Sunday, August 12, 2012

Mratibu Msaidizi wa Sensa Mkoa wa Iringa Conrad Millinga (kulia) na na Mwandishi wa Habari wa gazeti la Mwananchi, Tumaini Msowoya walipowasili katika viwanja vya Ikulu Ndogo Iringa kushiriki FUTARI iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma.

Katibu wa Mkuu wa Mkoa, Bahati Golyama akimuongozi kingozi wa dhehebu la dini ya Orthodox kuingia katika viwanja vya Ikulu Ndogo kwa ajili ya Futuru.

 Waumini wa Dini ya kiislamu waliojumuika pamoja katika swala ya Magharibi wakai wa hafla ya FUTARI iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma.

Wageni waalikwa katika hafla hiyo wakishiriki kupakua FUTARI katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa.

Wageni waalikwa katika hafla hiyo wakishiriki kupakua FUTARI katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa.

Wageni waalikwa katika hafla hiyo wakishiriki kupakua FUTARI katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa.



Wageni waalikwa katika hafla hiyo wakishiriki kupakua FUTARI katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa.

Wageni waalikwa katika hafla hiyo wakishiriki kupakua FUTARI katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa.

Viongozi vijana wakipanga mikakati, Bahati Golyama, Katibu wa RC Iringa (katikati), Gasto Mwambigija Andongwisye, Afisa Utumishi (kulia) na Mathias (kushoto) katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma akitoa neno la shukraki kwa waalikwa wa FUTARI.


Baadhi wa waumini walioshiri katika FUTARI hiyo. Mhe. Evarista Kalalu, DC Mufindi (kulia), Bibi. Gertrude Mpaka, RAS Iringa (wa pili kulia)



DKT. ISHENGOMA AFUTURISHA MKOANI IRINGA



Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma amewaomba viongozi wa dini kuendelea kutoa elimu na hamasa kwa wananchi juu ya umuhimu wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi litakalofanyika nchi nzima kuanzia tarehe 26 Agosti, 2012.

Ameyasema hayo katika viwanja vya Ikulu Ndogo ya Iringa alipokuwa akitoa neno la shukrani kwa viongozi wa dini mbalimbali na wageni waalikwa katika futari aliyoiandaa kwa ajili yao kwa ajili ya kutakiana heri katika mfungo mtukufu wa Ramadhani.

Amesema viongozi hao wa madhehebu ya dini wanao wajibu na mchango mkubwa katika kuwahamasisha wananchi washiriki katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ili kuhakikisha kuwa zoezi hilo linafanikiwa kwa maslahi ya nchi.

Dkt. Ishengoma amesema kuwa jukumu hilo linakuja kutokana na dhamana waliyonayo ya kuliwakilisha na kuliongoza kundi kubwa la waumini katika jamii. Amesema kutokana na umuhimu huo anawaomba viongozi hao washiriki kikamilifu ili Serikali iweze kupanga sawia mipango ya maendeleo. Amesema kuwa mipango ya maendeleo ili ifanikiwe takwimu za watu zinahitajika sana.

Akiongelea umuhimu wa zoezi hilo amesema kuwa zoezi hilo litaisaidia  Serikali kupanga mipango ikiwa na lengo la kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi wake. Amesema kujulikana kwa idadi hiyo ya watu ni muhimu kwa sababu kutaisaidia Serikali kuyatambua makundi mbalimbali ya watu katika jamii na kuwafikishia mahitaji yao maalumu ili waweze kufurahia uhuru wao katika nchi yao.

=30=


SIKU RC ALIPOFUTURISHA IRINGA


 Baadhi ya Waumini wa Dini ya kiislam wakipata swala kabla ya FUTARI iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma


 Baadhi ya Waumini wa Dini ya kiislam wakipakua FUTARI. Picha kwa hisani ya Blog ya Francis Godwin 

 Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka (Picha kwa hisani ya Blog ya Francis Godwin )

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (kushoto) akishiriki katika FUTARI (Picha kwa hisani ya Blog ya Francis Godwin )


 Baadhi ya wageni waalikwa akipata FUTARI

Wageni waalikwa akisikiliza nasaha za Mkuu wa Mkoa (hayupo pichani)