Monday, December 19, 2011

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa yapata Wakili




Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, imepata Wakili, baada ya Mwanasheria katika Ofisi hiyo Paulos Lekamoi, kusajiliwa na kutambuliwa na Mahakama Kuu ya Tanzania.




Wakili Paulos Lekamoi akitambuliwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Bara

Fuatilia habari zaidi juu ya Paulos Lekamoi ni nani hasa??

YALIYOJILI MIAKA 50 YA UHURU KWA MKOA WA IRINGA KITAIFA

































 Baadhi ya watendaji katika Banda la Mkoa wa Iringa


 Baadhi ya watendaji katika Banda la Mkoa wa Iringa



 Mandari ya Banda la Mkoa wa Iringa kwa nje



 Sidhani kama kuna kitu ambacho kingeweza kuwatoa viongozi hawa wa Mkoa wa Iringa katika banda hili la Mkoa wa Kagera kabla ya kutimiza hadhima yao mahususi. 


 Miaka 50 ya Uhuru na Tafakari ya hali ya juu


 ...Hii inakutosha Mhe. RC ni maneno ya mjasiriamali 'Khadija Design' akimwambia Mhe. Mkuu wa Mkoa hayupo pichani.


 Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mhe. Zainab Kwikwega akisaini kitabu cha wageni katika Banda la Mkoa wa Iringa katika viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere katika maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara


 Tarehe 01. Disemba, 2011 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma (Mb.) na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka (katikati) na Kiongozi mwandamizi wa Banda la Mkoa wa Iringa, Shenal Nyoni wakiweka mikakati ya mapokezi ya viongozi wa kitaifa watakaotembelea banda la Mkoa wa Iringa


 Tarehe 01. Disemba, 2011 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma (Mb.) na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka (kulia) wakifurahia jambo katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam katika sherehe za miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara


 Tarehe 01 Disemba, 2011, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma (Mb.) akiwa ni
miongoni mwa mamia kwa maelfu ya watanzania waliojumuika katika maadhimisho ya
Miaka 50 ya Uhuru katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam

Tarehe 01 Disemba, 2011, Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka akiwa ni
miongoni mwa ma mia kwa maelfu ya watanzania waliojumuika katika maadhimisho ya
Miaka 50 ya Uhuru katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam



TANROADS YAKUSANYA MIL 18


Ofisi ya Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Iringa (TANROADS) imekusanya zaidi ya shilingi milioni 18 katika kipindi cha kuanzia Julai, 2011 hadi Septemba, 2011 zikiwa ni tozo kwa magari yaliyozidisha uzito.

Taarifa hiyo imetolewa na Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa iringa, Mhandisi. Paul Lyakurwa, wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji kwa mwaka 2010/ 2011 na mpango wa matengenezo na ukarabati kwa mwaka 2011/2012 na taarifa ya utekelezaji hadi Septemba, 2011 ya Wakala wa Barabara Mkoa wa Iringa katika Kikao cha Bodi ya Barabara ya mkoa wa Iringa kilichofanyika katika ukumbi wa St. Dominic katika Manispaa ya Iringa,

Mhandisi. Lyakurwa amesema kuwa ofisi yake inajukumu la kudhibiti uzito wa magari barabarani kwa kutumia mizani isiyohamishika iliyopo Makambako.
Amesema katika kipindi cha Julai, 2011 hadi Septemba, 2011 magari yaliyopimwa ni 1,005 kati ya hayo magari 103 yalizidisha uzito na kulipishwa tozo la uharibifu wa barabara kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Barabara Na. 30 ya mwaka 1973 na kanuni zake za mwaka 2001 ofisi yake imekusanya shilingi 18.175 milioni.

Akielezea utekelezaji wa ahadi za Mhe. Dk. Jakaya Kikwete wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 zilizo katika Ilani ya uchaguzi ya CCM kuhusu sekta ya barabara Mkoani Iringa, hasa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Njombe- Makete (Km. 109 kwa kiwango cha lami amesema kuwa ujenzi wa Km. 11.5 kwa kiwango cha lami kati ya Mang’oto na Tandala ndani ya Wilaya ya Makete umekamilika kwa gharama ya shilingi 4,612,654 milioni.

Amesema ujenzi wa Km. 1 umepangwa kutekelezwa mwaka wa fedha 2011/2012 maeneo ya Mang’oto kwa gharama ya shilingi 797,040 milioni pamoja na utekelezaji huo kiasi cha shilingi 1,480,644 milioni zinahitajika kulipia deni la kazi zilizofanyika kati ya mwaka 2008/ 2009 na mwaka 2010/ 2011.    

Wakati huohuo Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma ameagiza ushirikishwaji wa jamii katika utunzaji wa miundombinu ya Mkoa wa Iringa ili iweze kuwanufaisha wananchi walio wengi.

Akifungua kikao cha Bodi ya Barabara cha Mkoa wa Iringa, amesema bado kuna mapungufu kadhaa katika ushirikishwaji wa jamii katika utunzaji wa miundombinu ya barabara katika Mkoa wa Iringa hususani shughuli zinazofanyika ndani ya hifadhi ya barabara na kuagiza jamii ihusishwe kikamilifu katika utunzaji huo wa miundombinu ya barabara.
=30=