Sunday, February 7, 2016

MKUU WA MKOA ALIPOTEMBEA WAHANGA WA MAFURIKO WA MAPOGOROMkuu wa Mkoa wa Iringa


Hali ya barabara kuelekea Ruaha National Park



Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza (kushoto) akiongozwa na afisa Tarafa ya Idodi

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina masenza akisalimiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mapogoro Faustine Lova

Hali ya barabara iliyomeguliwa na maji




Tafakari ikiendelea


Baadhi ya nyumba zilizoharibiwa kabisa

Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Patrick Golwike








RC MASENZA AWATAKA WAKAZI 300 KUHAMA DHIDI YA MAFURIKO MAPOGORO



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Wahanga wa mafuriko ya mto Mapogoro zaidi ya 300 wametakiwa kuhama katika nyumba zao kutokana na kupata unyevu kiwango cha kuhatarisha maisha yao.

Tahadhari hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipowatembelea wananchi wa Kijiji cha Mapogoro katika Tarafa ya Idodi wilayani Iringa walioathiriwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali wilayani Iringa.
 
Nyumba ya mwanakijiji iliyobomolewa na maji
Masenza alisema “nyumba zilizopata unyevu kutokana na mafuriko ya maji muhame, sitaki kusikia mwananchi hata mmoja amedondokewa na nyumba. Kutokana na nyumba nyingi kujengwa bila misingi na hata zinazojengwa kwa misingi, misingi hiyo inakuwa si imara hivyo hatari ya kudondoka nyumba inaweza kuwa kubwa katika kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha”. Kwa tathmini ya haraka kaya 137 katika kitongoji cha Kitanewa chenye wakazi zaidi ya 300 wanatakiwa kuhama ili kuepukana na kadhia ya mafuriko.   

Akiongelea sababu za mafuriko hayo, Masenza alisema kuwa miongoni mwa visababishi ni uharibifu wa mazingira. Alisema shughuli za kilimo pembezoni mwa kingo za mto na ukataji miti ovyo vinachangia mafuriko ya mara kwa mara maeneo yasiyotarajiwa. Aliwataka waheshimiwa madiwani na watendaji wa kata na vijiji kuwaelimisha wananchi dhidi ya athari ya uharibifu wa mazingira.

Mkuu wa mkoa aliwataka wazazi na wananchi kwa ujumja kuwalinda watoto dhidi ya hatari ya maji hayo. “Ndugu zangu lazima muwe waangalifu kwa watoto wasiende kwenye maji na kusombwa nawaomba sana” alisisitiza.  

Mafuriko hayo yalisababisha maafa ya kusombwa nyumba 14, hekari 717 katika vijiji vya Idodi, Mapogoro na Kitisi, eneo la banio la maji katika mfereji Mapogoro limefunikwa na mchanga na sehemu ya barabara kusombwa na maji na kusababisha magari ya upande mmoja kushindwa kuvuka kuelekea upande wa pili. Aidha, meneja wa Tanroads mkoa wa Iringa, mhandishi Daniel Kindole alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha barabara iliyomegwa na maji inakarabatiwa na kuendelea kupitika kama kawaida. Aliongeza kuwa vifaa kazi zinaendelea kukusanywa ili kupelekwa eneo la tukio kurejesha hali ya kawaida.

Uongozi wa wilaya, mkoa na shirika la msalaba mwekundu wanaendelea ja jitihada za kutafuta mahema na chakula kwa ajili ya kuwasaidia watu ambao nyumba zao zilizolewa na chakula chao kuharibiwa na maji hayo.
=30=