Saturday, February 22, 2014

TATHMINI YA MAZINGIRA KUFANYIKA TENA KABLA YA STENDI YA IGUMBILO



Serikali imelitaka baraza la usimamizi wa mazingira (NEMC) kufanya upya tathmini ya athari za kimazingira katika eneo la Igumbilo inapotarajiwa kujengwa stendi mpya ya mabasi na halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira, Dkt. Binilith Mahenge alipofanya ziara ya kutembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa stendi ya mabasi mjini Iringa.


Waziri wa Nchi OMR- Mazingira, Dkt. Binilith Mahenge (wa tatu kushoto)
 
Dkt. Mahenge amelitaka baraza la usimamizi wa mazingira kufanya upya tathmini juu ya athari za kimazingira na kuwasilisha taarifa hiko kwake. Kauli hiyo imekuja kutokana na mvutano wa muda mrefu sasa baina ya Manispaa ya Iringa na wadau wa maji kwamba mradi huo itaharibu chanzo pekee ya chaji katika mji wa Iringa. Aidha, Dkt. Mahenge amesema kuwa katika kipindi chote manispaa ya Iringa isifanye shughuli zozote za maendeleo katika eneo hilo.

Waziri wa Nchi OMR amesema kuwa lengo la kutembelea eneo la Igumbilo ni kujionea hali halisi kufuatia hoja zilizotolewa na wadau mbalimbali hasa wa maji kuhusu ujenzi wa stendi hiyo. Amesema kuwa baada ya tathmini hiyo wataalam watamshauri kitaalam kwa mujibu wa taaluma. Amesema kuwa maamuzi ya kitaaluma hayawezi kufanywa kisiasa.

Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa, Gervas Ndaki litaka suala hilo lisichukuliwe kisiasa. Amesmea kuwa wapo baadhi ya wafanyabiashara wanaopinga kwa nguvu dhana ya stendi hiyo kuhamishwa mjini na kujengwa eneo la Igumbilo kutokana na maslahi yao ya kibiashara.

Katika taarifa fupi ya mkoa wa iringa iliyowasilsihwa kwa Waziri wa nchi OMR na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu amesema kuwa mradi wa ujenzi wa stendi, unatokana uhitaji mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu ya usafiri katika manispaa ya Iringa na mkoa kwa ujumla. Amesema lengo la ujenzi wa stendi mpya ni kuboresha muindombinu ya stendi ndani ya mji kutokana na misongamano mikubwa katikati ya mji na kukosa nafasi ya kupanua stendi. Amesema kuwa halmashauri hiyo kwa kujenga stendi hiyo inakusudia kuongeza kuboresha vyanzo vya mapato na kukuza shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi wake.

Akiongelea sheria iliyoanzisha mamlaka za maji, Ayubu amesema kuwa sheria hiyo inazitaka mamlaka kusambaza kwa wananchi maji yaliyo safi na salama. Amesema kuwa ikitokea mamlaka imewasambazia wananchi maji ambayo hayako katika viwango mamlaka itakuwa inakiuka sheria. Amesema kuwa wananchi wa manispaa ya Iringa watakuwa kwenye mazingira hatarishi kwa kunywa maji yenye takakemikali na kupelekea madhara kiafya.
=30=
  

No comments:

Post a Comment