Wednesday, October 31, 2012




Aga Khan Health Services Resumes Delivery Services at Iringa Primary medical Center.
Aga Khan Health services Iringa has resumed delivery services and has registered its first delivery today morning.

Speaking with Daily news in an exclusive interview the Joining Hands Initiative project manager Anitah Muruve said that both the mother and the baby are in good condition. She said the delivery services have been established under Joining Hands: Improving Maternal, Newborn and Child Health (JHI) Project which is a Canadian International Development Agency (CIDA) funded initiative that aims to contribute to improved reproductive and maternal, newborn and child health (MNCH) in fifteen districts across five target regions in Tanzania.
 Kerstin Scheffler with her new new baby (cetre)

Kerstin Scheffler with her new new baby (cetre)

Maruve said that the project is focusing on improving quality of and access to maternal, newborn and child health services; increasing utilization of MNCH service at primary care level.

The project manager added that the project objectives are improving maternal, newborn and child health practices through behaviour change communication (BCC) and health promotion (HP)  and enhancing knowledge transfer and exchange on maternal, newborn and child health  through a strong public private partnership (PPP) approach under which the project is being implemented. The delivery services are open to the public. 

The Aga Khan Health Services Tanzania will continue to establish deliveries in its other health facilities in Mwanza, Dodoma, Mbeya and Morogoro regions.
Speaking on the services received, the mother of the new born baby Kerstin Scheffler said she has enjoyed and appreciate the services offered throughout she has been at the centre.

Veronica James, The Iringa Aga Khan hospital, Manager said her centre is keeping on improving her services in order to offer better health care services to the people. She further, calls upon people to go for better maternal and child health.

The project has got three phases as project implementation planning (PIP), inception and implementation.
=30=
MTOTO WA KWANZA AZALIWA HOSPITALI YA AGA KHAN-IRINGA


Hospitali ya Aga Khan imefanikia kuanzisha huduma ya kuboresha afya ya mama mjamzito na mtoto kwa kupitia mradi wake wa Tuunganishe mikono pamoja na mwanamke wa kwanza mjamzito amefanikiwa kujifungua salama asubuhi ya leo.

Baba mzazi wa mtoto aliyezaliwa leo hospitali ya Aga Khan Said Gallos Mlewa (kushoto) akiwa na familia yake.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kukabidhi zawadi kwa niaba ya jamuiya ya Aga Khan mkoa wa Iringa, Meneja wa hospitali ya Aga Khan-Iringa, Veronica James amesema “leo imekuwa ni siku ya furaha sana kwa hospitali ya Aga Khan na kwa wananchi wa manispaa ya Iringa na vitongoji vyake kutokana na huduma za kujifungua kwa mama mjamzito wa kwanza hospitalini hapa”.

Akielezea malengo ya mradi wa Tuunganishe nikono pamoja Veronica amesema kuwa mradi huo unalenga kuwasogezea wananchi huduma karibu na kwa ubora unaotakiwa kwa kupunguza foleni kwa wanawake wajawazito katika vituo vingine vinavyotoa huduma ya mama wajawazito na kujifungua kwa lengo la kuwapunguzia hadha wajawazito hao.

Meneja wa hospitali ya Aga Khan iringa amesema kuwa mradi huo unalenga kuongeza kiwango na matumizi ya huduma ya afya ya mama mjamzito na watoto nchini. Amesema kuwa mradi huo pia unalenga kuboresha kiwango cha upatikanaji wa huduma ya afya ya mama mjamzito na watoto. Malengo mengine ameyataja kuwa ni pamoja na kuboresha huduma ya afya yam ma mjamzito na watoto katika jamii na kushirikiana na kujifunza kuhusu afya ya mama mjamzito na watoto.

Akielezea furaha yake mama mzazi Kerstin Scheffler (38) amesema kuwa amefurahishwa na huduma katika hospitali hiyo kwa kipindi chote alichokuwa hospitalini hapo kutoka kwa madaktari na wauguzi. Mama huyo aliyejifungua mtoto wake wa tatu leo na kupewa jina la Malaika Lina ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuzitumia huduma za afya ya mama mjamzito na mtoto katika hospitali hiyo ili waweze kunufaika vizuri.
Katika maelezo yake ya jumla Daktari mfawidhi wa hospitali ya Aga Khan Iringa, Dkt. Jumaa Mbete amesema mama huyo amejifungua salama majira ya saa 3:25 asubuhi hospitali hapo na mtoto akiwa na uzito wa kilo 3.3.

Dkt. Mbete amesema kuwa lengo la hospitali yake ni kusaidiana na serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuimarisha huduma ya afya ya mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano nchini.

Akiongelea gharama, Daktari mfawidhi amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakihofia gharama katika hospitali yake jambo ambalo si kweli. Amesema kuwa gharama ni ndogo sana akitolea mfano wa gharama kwa mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano kuwa huduma ni bure. Amesema kuwa katika hospitali hiyo huduma hiyo hutolewa kwa masaa 24 na kutoa wito kwa wananchi kujitokeza na kunufaika na huduma hiyo.

Mradi wa Tuunganishe mikono pamoja ni mradi wa miaka mitatu ukiendeshwa katika mikoa ya iringa, Dodoma, Mwanza, Mbeya na Morogoro na mashika yanayotekeleza mradi huo Mfuko wa Aga Khan, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, shirika la misaada ya maendeleo la Canada na chuo kikuu cha Aga Khan.