Thursday, September 12, 2013

IRINGA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA JUHUDI




W
atumishi mkoani Iringa wametakiwa kufanya kazi kwa kujituma ili kufikia malengo ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo na matokeo makubwa yanayoonekana.

Kauli hiyo imetolewa na Muu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma alipokuwa akiongea na wafanyakazi wa serikali wilayani Mufindi katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi kupitia utaratibu wake wa kuongea na kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa serikali mkoani Iringa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma

Dkt. Christine amesema kuwa kila mfanyakazi wa serikali lazima afanye kazi kwa nafasi yake na kwa kujituma ili kazi yake iweze kwenda vizuri na kufikia malengo ya serikali ya kuwaletea maendeleo wananchi wake. “Kazi hii ni yetu ya kumuendeleza mwana Mufindi na Iringa kwa ujumla. Hivyo, kila mmoja asipende kufanya kazi kwa kuchungwa ni vizuri kujichunga mwenyewe. Lazima muwe na ratiba zenu za kazi na zenye malengo” alisisitiza Dkt. Christine.

Amesema katika kuhakikisha matokeo makubwa yanapatikana na kuonekana kwa wananchi ni vizuri utaratibu wa matokeo makubwa sasa (BRN) ukaanzia nyumbani ili uweze kufahamika vizuri kuanzia ngazi ya familia. Amesema kuwa kabla ya kufikiria kutoa matokeo makubwa kwa ujumla wake ni vizuri kila mfanyakazi akajiangalia yeye mwenyewe. “Lazima uangalie wewe mwenyewe unaendaje na BRN” alisisitiza Dkt. Christine.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa ameyataja maeneo ya vipaumbele katika utaratibu wa matokeo makubwa sasa kuwa ni maji, kilimo, elimu, uchukuzi, nishati na mapato.

Akiongelea upande wa mapato, amesema kuwa ni lazima halmashauri ya wilaya ya Mufindi ikajipanga vizuri kuhakikisha inaongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani ili iweze kutoa huduma bora kwa wananchi. Amesema “halmashauri hii inasikifa kwa uchapa kazi na ukusanyaji wa mapato hivyo hakikisheni mnaitendea haki halmashauri hii isirudi nyuma”alisisitiza Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa amekemea vikali siasa katika utekelezaji wa utaratibu wa matokeo makubwa sasa (BRN). Amesema “kwenye utaratibu wa BRN msiweke siasa, mpo hapa kwa ajili ya kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2010-2015.siaka kazini ni marufuku, fanyeni kazi za serikali kwa mujibu wa taratibu zilizopo” aling’aka Mkuu wa Mkoa wa Iringa.

Akiongelea maandalizi ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere na Wiki ya Vijana, Mkuu wa Mkoa amewataka wafanyakazi hao kushirikiana na viongozi katika kufanikisha sherehe hizo kubwa mkoani hapa. “Amesema shirikianeni na viongozi wenu ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri wa kuboresha maandalizi na maadhimisho ya sherehe hizi muhimu katika mkoa na taifa letu kwa ujumla”.

Akiongelea miradiitakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru mkoani Iringa, Mkuu wa Mkoa amezitaka wilaya kuhakikisha kuwa miradi ya Mwenye inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaokubalika.
Mkoa wa Iringa umepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere na wikiya Vijana kitaifa kwa mwaka 2013.
=30=


No comments:

Post a Comment