Saturday, February 22, 2014

TATHMINI YA MAZINGIRA KUFANYIKA TENA KABLA YA STENDI YA IGUMBILO



Serikali imelitaka baraza la usimamizi wa mazingira (NEMC) kufanya upya tathmini ya athari za kimazingira katika eneo la Igumbilo inapotarajiwa kujengwa stendi mpya ya mabasi na halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira, Dkt. Binilith Mahenge alipofanya ziara ya kutembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa stendi ya mabasi mjini Iringa.


Waziri wa Nchi OMR- Mazingira, Dkt. Binilith Mahenge (wa tatu kushoto)
 
Dkt. Mahenge amelitaka baraza la usimamizi wa mazingira kufanya upya tathmini juu ya athari za kimazingira na kuwasilisha taarifa hiko kwake. Kauli hiyo imekuja kutokana na mvutano wa muda mrefu sasa baina ya Manispaa ya Iringa na wadau wa maji kwamba mradi huo itaharibu chanzo pekee ya chaji katika mji wa Iringa. Aidha, Dkt. Mahenge amesema kuwa katika kipindi chote manispaa ya Iringa isifanye shughuli zozote za maendeleo katika eneo hilo.

Waziri wa Nchi OMR amesema kuwa lengo la kutembelea eneo la Igumbilo ni kujionea hali halisi kufuatia hoja zilizotolewa na wadau mbalimbali hasa wa maji kuhusu ujenzi wa stendi hiyo. Amesema kuwa baada ya tathmini hiyo wataalam watamshauri kitaalam kwa mujibu wa taaluma. Amesema kuwa maamuzi ya kitaaluma hayawezi kufanywa kisiasa.

Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa, Gervas Ndaki litaka suala hilo lisichukuliwe kisiasa. Amesmea kuwa wapo baadhi ya wafanyabiashara wanaopinga kwa nguvu dhana ya stendi hiyo kuhamishwa mjini na kujengwa eneo la Igumbilo kutokana na maslahi yao ya kibiashara.

Katika taarifa fupi ya mkoa wa iringa iliyowasilsihwa kwa Waziri wa nchi OMR na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu amesema kuwa mradi wa ujenzi wa stendi, unatokana uhitaji mkubwa wa uboreshaji wa miundombinu ya usafiri katika manispaa ya Iringa na mkoa kwa ujumla. Amesema lengo la ujenzi wa stendi mpya ni kuboresha muindombinu ya stendi ndani ya mji kutokana na misongamano mikubwa katikati ya mji na kukosa nafasi ya kupanua stendi. Amesema kuwa halmashauri hiyo kwa kujenga stendi hiyo inakusudia kuongeza kuboresha vyanzo vya mapato na kukuza shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi wake.

Akiongelea sheria iliyoanzisha mamlaka za maji, Ayubu amesema kuwa sheria hiyo inazitaka mamlaka kusambaza kwa wananchi maji yaliyo safi na salama. Amesema kuwa ikitokea mamlaka imewasambazia wananchi maji ambayo hayako katika viwango mamlaka itakuwa inakiuka sheria. Amesema kuwa wananchi wa manispaa ya Iringa watakuwa kwenye mazingira hatarishi kwa kunywa maji yenye takakemikali na kupelekea madhara kiafya.
=30=
  

SEKTA YA KILIMO KUAJIRI ZAIDI




Sekta ya kilimo inachangia asilimia kubwa katika maendeleo ya taifa na kuajiri watu wengi zaidi nchini. 

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma katika kongamano kati ya serikali na wadau kuhusu siku ya kilimo na usalama wa chakula afrika lililofanyika katika kijiji cha Kaning’ombe wilayani Iringa.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la wadau wa kilimo (ANSAF), Audax Rukonge

 Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma aliyemuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

 Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (watatu kushoto) aliyemuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Dkt. Bilal amesema “kama tujuavyo kilimo ni uti wa mgongo kwa uchumi wa taifa letu. Kilimo hutegemewa na watanzania wengi hasa akina mama, na asilimia 75 ya kipato cha watanzania hutokana na kilimo”. Amesema kuwa kilimo kinasaidia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi wan chi (GDP). Akiongelea umasikini, amesema kuwa pamoja na ukweli kwamba umasikini bado upo nchini kilimo ni suluhisho la mabadiliko kwa watanzania wengi. Amesema kwa msingi huo ni vizuri dira na malengo yaelekezwe katika kilimo cha kibiashara.

Makamu wa Rais amesema kuwa elimu ya uzalishaji bora wenye tija kwa wakulima wadogo itolewe ili waondokane na umasikini. Amesema kuwa kufanya hivyo uchumi wan chi utazidi kukua na kuongezeka kwa ustawi wa jamii.

Dkt. Bilal amesema kuwa serikali itaendelea na jitihada za kuendeleza na kuimarisha sekta ya kilimo nchini. Amesema program ya kuendeleza sekta ya kilimo ilizinduliwa rasmi mwaka 2005/2006 ambapo malengo makubwa ya program hiyo ni kuhakikisha kilimo kinakua kwa asilimia 6 kwa mwaka. Amesema hadi sasa lengo halijafikiwa sababu ukuaji bado ni asilimia 4 tu.  Amesema malengo ya hayawezi kufikiwa bila kuunganisha nguvu na jitihada za pamoja. Ameseme kupitia mkakati wa kilimo kwanza, serikali inaendelea kusimamia na kutekeleza malengo iliyojiwekea na kwa kuzishirikisha sekta binafsi ili kuleta mafanikio makubwa kwa pamoja.

Akiongelea makubaliano na ahadi za Maputo mwaka 2003, Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la wadau wa kilimo (ANSAF), Audax Rukonge amesema kuwa katika kilele cha mkutano wa umoja wan chi za Afrika, AU mwaka 2003 wakuu wan chi walikubaliana kuwa kila nchi itenge kiasi cha asilimia 10 ya bajeti ya kitaifa iingizwe kwenye kilimo.

Amesema kuwa kiwango hicho kilitarajiwa kutosha kuchangia kuongeza uzalishaji na tija, kukuza sekta ya kilimo kwa asilimia 6 kwa mwaka na kuondoa tatizo la njaa na umasikini. Amesema kuwa miaka kumi baadae ni nchi nane tu za Afrika zimetimiza ahadi hiyo na kilimo katika nchi hizo kimekua kwa asilimia 6 na zaidi.

Amesema kuwa unahitajika mtazamo mpya wa kibiashara dhidi ya kilimo tofauti na kisiasa kwa kuwekeza maeneo ya kimkakati na yenye ufanisi mkubwa.

Kongamano hili ni fursa ya kuhakikisha yanapatikana mafanikio katika kilimo kwa kuzikabili changamoto mbalimbali kwa kuzifanyia kazi ili kupata mazao bora yenye tija. Aidha, ni muendelezo wa Kongamano la Umoja wa Bara la Afrika uliozinduliwa na Rais Yayi Boni wa Benini, Mwaka 2012, katika kuendeleza Kilimo na Usalama wa chakula  ili kupata chakula cha uhakika.
=30=