Wednesday, September 23, 2015

TASAF WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UWAZI NA UWAJIBIKAJI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kulipa uzito tatizo la utapiamlo ili kupunguza udumavu, ulemavu na vifo vya watoto na wanawake wanaonyonyesha.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua mkutano wa kamati za lishe za halmashauri na mkoa wa Iringa  kuhusu masuala ya lishe ya mama na mtoto katika ukumbi wa Veta.
Masenza alisema “matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata kuua watoto wetu na wanawake hasa wale wajawazito na wanaonyonyesha. Pia jamii kwa ujumla imekuwa ikiathirika kwa njia moja au nyingine kwa kuwepo kwa utapiamlo”. Masenza aliongeza “pamoja na maendeleo ambayo nchi yetu imeyapata katika maeneo mbalimbali, bado tatizo la lishe duni linaendelea kuathiri uchumi na kuchangia kuwepo kwa umasikini. Lishe duni pia huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili hivyo kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na taifa”.
Alisema kuwa uboreshaji wa hali ya lishe nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na kupunguza umasikini kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Aliongeza kuwa kwa upande wa watoto lishe husaidia kuongeza uwezo wao kiakili na usanisi shuleni.
Mkurugenzi wa Mwanzo bora Dkt. Daniel Nyagawa alilitaja lengo kuu la mradi huo kuwa ni kuisaidia serikali katika kutekeleza mkakati wa taifa wa lishe pamoja na mkakati wa taifa wa kubadili tabia na mienendo ya maisha.
Aliongeza kuwa mradi wa lishe wa mwanzo bora unalenga kupunguza upungufu wa damu kwa wajawazito na wanawake wanaonyonyesha kwa asilimia 20. Aidha, unalenga kupunguza udumavu kwa watoto chini ya umri wa miaka miwili kwa asilimia 20. Mwisho mradi unalenga kujengea uwezo wa utekelezaji kwa serikali mashirika yasiyo ya kiserikali na kijamii.
Dkt. Nyagawa alisema kuwa mradi unatumia mkakati wa mawasiliano yanayolenga kubadili tabia katika masuala ya lishe. Alisema kuwa mradi unalenga tabia ambazo zikifuatwa zitaleta matokeo makubwa katika kupunguza udumavu na upungufu wa damu. Aliongeza mradi unalenga kubadilisha tabia binafsi ambazo zamani miradi mingi haikufanya.
Akiongelea walengwa wa mradi huo, Dkt. Nyagawa aliwataja “walio ndani ya siku 1,000 tangu kutungwa kwa mimba hadi mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili”.Alifafanua kuwa ni mama mjamzito, anayenyonyesha na mama mwenye mtoto umri usiozidi miaka miwili. Baba ambaye mwenza au mke wake ana sifa zilizotangulia na wale wote wanaolea watoto wenye umri usiozidi miaka miwili.
Mradi wa lishe wa mwanzo bora ni mradi wa lishe uliofadhiliwa na serikali ya marekani kupitia USAID ukitekelezwa katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Dodoma, Manyara na Mbeya.
=30=                                          

JAMII YATAKIWA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Jamii imetakiwa kulipa uzito tatizo la utapiamlo ili kupunguza udumavu, ulemavu na vifo vya watoto na wanawake wanaonyonyesha.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua mkutano wa kamati za lishe za halmashauri na mkoa wa Iringa  kuhusu masuala ya lishe ya mama na mtoto katika ukumbi wa Veta.
Masenza alisema “matatizo mbalimbali ya utapiamlo yanaendelea kudumaza, kulemaza na hata kuua watoto wetu na wanawake hasa wale wajawazito na wanaonyonyesha. Pia jamii kwa ujumla imekuwa ikiathirika kwa njia moja au nyingine kwa kuwepo kwa utapiamlo”. Masenza aliongeza “pamoja na maendeleo ambayo nchi yetu imeyapata katika maeneo mbalimbali, bado tatizo la lishe duni linaendelea kuathiri uchumi na kuchangia kuwepo kwa umasikini. Lishe duni pia huathiri ukuaji na maendeleo ya mtoto kimwili na kiakili hivyo kufifisha mchango wake katika maendeleo ya jamii na taifa”.
Alisema kuwa uboreshaji wa hali ya lishe nchini ni msingi wa afya njema, ubunifu, maendeleo mazuri ya kiuchumi na kupunguza umasikini kwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. Aliongeza kuwa kwa upande wa watoto lishe husaidia kuongeza uwezo wao kiakili na usanisi shuleni.
Mkurugenzi wa Mwanzo bora Dkt. Daniel Nyagawa alilitaja lengo kuu la mradi huo kuwa ni kuisaidia serikali katika kutekeleza mkakati wa taifa wa lishe pamoja na mkakati wa taifa wa kubadili tabia na mienendo ya maisha.
Aliongeza kuwa mradi wa lishe wa mwanzo bora unalenga kupunguza upungufu wa damu kwa wajawazito na wanawake wanaonyonyesha kwa asilimia 20. Aidha, unalenga kupunguza udumavu kwa watoto chini ya umri wa miaka miwili kwa asilimia 20. Mwisho mradi unalenga kujengea uwezo wa utekelezaji kwa serikali mashirika yasiyo ya kiserikali na kijamii.
Dkt. Nyagawa alisema kuwa mradi unatumia mkakati wa mawasiliano yanayolenga kubadili tabia katika masuala ya lishe. Alisema kuwa mradi unalenga tabia ambazo zikifuatwa zitaleta matokeo makubwa katika kupunguza udumavu na upungufu wa damu. Aliongeza mradi unalenga kubadilisha tabia binafsi ambazo zamani miradi mingi haikufanya.
Akiongelea walengwa wa mradi huo, Dkt. Nyagawa aliwataja “walio ndani ya siku 1,000 tangu kutungwa kwa mimba hadi mtoto anapofikisha umri wa miaka miwili”.Alifafanua kuwa ni mama mjamzito, anayenyonyesha na mama mwenye mtoto umri usiozidi miaka miwili. Baba ambaye mwenza au mke wake ana sifa zilizotangulia na wale wote wanaolea watoto wenye umri usiozidi miaka miwili.
Mradi wa lishe wa mwanzo bora ni mradi wa lishe uliofadhiliwa na serikali ya marekani kupitia USAID ukitekelezwa katika mikoa ya Iringa, Morogoro, Dodoma, Manyara na Mbeya.
=30=                                          

WANAWAKE IRINGA WATAKIWA KUPIMA SARATANI YA KIZAZI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wanawake mkoani Iringa wametakiwa kujitokeza kupima saratani ya mlango wa kizazi ili wanapogundulika na saratani hiyo waanze matibabu mapema.
Wito huo umetolewa na mganga mkuu wa mkoa wa Iringa, Dkt. Robert Salim alipokuwa akifungua semina ya kufuatilia utekelezaji wa mipango na maazimio yaliyowekwa kuhusu kukabiliana na saratani ya mlango wa kizazi iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha afya ya msingi mjini Iringa.
Dkt. Salim alisema kuwa saratani ya mlango wa kizazi inasababisha maradhi na vifo kwa wanawake wengi nchini isipotambuliwa na kuanza kutibiwa mapema. Alisema kuwa wanawake wote walioanza mahusiano ya kimapenzi wanatakiwa kujitokeza katika vituo vya afya kupima ili wanapogundulika wameathirika na saratani hiyo waanze tiba mapema. Alisema kuwa yapo mahusiano makubwa baina ya maambukizi ya virusi vya ukimwi na saratani ya mlango wa kizazi. Kutokana na mahusiano hayo ambayo kwayo mkoa wa Iringa umeathirika sana na maambukizi ya ukimwi kwa 9.1% hivyo kusababisha ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi kuwa juu.
Nae Mkurugenzi wa uboreshaji afya kutoka taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Dkt. Sarah Maongezi alisema kuwa semina hiyo ililenga kufuatilia utekelezaji wa mipango na maazimio ya awali waliyojiwekea katika kukabiliana na tatizo la saratani ya mlango wa kizazi mkoani hapa. Alisema kwa kuwa mkoa wa Iringa ulianza muda mrefu mapambano dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi hivyo mkoa unatakiwa kuwa umepiga hatua za mafanikio zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine nchini. Alisema kuwa kwa hatua iliyofikiwa na mkoa wa Iringa, mkoa huo unaweza kujihamasisha kununua vifaa na vifaa tiba kwa lengo la kukabiliana na saratani ya mlango wa kizazi.
Saratani ya mlango wa kizazi ni miongoni mwa magonjwa yanayosababisha vifo kwa wanawake wengi ikikadiriwa kuwa zaidi ya wanawake 4,000 hupoteza maisha nchini kila mwaka.
=30=

FOX APONGEZWA KWA KAZI ZA KIJAMII MUFINDI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza amepongeza kazi za kijamii zinazofanywa na muwekezaji Geoff Fox kwa lengo la kuwapunguzia umasikini wananchi wa Mufindi.
Pongezi hizo alizitoa alipotembelea shughuli za maendeleo zinazofanywa na muwekezaji huyo wilayani Mufindi kwa lengo la kujifunza pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa. “Nimefurahishwa na kazi za kijamii zinazofanywa na muwekezaji za kuisaidia jamii katika sekta za afya, elimu na ustawi wa jamii. Kazi hizi ni jukumu letu kama serikali lakini kutokana na sera yetu ya ushirikishaji jamii na sekta binafsi, sekta binafsi inapata fursa ya kusaidia juhudi hizi za kimaendeleo” alisema Masenza.
Alipotembelea zahanati ya Mdabulo inayomilikiwa na kanisa katoliki Jimbo la Iringa, mkuu wa mkoa alipongeza kazi nzuri inayoendelea kufanywa na zahanati hiyo iliyoanzishwa mwaka 1946 ikiwa umbali wa km 48 kutoka mjini Mafinga. Masenza alishauri uandaliwe utaratibu wa kutoa elimu ya magonjwa ya kisukari na saratani na mlango wa kizazi kutokana na magonjwa hayo kutokupewa kipaumbele. “Magonjwa ya kisukari na saratani ya mlango wa kikazi yamekuwa hayapewi umuhimu sana lakini yanachangia sana katika vifo vya wananchi wetu. Ni vizuri mkaweka utaratibu wa kuwa mnatoa elimu ya utambuzi na kujikinga na magonjwa haya ili kupunguza hatari ya vifo” alisema Masenza. Masenza aliiagiza halmashauri kununua mitungi …na siki ili kusaidia uchunguzi wa saratani hiyo.
Mkuu wa mkoa aliwaagiza wataalamu wa sekta ya afya wa halmashauri ya wilaya ya mufindi kuweka utaratibu wa kuitembelea zahanati ya Mdabulo mara kwa mara na kutoa ushauri wa kitaalam.
Kutokana na zahanati hiyo kuwahudumia wananchi wengi, mkuu wa mkoa alimuagiza mganga mkuu wa mkoa kufuatilia mchakato wa kuipandisha hadhi zahanati ya Mdabulo kuwa kituo cha afya ufanyike haraka…ili…
=30=
 

WATUMISHI FEKI HAWANA NAFASI IRINGA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkoa wa Iringa umejipanga kukabiliana na watumishi feki katika sekta ya afya ili kutoa huduma za kitaalam kwa wananchi wake.
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipokuwa akiongea na vyombo vya habari juu ya mkoa ulivyojipanga kukabiliana na changamoto ya watumishi wasio na sifa katika sekta ya afya mkoani hapa kufuatia wimbi la watumishi wasio na sifa kubainika wakitoa huduma katika hospitali za serikali.
Ayubu alisema kuwa mkoa wa Iringa upo makini kimfumo na rasilimali watu kukabiliana na tatizo la watumishi feki. Alisema mifumo ya kuhakiki watumishi imeboreshwa zaidi katika miaka ya hivi karibuni kwa lengo la kukabiliana na watumishi feki.
“Mtumishi yeyote anapoajiliwa anawasilisha vyeti vyake vya kitaaluma alivyonavyo na vinakaguliwa. Kutokana na wimbi la kugushi vyeti, mkoa umepanua wigo kwa kushirikisha taasisi zote zinazohusika na utoaji vyeti husika kama NECTA, NACTE, vyuo vikuu ili wathibitishe uhalali wa vyeti hivyo”, alisisitiza Ayubu.
Aliongeza kuwa mfumo wa kieletroniki wa malipo na mishahara ulioanza mwaka 2011, umeongeza ufanisi katika udhibiti wa vyeti feki kwa sababu mfumo unaingiza vyeti vyote kasha vinaenda kuhakikiwa Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Alisema kuwa pamoja na kusaidia kubaini watumishi wenye vyeti feki chini mfumo huo umeondoa tatizo la watumishi kulipwa zaidi ya mara moja na kuondoa changamoto ya mishahara hewa. Katika mfumo huu kama mtumishi alishaajiliwa serikalini mfumo utamgundua kirahisi hivyo kuwa vigumu kulipwa mshahara zaidi ya mmoja. Alisema kuwa hata ule mchezo wa watu kutumia vyeti vya watu wengine unapatiwa tiba.
Ayubu aliongeza kuwa watumishi wote wa serikali wanavaa vitambulisho vya vya kazi vinavyomtambulisha jina kamili na cheo ili iwe rahisi kwa anayepewa huduma kumtambua mtoa huduma. Ameongeza utaratibu huo unaondoa malalamiko kwa wananchi kwa sababu kila mtumishi anafahamika kwa jina na cheo chake.
Ayubu alisema mwaka 2011 mkoa ulifanya uhakiki wa taarifa za watumishi wa umma ili kubaini uwepo wa watumishi hewa. Alisema kuwa anajivunia kutokuwepo kwa watumishi hewa na mishahara hewa.
Afisa utumishi katika ofisi ya mkuu wa mkoa, Gasto Andongwisye alisema katika kuhakikisha mkoa unaendelea kuwa na watumishi wenye sifa kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma na kudhibiti mishahara hewa, ofisi ya mkuu wa mkoa kupitia sehemu ya utawala na rasilimali watu imeendelea kufanya uhakiki kila mwezi kwa watumishi na ‘payroll’.
Andongwisye aliongeza kuwa katika kuhakikisha hakuna mtumishi mamluki anayejipenyeza katika hospitali za serikali mkoani hapa na kutoa huduma, idara zote katika hospitali wamekuwa wakifanya vikao vya kila siku kupeana taarifa za kazi na vikao vya watumishi wote kila idara kwa lengo la kufahamiana na kujadili changamoto zilizopo.
=30=