Tuesday, June 2, 2015

SEKTA YA MADINI KUINGIZA WATU 6,000 MKOANI NJOMBE



Christopher Philemon - NJOMBE
Zaidi ya wachina 6,000 wanatarajiwa kuingia katika Mkoa wa Njombe kwenye sekta ya madini hasa makaa ya mawe  na chuma kwenye eneo la Liganga na Mchuchuma wilayani Ludewa.

Hayo yamesemwa  jana kwenye Ukumbi wa Lutheran Makambako na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Rehema Nchimbi alipokuanaongea na watumishi wa Halmashuri ya Mji Makambako, alisema kuwa Mradi wa Linganga  na Mchuchuma unatarajiwa kuanza kuchimbwa makaa ya m awe na chuma hivi karibuni utatoa ajira zaidi ya 30,000 zikiwepo  za wazawa na wageni.

Kutokana na hilo amewataka watumishi wa Halmashauri ya Mji Makambako hasa sekta ya Ardhi kuakikisha wanaweka mipango mizuri ya matumizi ya ardhi na kupima viwanja ili kuwavutia wawekezaji mbalimbali katika ujenzi wa Hoteli za kisasa na halmashuri kuakikisha wanaboresha miundombinu ya Maji na barabara .

Dk. Nchimbi alisema kuwa mpaka sasa shirika la maendeleo ya Taifa (NDC) limeanza mchakato wa uthamini  wa mali za wananchi ili waweze kulipwa fidia kupisha mradi huo.

Aliwataka wananchi wa  Makambako na Njombe kwa Ujumla kujiandaa na ujio wa wageni mbalimbali kwa kufuga kuku, ng’ombe pamoja na mifugo mingine ili  kuweza kuwauzia wageni hao na kuongeza kipato cha familiya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako Hanana Chesco Mfikwa alisema kuwa  wanajiandaa kwa kuwapokea wageni hao kwa kuakikisha wanaweka mipango mizuri ambayo itasaidia wageni kuwekeza zaidi katika eneo la Makambako.
=30=

NJUWASA YAPOKEA BIL. 2.6 KUBORESHA HUDUMA YA MAJI NJOMBE




Christopher Philemon - NJOMBE

Mamlaka ya Maji Mkoa wa Njombe (NJUWASA)  imepokea kiasi cha fedha 2.6 ( 2,577,138,890.00)  bilioni  kutoka Wizara ya Maji  toka mwaka 2013 kwa ajili ya kuboresha hudumaya maji katika Mji wa Njombe.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Mkoa wa Njombe Mhandisi, Daudi Majani amesema kuwa mpaka sasa fedha hizo zimetumika kujenga chanzo cha maji  cha Nyenga,matanti matatu ya maji na utandazaji wa mabomba ya maji ambapo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika mwisho wa mwezi wa saba mwaka huu.

Alisema kuwa mpaka sasa Ujenzi wa kidakio cha maji umekamilika  na ujenzi wa matanki matatu yaliyopo katika maeneo ya Airport, Kambalage, Igeleke na Nzengelendete  na kila tenki linauwezo wa ujazo wa lita 135,000 kila mojaHatua inayoendelea sasa ni utandazaji wa mabomba ya maji katika maeneo mbalimbali ya Mji wa Njombe.
Mradi huo ukikamilika utawezesha kufanya mji wa Njombe kuongeza upatikanaji wa maji kutoka  asilimia 55 hadi 80  na kufanya mji huo kuondoka na huwaba wa maji .

Majani amesema hayo jana kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Rehema Nchimbi alipotembelea vyanzo vya maji na kuangalia mtandao wa maji katika mji wa Njombe.

Mkuu huyo wa Mkoa amezitaka Halmashuri za Mji wa Njombe kushirikiana na mamlaka ya maji Mkoa wa Njombe kuakikisha wanatoa elimu kwa wananchi waliopo kwenye vyanzo vya maji ili kutunza vyanzo vya hivyo.
=30=





DR. NCHIMBI AWATAKA WATUMISHI KUHAMIA WANGING'OMBE



Christopher Philemon - NJOMBE
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk.Rehema Nchimbi amewataka  watumishi walioamishiwa  na walioajiliwa katika halmashuri ya Wiaya ya Wanging’ombe   kuakikisha wamehamia kimakazi  katika wilaya hiyo.

Dk. Rehema Nchimbi,amesema kuwa wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe  watakiwa kupata huduma kutoka kwa watumishi hao na anashangaa kuona watumishi wanaishi Njombe mjini na kufanyakazi katika halmashuri ya wilaya ya Wanging’ombe ambayo ipo zaidi ya umbali wa kilometa 40 kutoka Njombe Mjini.

Nchimbi ametoa wiki mmoja toka leo kuakikisha watumishi hao wawe wameamia na kuishi katika Wilaya hiyo ili kuongeza ufanisi wa kazi na kuwa karibu na wananchi, aliyasema hayo kwenye ukumbi wa halmashuri ya wilaya ya Wang’ingombe wakati akifanya mkutano wa watumishi wa halmshauri hiyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Fedrick Mwakalebela  alisema kuwa Wilaya hiyo inamahitaji yote  muhimu kama vile ofisi, miundombinu ya maji na barabara  na kuwasihi watumishi hao wakikishe wanahamia katika wilaya hiyo haraka iwezekanazo kwani maendeleo ya Wanging’ombe yataletwa na wananchi wa Wanging’ombe kwa kushilikiana na watumishi. 

Mkurungenzi wa Wilaya hiyo Melizedeki Humbe alisema kuwa watumishi wengi katika wilaya hiyo bado wanaishi Njombe mjini lakini wamewaka mikakati ambayo ndani ya wiki mmoja waliopewa kuakikisha watumishi hao wote wanaamia katika wilaya hiyo mpya iliyo anzishwa mwaka 2012.
=30=