Tuesday, September 17, 2013

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa akiongea na ujumbe wa wanazuoni kutoka Angola






Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma 





Mkuu wa Mkoa akiongea na Wafanyabiashara wakubwa wa Mkoa wa Iringa (hawapo pichani) kushoto ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu

Mkuu wa Mkoa akiongea na Wafanyabiashara wakubwa wa Mkoa wa Iringa



Mkuu wa Mkoa wa Iringa (katikati) muda mfupi kabla ya kufunga mafunzo juu ya mbinu za kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja mahala pa kazi kwa watumishi wa TANAPA kutoka hifadhi za kusini yaliyofanyika katika ukumbi wa Neema Craft Manispaa ya Iringa. Kushoto ni Mratibu wa SPANEST, Godwell Meing'ataki na Risala Kabongo (kulia) Afisa Utalii -TANAPA Kanda ya Kusini

Mkuu wa Mkoa wa Iringa akisoma hotuba ya kufunga mafunzo juu ya mbinu za kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja mahala pa kazi kwa watumishi wa TANAPA kutoka hifadhi za kusini yaliyofanyika katika ukumbi wa Neema Craft Manispaa ya Iringa



Mkuu wa Mkoa wa Irinag, Dk.Christine Ishengoma mwenye nguo nyekundu katika picha ya pamoja na wanasena wa TANAPA kanda ya kusini

Makamu wa Rais wa Commercial Seeds Production, Chadjen Ucharattana akimuonesha mahindi Mkuu wa Mkoa wa Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma akiangalia mahindi ya njano toka kwa Makamu wa Rais wa Commercial Seeds Production, Chadjen Ucharattana

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk.Christine Ishengoma (kulia) akitoa taarifa kwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli (kushoto) katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Waziri wa Ujenzi baada ya kukagua barabara ya Iringa-Dodoma (km 260)

Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk.Christine Ishengoma (kulia) wakifuatilia hali ya mambo katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Waziri wa Ujenzi baada ya kukagua barabara ya Iringa-Dodoma (km 260)

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu (kushoto) akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu- Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Sihaba Nkinga (kulia) katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa

Katibu wa Kamati ya Itifaki, Ratiba, mapokezi na Malazi, Neema Mwaipopo (kulia) akichangia mada katika kikao cha maandalizi ya Sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana Kitaifa

No comments:

Post a Comment