Thursday, September 26, 2013

KLAB YA RAS IRINGA YAANZA SAFARI YA DODOMA




Na Charles Amulike - Iringa
Timu ya kuvuta kamba (wanawake) ya clabu ya RAS Iringa imeanza safari yake kuelekea mkoani Dodoma kushiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Idara Serikali, Mikoa na Wizara (SHIMIWI) ikitarajia kurudi na kikombe.

 Katibu wa Clabu ya SHIMIWI ya RAS IRINGA Neema Mwaipopo (kulia) akimueleza Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa maandalizi ya timu


Hayo yamesemwa na Katibu wa SHIMIWI Katika Ofiis ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Neema Mwaipopo wakati wa kuiaga timu hiyo tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
Mwaipopo amesema kuwa timu hiyo yenye juml;a ya wachezaji 15 inakwenda mjini Dodoma kushiriki mashindano hayo ya SHIMIWI kwa kucheza na timu za ofisi za wakuu wa mikoa, wizara na taasisi mbalimbali za serkali. Ameongeza kuwa timu hiyo imejiandaa vizuri na kutarajia kurudi na ushindi wa kishindo.

Akiongelea changamoto wakati wa maandalizi ya timu hiyo Nahodha wa timu hiyo, Agness Mlula amesema kuwa wachezaji wengi walishindwa kuhudhuria mazoezi kutokana na wengi wao kunyimwa ruhusa kazini. Amesema pamoja na changamoto hiyo, timu hiyo imejipanga vizuri na wanatarajia kurudi na ushindi katika mashindano hayo.

Timu hiyo inatarajia kurudi mkoani Iringa tarehe 6 Oktoba mwaka huu 2013 mara tu watakapomaliza mashindano hayo. 

Nahodha wa Klabu ya RAS IRINGA, Agness Mlula

=30=

No comments:

Post a Comment