Monday, November 19, 2012



TAMKO LA ASKOFU METHODIUS KILAINI

Askofu Methodius Kilaini

Kwa masikitiko makubwa nimesoma katika gazeti la Mwananchi kwamba nimeiponda safu ya uongozi na sekretariati ya CCM. Mimi sijaongea na gazeti lolote juu ya uongozi wa CCM na wala sina nia au sababu ya kuuponda uongozi huo. 

 Ni vibaya kwa gazeti lo lote lile kutumia jina la mtu kwa kueneza maoni yake. Kama ni waugwana natumaini watasahihisha waliyoyaandika. Nasikitika sana kwa kunikwazwa na hilo. 
 

Askofu Method Kilaini
Bukoba Catholic Diocese