Friday, March 20, 2015

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI JIJINI MBEYA



Mamlaka ya Majisafi na usafi wa mazingira jiji la mbeya itaadhimisha kilelel cha wiki ya maji mwaka 2015 katika viwanja vya Ofisi za Mamlaka ya Maji. 

Kilele hicho kilitanguliwa na Uzinduzi wa wiki ya Maji uliofanyika kuanzia tarehe 16 Machi, 2015 kwa kufanya kazi za usafi wa mazingira katika eneo la ofisi na kwenye vituo vyote vya kutolea huduma. Aidha, shughuli nyingine ni kuhamasisha wananchi juu ya ulipaji wa ankara za maji kwa wakati.

Kazi nyingine zilizofanywa katika wiki hiyo ni pamoja na kutembelea taasisi pamoja na shule kuhamasisha taasisi kujiunga na mtandao wa majitaka na kupanda miti eneo la Ivumwe.

Katika kilelel cha Maadhimisho hayo mada ya Usafi wa Mazingira na Utunzaji wa vyanzo vya Maji itatolewa.
Michezo na burudani mbalimbali vitaanikiza ikiwa ni pamoja na mchezo wa kuvuta kamba na ngoma.

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya. Maadhimisho ya wiki ya maji yanaongozwa na Kaulimbiu isemayo:

Maji kwa Maendeleo endelevu.

=30=