Wednesday, February 15, 2012

Mgodi wa Tarajali kuanza Ruvuma

Na. Revocatus Kassimba, Ruvuma
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Ghalib Bilal amewahakikishia wakazi wa Mkoa wa Ruvuma na Tanzania kwa ujumla kuwa  mradi wa mgodi tarajali wa Urani wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma utatekelezwa kwani una umuhimu na maslahi kitaifa.

 Makamu Rais Dk. Mohamed Ghalib Bilal akihutubia mamia ya wananchi wa kijiji cha Likuyu Sekamaganga wilaya ya Namtumbo wakati alipofanya ziara katika mradi wa urani

Dk. Bilal amesema hayo wakati akiongea na wafanyakazi wa mgodi huo unaomilikiwa na kampuni ya Mantra Tanzania kuwa Serikali inafuatilia kwa makini kuona madini hayo muhimu yanalifaidisha Taifa.

Aliongeza kuwa anao uhakika kuwa taratibu zote za hifadhi ya mazingira na usalama wa maisha ya wakazi wanaozunguka eneo hilo umetiliwa mkazo na kampuni kwa kushirikiana na taasisi ya nishati ya atomiki nchini.

Aidha, kwa upande wake Mkurugenzi wa Mantra Tanzania, Asa Mwaipopo ameiomba Serikali kuharakisha taratibu za kisheria ili mgodi uweze kuanza hapo mwaka ujao kwa ujenzi na ifikiapo 2014 uzalishaji uanzae ili ajira zipatazo 1600 wakati wa ujenzi wa mgodi na nyingine 400 wakati wa uzalishaji ziweze kupatikana kwa watanzania na kusaidia kukuza uchumi.

 
Makamu wa Rais akipokewa na viongozi wa kampuni ya Mantra wakati alipowasili katika eneo litakalojengwa mgodi wa Uranium wilaya ya Namtumbo