Thursday, November 23, 2017

VYAMA VYA SIASA VYAASWA KUFANYA KAMPENI KISTAARABU



Na. Dennis Gondwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-IRINGA
Vyama vya siasa mkoani Iringa vimetakiwa kufanya kampeni za kistaarabu na kuachana na vitendo vya vurugu kwa sababu serikalai ipo macho muda wote.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, mheshimiwa Amina Masenza alipokuwa akiongea katika kipindi cha Sunrise power kinachorushwa na kituo cha redio Nuru cha mjini Iringa jana.
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (picha na maktaba)
Mheshimiwa Masenza ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa alivitaka vyama vya siasa kuendesha kampeni za kistaarabu katika maeneo utakapofanyika uchaguzi mdogo wa madiwani. 

Napenda mkubuke kuwa baada ya uchaguzi maisha yanaendelea kama kawaida. Kila chama lazima kipige kampeni kwa uhuru na ustaarabu bila kusababisha viashiria vya vurugu” alisema mheshimiwa Masenza. 

Aliongeza kuwa mtu yeyote atakayefanya vurugu afahamu kuwa serikali ipo macho itamshughulikia kwa mujibu wa sheria za nchi.

Uchaguzi mdogo wa madiwani unatarajiwa kufanyika tarehe 26/11/2017 katika Kata za Kitwiru na Kimala katika halmashauri za Manispaa na Kilolo mtawalia katika mkoa wa Iringa.
=30=

No comments:

Post a Comment