Tuesday, September 20, 2011

RC IRINGA AHAIDI USHIRIKIANO KUKUZA PATO LA MWANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma ameahidi kushirikiana na viongozi wa Mkoa huo ili kuinua pato la mwananchi wa chini kwa minajili ya kumuinua kiuchumi.

Kauli hiyo ameitoa ofisini kwake wakati akipokea taarifa ya makabidhiano ya Mkoa wa Iringa iliyowasilishwa kwake na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka.

Amesema “ni matumaini yangu kuwa tutakuwa bega kwa bega ili kuhakikisha mwananchi wa chini anainua uchumi wake yeye mwenyewe hasa kwa kuongeza pato lake”.

Dkt. Ishengoma ameitaja changamoto nyingine inayoukabili Mkoa wa Iringa kuwa ni ile ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI. Amesema Mkoa unachangamoto mahususi ya kuhakikisha inateremsha kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kutoka asilimia 15.7 ya sasa  hadi kufikia angalau asilimia tano. Amesema kuwa japokuwa dawa ya ugonjwa huo bado haijapatikana ila wananchi wenyewe wanayo dawa ikiwa ni pamoja na kubadili tabia.

Aidha, amewataka viongozi wa Mkoa kuangalia maeneo yanayohitaji kufikishiwa zaidi elimu ya maambukizi ya UKIMWI ili kuweza kuinusuru jamii na janga hilo. Amesema kuwa ugonjwa huo ni lazima jitihada za kuudhibiti zifanyike ili kupunguza idadi ya yatima na wajane wanaotokana na matokeo ya ugonjwa huo.

Awali akiwasilisha taarifa ya makabidhiano ya Mkoa wa Iringa, Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka amesema kuwa katika mwaka 2005 pato la Mkoa wa Iringa lilikuwa ni shilingi 867,482,000,000 huku Mkoa ukishika nafasi ya tano kitaifa. Aidha, pato la mkazi lilikuwa ni shinlingi 558,444 na Mkoa ulishika nafasi ya pili kitaifa.

Amesema katika mwaka 2010/2011 pato la Mkoa lilifikia Shilingi  1, 469, 720, 000,000 na pato la mkazi lilikuwa limeongeka kufikia Tshs 859,875 ambalo ni ongezeko la Shilingi 301,431 (54%).

Mpaka amesisitiza kuwa pato la Mkoa linaonekana ni kubwa lakini kwa kiasi kikubwa huchangiwa na mashamba makubwa ya chai, viwanda vya chai, misitu na viwanda vya mbao.

Upande wa Maambukizi ya UKIMWI Katibu Tawala huyo amesema kuwa Mwaka  2003/2004 maambukizi yalikuwa 13.4% na Mwaka 2010/11 maambukizi yamefikia 15.7%. Aidha, hadi Desemba, 2010/11 wananchi 74,632 wenye Virusi vya UKIMWI walioandikishwa kwenye Mpango wa Dawa za kupunguza makali.

Mkoa umekamilisha Mpango wa miaka minne 4 wa kupambana na tatizo la UKIMWI. Mpango huu ni kuanzia Oktoba 1998 hadi Septemba 2012.

MKUU WA MKOA WA IRINGA AWASILI RASMI MKOANI IRINGA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (mwenye suti nyekundu) akizungumza na watumishi waliojitokeza kumlaki

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (mwenye suti nyekundu) akizungumza na watumishi waliojitokeza kumlaki kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka


 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (mwenye suti nyekundu) akiwasalimia wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa nje ya jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa 

Mhandisi David Mwakalalile ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Kenneth Komba, Afisa Michezo ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Bibi. Hawa Kalolo ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Avelina Ngonyani, Mwangalizi wa Ofisi ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Neema G. Mwaipopo, Afisa Tawala ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Dennis Gondwe, Afisa Habari ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Bibi. Laurencia Mwanga, Katibu Muhtasi ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake


 Joseph Mnyikambi Afisa Elimu Mkoa ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Bw. Adam Swai, Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Uchumi na Sekta za Uzalishaji ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

  Bw. Theophil Likangaga, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Huduma za Jamii ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

  Bw. Vicent James, Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Miundombinu  ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake


 Bw. Barnabas Ndunguru, Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

HATIMAE DIMOSO AWAPELEKA MATOMBO

Menrad Dimosso akitoa shukrani zake kwa ujumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na zawadi waliyompatia katika sherehe ya harusi yake iliyofanyika katika ukumbi wa NESTO ZANGIRA- MATOMBO.

 Menrad Dimosso akitoa shukrani zake kwa Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Mipango na Uratibu, Nuhu Mwasumilwe baada ya kukabidhi zawadi ya Mkoa katika sherehe ya harusi yake iliyofanyika katika ukumbi wa NESTO ZANGIRA- MATOMBO.

Bwana harusi Menrad Dimosso na mkewe wakila keki kwa staili walioichagua wao 

 Hiyo ilikuwa miondoko ya KWAITO likiwa ni ombi mahususi la Sam Nyagawa

Mwenyekiti wa Kamati ya Harusi ya Menrad Dimosso Bi. NINA

Baadhi ya watumishi wa RS Iringa waliopata fursa ya kuwa mashuhuda

 Baadhi ya watumishi wa RS Iringa waliopata fursa ya kuwa mashuhuda

Mke wa Menrad Dimosso akirekebisha koti la MZEE baada ya kumvika ndani ya ukumbu wa NESTO ZANGIRA 

 Mke wa Menrad Dimosso akiingia ukumbini

Menrad Dimosso akiingia ukumbini