Wednesday, May 18, 2011

Mil 226 ZATOZWA KWA MAGARI KUZIDISHA UZITO

Zaidi ya shilingi milioni 226 zimelipwa kama tozo la uharibifu wa barabara kwa wakala wa barabara Mkoa wa Iringa kutokana na magari kuzidisha uzito imefahamishwa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa matengenezo na ukarabati wa barabara kwa mwaka wa fedha 2010/ 2011 kwa kipindi kinachoanzia Julai 2010 hadi Machi, 2011 na mpango wa mwaka wa fedha 2011/ 2012, katika kikao cha Bodi ya barabara Mkoa wa Iringa, Meneja wa wakala wa barabara (Tanroads) Mkoa wa Iringa, Mhandisi Paul Lyakurwa amesema katika kipindi cha Julai, 2010 hadi Machi, 2011 magari yaliyopimwa katika mizani isiyohamishika iliyopo katika mji mdogo wa Makambako ni 19,104 na kati ya magari hayo magari 2,494 (sawa na asilimia 13) yalizidisha uzito na kulipishwa tozo la uharibifu wa barabara kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Barabara Na. 30 ya mwaka 1973 na Kanuni zake za mwaka 2001 ambapo jumla ya shilingi milioni 226.582 zililipwa .

Meneja wa wakala wa barabara mkoani hapa amekemea vikali tabia inayoendelea kila kukicha ya matumizi mabaya ya hifadhi ya barabara kwa baadhi ya wananchi kuendea kufanya shughuli mbalimbali zikiwemo za kilimo na biashara ndani ya hifadhi ya barabara jambo linalosababisha kuziba kwa mifereji na makalavati na kusababisha maji kutuama barabarani na kusababisha harufu mbaya na magonjwa ya mlipuko. 

Baadhi ya Wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Iringa 


Baadhi ya Wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Iringa 

Aidha, amesema kuwa ofisi ya meneja wa wakala wa barabara mkoa wa Iringa inalo jukumu la kudhibiti uzito wa magari barabarani kwa kutumia mizani isiyohamishika iliyopo katika mji mdogo wa Makambako, Wilayani Njombe.

No comments:

Post a Comment