Wednesday, May 18, 2011

ZAIDI YA BIL NNE ZAKUSANYWA KUTOKA VYANZO VYA NDANI IRINGA

Serikali za Mitaa mkoani Iringa zimefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni nne kutokana na vyanzo vyake vya ndani (own sources).

Akiwasilisha taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo na bajeti kwa mwaka 2010/ 2011 na mapendekezo ya mpango wa matumizi ya muda wa kati na bajeti (MTEF) mwaka 2011/ 2012- 2013/2014, Katibu Tawala Msaidizi- Sehemu ya Mipango na Urabitu, Nuhu Mwasumilwe amesema katika kipindi cha mwaka 2010/2011 Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa zilitarajia kukusanya jumla ya shilingi 7,051,034,698.00 kutokana na vyanzo vyake vya ndani.
Aidha, hadi kufikia mwezi Machi, 2011 jumla ya shilingi 4,476,848,601.96 zimekusanywa ambazo ni sawa na asilimia 63 ya lengo.

Kuhusu mapokezi na matumizi ya fedha zilizodhinishwa mwaka 2010/ 2011, Mwasumilwe amesema kuwa mwaka 2010/2011, mkoa wa Iringa uliidhinishiwa kutumia jumla ya shilingi 142,573,623,000.00 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo.

Aidha, kati ya hizo shilingi 105,256,869,000.00 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi 37,316,754,000.00 kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Hadi kufikia mwezi Machi, 2011 mkoa umetumia jumla ya shilingi 78,469,247,154.70 ambazo ni sawa na asilimia 81 ya fedha iliyopokelewa kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo.

No comments:

Post a Comment