Tuesday, December 10, 2013

Mizinga nyuki kwa vikundi



Na Zainab Maeda,Mwananchi  
 Posted  Jumanne,Decemba10  2013  saa 12:8 PM

Iringa.Vikundi saba vilivyopo Kata ya Kiwele na Nduli mkoani Iringa vimekabidhiwa mizinga 100 ya nyuki kwa ajili ya ufugaji nyuki ili kujikwamua kiumaskini.

Akikabidhi mizinga hiyo kati ya mizinga 120 Mshauri wa Maliasili Mkoa wa Iringa, Aloyce Mawere kwenye mkutano uliofanyika katika hicho, aliwataka wanakikundi hao kusimamia sheria zilizowekwa ili kufanikiwa katika ufugaji wa nyuki.

Mawere alisema endapo wanavikundi hao watafanyakazi kwa ushirikiano na jamii inayozunguka misitu ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria zilizopo wataona mafanikio na wataachana na umaskini .

Aliongeza kuwa suala la ufugaji wa nyuki ni ajira tosha kwa vijana na si wazee tu “Naomba jamii nzima ielimike kwamba suala la ufugaji siyo kazi ya wazee peke yao pia ni ajira kwa vijana ambao hawana kazi pamoja na akina mama,hivyo sasa hiyo mizinga mliopatiwa mhakikishe mnaitumia ipasavyo na mnaifanyia kazi siyo masnduku ya nguo hayo,” alisema.
@Mwananchi

No comments:

Post a Comment