Friday, September 21, 2012

NENDA KWA USALAMA KUKUMBUSHA SHERIA NA TARATIBU



Wiki ya nenda kwa uslama barabrani inalenga kuwakumbusha madereva na watumiaji wa barabara juu ya sheria na taratibu za matumizi mazuri ya barabara kwa usalama wa watumiaji na vyombo vya moto nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Mkaguzi wa Polisi, Abel Baetazal Swai kutoka Makao Makuu ya Kikosi cha Usalama Barabarani, Kitengo cha Elimu alipokuwa aliwaelimisha wananchi wa Manispaa ya Iringa katika Banda la Polisi lililopo katika uwanja wa maonesho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani yanayoendelea mjini Iringa.
Mkaguzi Swai amesema kuwa maana halisi ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani n kufanya marejeo kwa madareva ambao wamepitia mafunzo ya udereva kuweza kukumbushwa sheria na taratibu pindi wanapokuwa barabarani. Amesema kuwa polisi wanakuwa wanatoa elimu kwa makundi mbalimbali yanayotumia vyombo vya moto kwa namna moja na ambayo hayatumii vyombo hivyo kwa namna nyingine. Amesema kuwa katika kipindi hicho kazi nyingine zinazofanyika ni pamoja na kukagua magari bure. 

Akielezea tathmini yake juu ya hali ya usalama barabarani Mkaguzi wa Polisi Swai amesema kuwa hali si mbaya kwa sababu elimu inayotolewa imekuwa ikiwasaidia sana madereva na watumiaji wengine wa barabara kurejea katika sheria na taratibu za usalama barabarani.  Amesema kuwa elimu hiyo imekuwa ikitolewa katika shule na mikusanyiko mbalimbali, na majaribio ya tathmini yaliyofanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Pwani inaonesha kupungua kwa ajali za barabarani. 

Mkaguzi wa Polisi Swai amesema kuwa elimu hiyo imekuwa ikitolewa kwa shule za msingi na sekondari na kupitia vipindi mbalimbali vya redio na vyombo vingine vya habari.
Akielezea vyanzo vya ajali, Swai amevitaja vyanzo hivyo kuwa ni miundombinu duni, makosa ya kibinadamu na vyombo vyenyewe. Amesema mkusanyiko wa vyanzo hivi ndiyo huchangia sana katika ajali za barabarani.

Wakati huohuo, Afisa wa Polisi, Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, Kitengo cha kuzuia Uhalifu, Mariam Mruma wakati akifafanua juu dhana ya kuzuia uhalifu katika makazi na vyombo vya moto amesema kuwa ni vema wananchi kuwa makini na kuchukua tahadhari zote dhidi ya uhalifu katika maeneo yao. Amesema Jeshi la Polisi linatumia maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani kutoa elimu kwa jamii dhidi ya kuzuia uhalifu katika makazi na vyombo vya moto. Amesema katika magari ni vizuri wananchi kukokuacha vitu vya thamani ndani ya magari kwa sababu vitu hivyo vinawashawishi wahalifu kutenda kosa na kushauri pia wanapoyapaki magari yao kuyapati katika maeneo yaliyo wazi na yenye mwanga si maeneo ya vificho. 

Mruma amesema kuwa katika makazi si vizuri kuwakaribisha nyumbani watu wasio fahamika vizuri kwa sababu wanaweza kutumia nafasi hiyo kusoma mazingira ya nyumbani hapo na hatimae kufanya uhalifu. Amesema ni vizuri kwa serikali za mitaa kufahamishwa juu ya ugeni wowote unaofika katika maeneo yao na majirani kwa tahadhali ya kiusalama. Aidha, ametoa wito kwa wazazi kuwaelimisha mtoto wao juu ya kuchukua tahadhari dhidi ya vitendovya udhalilishaji na pindi vinapotokea waweze kutoa taarifa kwao au kwa walimu kwa wale wao shule.
=30=

No comments:

Post a Comment