Thursday, November 23, 2017

WAKULIMA IRINGA WATAKIWA KUTUMIA VIZURI MVUA ZA MWANZO KUPANDIA



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-IRINGA
Wakulima mkoani Iringa washauriwa kuzitumia vizuri mvua zilizoanza kunyesha kupanda kwa kutumia mbegu bora na kuzingatia mistari.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, mheshimiwa Amina Masenza alipokuwa akiongea katika kipindi cha moja kwa moja cha Sunrise power kinachorushwa na kituo cha redio Nuru cha mjini Iringa jana.

Mheshimiwa Masenza alisema kuwa mvua zilizoanza kunyesha zitumike vizuri kwa kupandia. Aliwataka wakulima kuchagua mbegu bora zilizoidhinishwa na wataalam ili waweze kupata mazao bora. Aidha, alishauri kufuata ushauri wa wataalam wa akilimo ili kupata tija kupitia kilimo.

Mkoa wa Iringa ni miongoni mwa mikoa iliyo mstari wa mbele katika kilimo cha mazao ya chakula katika mikoa ya nyanda za juu kusini mwa Tanzania.
=30=

No comments:

Post a Comment