaji huo kwa kipindi cha wiki nzima ili kulifanikisha zoezi hili katika Mkoa wa Iringa. “kufanikiwa kwa zoezi hili Mkoani Iringa sit u kutakuwa na manufaa kwa Mkoa wetu, bali kwa nchi nzima na jambo hili litafikiwa pale tu wananchi wote watakapokuwa wameelewa umuhimu wa zoezi hili na kushiriki katika kulifanikisha” alisisitiza Dkt. Christine.

Akiongelea matukio yasiyo ya kawaida katika zoezi hili, Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa Mkoa wa Iringa amesema kuwa zoezi hilo limeanza katika hali ya utulivu mkubwa na hakuna tukio lolote lisilo la kawaida lililotokea na kuripotiwa. Aidha, amewata wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa makarani wa Sensa pindi watakapopita katika maeneo yao na kujibu kwa usahihi maswali watakayokuwa wakiulizwa.

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka, akitoa maoni yake baada ya kuhesabiwa asubuhi ya leo amesema kuwa kazi ya kuhesabu na kuhesabiwa ni jukumu la kila mtanzania pasipo kujali mipaka ya aina yoyote. Amesema kila mtanzania anayo haki ya kuhesabiwa katika Sensa hii ili kuhakikisha Serikali yake inapata taarifa sahihi kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo kwa wananchi wake.
Mpaka amesema “miongoni mwa michango ya wananchi katika jitihada za kujiletea maendelea kwa kushirikiana na Serikali yao ni pamoja na kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka huu”. Amesema zipo njia mbalimbali za kushiriki katika shughuli za maendeleo katika kipindi hiki kutoa taarifa sahihi ni jukumu namba moja ili kuiwezesha Serikali kupata takwimu sahihi. 

Sensa ya Watu na Makazi inafanyika kwa mara ya tano nchini ikiongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Sensa kwa Maendeleo, jiandae kuhesabiwa’ ipo katika siku yake ya kwanza nchini kote na itaendelea kwa siku saba ili kuhakikisha kila mwananchi anahesabiwa mara moja tu.
=30=