Thursday, June 6, 2013

UJANGILI KUWAMALIZA TEMBO NCHINI




Ujangili na uharibifu wa mazingira vinachangia sana kupunguza idadi ya tembo duniani na hasa Tanzania kutokana na tembo wengi kuuliwa na kusababisha kuathiri utalii na baadhi ya spishi za wanyamapori kuwa hatarini kupotea.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu katika mkutano wa wadau wa mtandao wa kuboresha ulinzi wa maeneo ya hifadhi kusini mwa Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo Wilaya ya Iringa.

Nyalandu amesema kuwa tafiti zinaonesha kuwa ujangili na uharibifu wa mazingira kwa pamoja vimechangia kupungua kwa idadi ya tembo dunia. Amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu za mwaka 1930 kulikuwepo na tembo milioni 50 na sasa wamepungua na kubaki tembo 402,067 tu. Amesema kuwa ujangili huo unahatarisha kupotea kwa tembo na baadhi ya spishi za wanyamapori zinazotegemea wcolojia waliopo tembo. Amesema kuwa ugangili huo unaathiri utalii pia. 

Naibu waziri wa maliasili amesema kuwa hali hiyo inaashiria kutokuwepo kwa amani na usalama katika hifadhi na uchumi wa nchi. Amesema athari ya kiuchumi ni kubwa kwa sababu ujangili unaathiri uchumi kwa sababu idadi ya watalii wanaotembelea inapungua na hatimae kupunguza pato la taifa. Amesema kuwa ujangili unaathiri sana uchumi wan chi kwa sababu asilimia 17 ya pato la taifa linategemea utalii.

 Akiongelea mbinu za kukabiliana na mtandao wa ujangili unaotumia silaha za kisasa, amesema vi vema kuongeza uwezo wa kukabiliana na njama zinazotishia kupotea kwa tembo katika sura ya dunia. Aidha, ameutaka mkutano huo kujadili kwa kina kutoka na ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili sekta ya ulinzi wa rasilimali za wanyamapori hasa tembo. 

Akielezea malengo ya mkutano huo, mratibu wa mradi wa kuboresha mtandao wa maeneo ya hifadhi kusini mwa Tanzania (SPANEST) ambao pia ni waandaaji wa mkutano huo, Godwell Ole Meing’ataki ameyataja malengo kuwa ni kutoa fursa kwa wadau na viongozi wa ngazi mbalimbali katika mikoa ya nyanda za juu kusini kubadilishana uzoefu, mbinu na mikakati ya kuboresha shughuli za uhifadhi katika mikoa ya nyanda za juu kusini. Lengo jingine amelitaja kuwa ni Kuweka mikakati ya kukabiliana na wimbi la ujangili wa tembo kwa kushirikisha wadau mbalimbali kwa kutambua kuwa hakuna mamlaka moja au mdau ambaye anaweza kukabiliana na janga hili bila ya ushirikiano wa wadau wengine pamoja na Kujadili kwa undani juu ya wimbi la ujangili wa tembo katika maeneo ya hifadhi na mapori ya wanyamapori katika maeneo ya nyanda za juu kusini na nchi kwa ujumla.

=30=



No comments:

Post a Comment