Sunday, April 22, 2018

RAS Iringa Netboli yaibugiza Ngorongoro Magoli 54-3



Timu ya Netiboli ya RAS Iringa imeiduwaza timu ya netiboli ya mamlaka ya hifadhi ya taifa ya Ngorongoro kwa kuibugiza magoli 54-3.

Katika mchezo ulioanza kwa kasi kubwa ilionekana dhahiri kabisa kuwa timu ya RAS Iringa imedhamiria kuibuka na ushindi ambapo dakika za mwanzo walionekana kuwapeleka kasi Ngorongoro jambo lilitotafsiriwa na wengi kuwa timu hiyo toka kaskazini mwa nchi ilipata hofu hata kabla ya mchezo.

Mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa chuo kikuu cha kikatoliki cha Ruaha (RUCU) ulishuhuriwa na mamia ya wananchi wapenda michezo.

Baada ya mchezo huo, mratibu wa timu zote za RAS Iringa, Issa Matea alisema kuwa ushindi huo ni salamu za awali kwa timu pinzani. Akiongelea ushindi huo, alisema kuwa ni ushindi huo ni chachu na hamasa aliyoitoa katibu tawala mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu kwa timu hiyo yenye wanadada mahiri.
=30=

RAS Iringa yaiburuza 2-0 MUHAS Kamba



Timu ya kuvuta kamba ya RAS Iringa wanawake imeishinda timu ya kuvuta kamba ya MUHAS wanawake kwa mivuto 2-0. Katika mvutano wa aina yake uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mlandege na kushuhudiwa na mamia ya wapenda michezo wa mkoa wa Iringa na wageni kutoka sehemu mbalimbali waliofika mkoani hapa kwa ajili ya sherehe za Mei Mosi, 2018. 

Akiongea baada ya mvutano huo, Mratibu wa timu zote za RAS Iringa, Issa Matea alisema kuwa timu ya RAS Iringa maarufu kama Kisiki imepata ushindi huo kutokana na mshikamano na kujituma. Alitoa rai kwa timu washindani kuwa chonjo kwa sababu timu hiyo inalojukumu moja tu katika michezo hiyo. 

Alilitaja jukumu hilo kuwa ni kulinda heshima ya mkoa wa Iringa kwa kuibuka na ushindi katika mivuto yote katika michezo ya Mei Mosi, 2018.
=30=