Saturday, December 8, 2012

USHIRIKIANO BAINA YA WANANCHI NA WAWEKEZAJI UDUMISHWE



Serikali imepongeza ushirikiano uliopo baina ya wananchi wa kijiji cha makungu na muwekezaji wa kiwanda cha karatasi cha Mgololo (MPM) katika kuchangia maendeleo ya wananchi.

Pongezi hazi amezitoa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipozindua mradi wa maji wa kijiji cha Makungu uliofadhiliwa na kiwanda cha karatasi cha Mgololo wilayani Mufindi.

Dkt. Christine amesema  “ushirikiano baina ya muwekezaji kiwanda cha karatasi cha Mgololo na wananchi ni jambo la kupongezwa sana katika kusogeza huduma za kijamii karibu zaidi na wananchi”. Amesema “mtu anayekupa maji anakupa uhai hivyo mnawajibu wa kutunza na kulinda miundombinu hii ya maji ili muweze kujihakikishia wahakika wa maji na kuufanya mradi huu kuwa endelevu”. Aidha, ametoa wito kwa wawekezaji wengine kuona kuwa wanawajibu wa kuisaidia jamii inayowazunguka kwa kufadhili miradi nashuighuli za kijamii ili kudumisha ushirikiano na uhusiano mwema.

Katika taarifa ya kijiji iliyowasilishwa na Afisa Mtendaji wa kijiji Ephaim Mhelela amesema kuwa kijiji kupata mradi huo kimefanikiwa kupunguza tatizo la maji kutokana na kuwa na bomba moja tu  la maji lililokuwa katika kitongoji kimoja kabla ya mradi huo.  

Amezitaja changamoto katika mradi huo kuwa ni pamoja na ukubwa wa eneo la kijiji jambo linalofanya baadhi ya vitongoji visifikiwe kwa urahisi kutokana na umbali. Changamoto nyingine ameitaja kuwa ni maji kutotosheleza kwa watumiaji wote waliofungiwa bomba kutokana na uchache wa naji yanayopatikana katika tenki na ukosefu wa fedha za kuendeshea mradi ili huduma hiyo iwafikie wananchi wote.

Aidha, ameitaja baadhi ya mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo kuwa ni pamoja na kutumia nguvu kazi ya wananchikwa kuchimba mitaro ya maji pindi pale bomba zinapopatikana za kusambaza maji na kuanzisha mfuko wa maji kwa kuwachangisha wananchi wenyewe.

Mradi huo wa maji unahudumia kijiji cha Makungu chenye vitongoji saba na idadi ya kaya 1,445 na wakazi 6,125, wakiwepo wanawake 3,230 na wanaume 2,895. aidha jumla ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi ni 3202.
=30=

No comments:

Post a Comment