Wednesday, August 3, 2016

JAMII YATAKIWA KULA VIAZI LISHE KUEPUKA UTAPIAMLO



Na Mwandishi Maalum Mbeya

Jamii imehimizwa kutumia viazi lishe vyenye virutubishi kwa lengo la kukabiliana na tatizo la utapiamlo kwa mama wajawazito na watoto.

Akielezea umuhimu wa viazi lishe vyenye virutubishi katika kukabiliana na tatizo la lishe Mkoani Iringa, Afisa kilimo, umwagiliaji na ushirika, Halmashauri ya wilaya ya Iringa, Lucy Nyalu alisema kuwa kutokana na Mkoa wa Iringa kuwa na tatizo la utapiamlo kwa kina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano. 

Alisema kuwa viazi lishe vyenye virutubishi vina rangi ya karoti na wingi wa vitamin A ya kibaolojia inayohitajika kwa kina mama wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Alisema kuwa Halmashauri hiyo imeandaa mashamba ya mbegu kwa lengo la kuzalisha mbegu za kutosha ili wananchi wazipate kwa urahisi.

Akiongelea faida zake, alizitaja kuwa ni majani ya viazi vitamu yana vitamin A na B,madini ya chuma na protini kwa wingi. Faida nyingine vinaweza kutumika kama chakula cha mifugo. Aliongeza kuwa aina mpya ya viazi lishe inaweza kuota popote ha kutoa mazao kwa wingi na vinaweza kuchanganywa na mazao mengine. Pamoja na kutumika kwa chakula, viazi lishe pia vinatumika kutengeneza chapati, maandazi, uji na sharubati.  

Halmashauri ya wilaya ya Iringa kwa kushirikiana na mradi wa Vista kutoka nchini Marakani uliotoa mbegu katika vijiji 36 vya Wilaya ya Iringa ambavyo tayari vinazalisha viazi lishe.

=30=

No comments:

Post a Comment