Sunday, March 16, 2014

ONGEZEKO LA WATU IRINGA WAONGEZA MAHITAJI YA ARDHI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Ongezeko kubwa la idadi ya watu katika manispaa ya Iringa linaenda sambamba na ongezeko la shughuli kuichumi hatimae kusababisha kuongezeka kwa mahitaji na matumizi ya ardhi.
 
Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa, Immaculate Senje
Kauli hiyo imetolewa na Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa, Immaculate Senje alipokuwa akiwasilisha mada ya Mpango kamambe wa mji wa Iringa (Iringa Master Plan) 2015-2035 katika mkutano wa wadau wa maandalizi ya Mpango Kamambe wa Mji wa Iringa uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari ya Lugalo.

Senje amelitaja ongezeko la idadi ya watu katika mji wa Iringa linaloenda sambamba na ongezeko la shughuli za kiuchumi linasababisha kuongezeka kwa mahitaji na tumizi ya ardhi. Amesema ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya matumizi ya ardhi upo umuhimu wa kuwa na mwongozo unaotoa dira ya ukuaji wa mji ambao ni endelevu.

Akiongelea matumizi ya ardhi, Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Iringa amesema kuwa mji wa Iringa kama ilivyo miji mingine nchini unayo maeneo ya makazi yaliyopangwa na kupimwa pamoja nay ale yanayoenelezwa kiholela. Amesema kuwa eneo la makazi lililopangwa wakati wa ukoloni liko katika makundi matatu ambayo ni ujazo wa chini, ujazo wa kati na ujazo wa juu.

Akiongelea maeneo ambayo yameendelezwa kiholela, ameyataja maeneo hayo kuwa yanapatikana katika kata za Mwangata, Ruaha, Mkwawa, Mtwivila, Kihesa na Nduli. Amesema kuwa yapo maeneo ya vijiji vilivyoingia katika Manispaa siku za karibuni kama Kigonzile, Nduli, Mgongo, Mkoga na kitongoji cha Ulonge kuwa yana makazi yaliyotawanyika.

Akielezea matarajio yake baada ya mkutano, Senje amesema kuwa masuala muhimu, kero na changamoto zinazowakabili wakazi wa Iringa zitaibuliwa na kuwa msingi mkuu utakaoongoza uandaaji wa Mpango Kamambe utakaokidhi mahitaji ya wakazi wa Manispaa ya Iringa.
=30=

No comments:

Post a Comment