Friday, May 24, 2013

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI BARABARA YA IRINGA-DODOMA




Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa barabara ya Iringa –Dodoma itakapokamilika itasaidia kuinua uchumi wa mkoa wa Iringa na maeneo ya jirani na kuwataka wananchi kuhakikisha kuwa wanaitunza ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Kauli hiyo ameitoa leo mchana katika hotuba yake muda mfupi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Iringa-Dodoma Km 260 kwa kiwango cha lami katika eneo la Migoli.
 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha wageni


Dkt. Kikwete amesema kuwa kukamilika kwa barabara hiyo kutasaidia kuinua uchumi wa mikoa ya Iringa na Dododma na maeneo ya jirani kutokana na kuwa itafungia milango ya kibiashara kwa kurahisisha usafiri kwa abilia na usafirishaji wa mizigo. Akiongelea jukumu la wananchi katika kunufaika vizuri na ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami, Rais Kikwete amewataka wananchi hao kijipanga katika kuongeza uzalishaji mali na kutumia vizuri fursa zilizopo ili kunufaika kiuchumi. 

Rais Kikwete amesema pamoja na minong’ono iliyopo kwa Serikali yake inatumia fedha nyingi sana klatika ujenzi wa barabara badala ya kupeleka fedha hizo katika maeneo mengine, amesema kuwa “kama taifa tumechelewa sana kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya barabara”. Amesema kuwa huo ni uamuzi wa makusudi wa kuwekeza kwa kasi katika miundombinu ya barabara ili kuweza kufungua fursa nyingine nyingi. Amesema kuwa lengo la Serikali ni kuunganisha kwa lami mtandao wa barabara zote nchini.  

Rais Dkt. Kikwete amekemea vikali tabia ya baadhi ya wananchi kuiba mafuta na vifaa mbalimbali katika miradi ya ujenzi wa barabara. Amesema kuwa wizi huo umekuwa ukirudisha nyuma muda wa utekelezaji na ukamilishaji wa miradi ya ujenzi wa barabara nchini. Amewataka wananchi kuwa walinzi dhidi ya wizi wa vifaa hivyo vya ujenzi na mafuta ili kuharakisha ujenzi ujenzi na ukamilishaji wa miradi hiyo.

Akimkaribisha Rais Kikwete kuhutubia, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli amepongeza mahusiano mazuri yanayofanywa na Rais Kikwete kwa wadau mbalimbali wa maendeleo jambo linalowezesha ujenzi wa mirandi mingi ya barabara nchini.
Dkt Magufuli ameseam kuwa mradi uliowekwa jiwe la msingi Iringa-Migori- Fufu Escarpment Km 189 unagharimu zaidi ya Tshs. Bilioni 164. 
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akipokea maelekezo ya mradi 

Akiongelea umakini katika kusimamia miradi ya ujenzi, Waziri wa Ujenzi amesema “Mkandarasi atakayezembea tutamfukuza” na msimamizi mshauri atakayeshindwa kuongoza atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
=30=

Sunday, May 19, 2013



Na Tulizo Kilaga

Wizara ya Maliasili na Utalii imeanza mikutano ya mchakato wa kupokea maoni kutoka kwa watu na makundi mbalimbali kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA).

Mkutano wa kwanza umefanyika leo jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Utalii kampasi ya Bustani kwa kuanza kupokea maoni kutoka kwa viongozi waliowahi kuwa mawaziri,makatibu wakuu na wakurugenzi wa wizara kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka hiyo.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Khamis Kagasheki wakati akifungua mkutano huo alisema Sheria ya Wanyamapori ya Mwaka 2009 inaitaka Wizara kuanzisha Mamlaka ya Wanyamapori kazi ambayo itakamilika Novemba mwaka huu.

Mhe. Waziri alisema kuwa Wizara kwa kutambua umuhimu wa ushirikishwaji imeamua kuanza na viongozi waliowahi kuitumikia Wizara ili waweze kutoa maoni juu ya Sheria na Muundo wa Mamlaka ya Wanyamapori pamoja na Sheria ya Idara ya wanyamapori itakayobaki katika Wizara.

“Nyalaka hizi zimetengenezwa na watu wa ndani ya Wizara wenye uzoefu wa muda mrefu na hivyo tumeona ni vizuri tuwashirikishe ninyi viongozi mliowahi kuitumikia Wizara ili muweze kutoa michango yenu itakayotuwezesha kupata kitu bora kitakachopelekwa katika Baraza la Mawaziri na kisha kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ili Bunge la Novemba tuweze kuiwakilisha ikiwa ina baraka na maoni kutoka kwa kamati ya Bunge ili ipitishwe kama Sheria ya Mamlaka ya Wanyamapori,” alisema Mhe. Waziri.

Kuanzishwa kwa Mamlaka ya Wanyamapori kutasaidia katika kurahisisha usimamizi wa rasilimali watu, kujitegemea kimaamuzi, na kuwa na uwezo wakujiendesha yenyewe bila kutegemea fedha kutoka hadhina.

Miongoni mwa mawaziri waliohudhuria mchakato huo ni Mhe. George Kahama, Mhe. Getruda Mongella, Mhe. Ezekiel Maige, Mhe. Dkt. Juma Ngasongwa, Mhe. Zabehi Mhita na Mhe. Arcado Ntegazwa.

Makatibu wakuu waliofika ni Mhe. Philimon Luhanjo, Mhe. Marten Rumbanga, Mhe. Rose Lugembe, Mhe. Balozi Dkt. Ladislaus Komba, Mhe. Alhaj Muhidin Ndolanga, Mhe. Salehe Pamba na waliowahi kuwa wakurugenzi wa Idara ya Wanyamapori.


Serikali itaendelea kuwekeza katika kukuza mifumo ya kiteknolojia kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya watanzania na dunia kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi wakati akifungua majadiliano ya kikanda ya ushirikiano wa manufaa kwa wote, yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo kikuu cha Ruaha.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Uratibu na Bunge William Lukuvi akihutubia mkutano huo
 
Lukuvi amesema “sote tunatarajia katika maendeleo ya nchi yetu na dunia kwa ujumla. Teknolojia huboresha tija kwa kubadilishana miundo ya mfumo wa uzalishaji kutoka mfumo mmoja na kuingia mifumo ambayo italeta ufanisi na manufaa zaidi katika shughuli za kiuchumi na kijamii”. Amesema “hapo awali Tanzania haikuwekeza sana katika mipango na kuweka utaratibu wa kuchagua, kujitwalia na kuhamisha teknolojia ambayo ingeingizwa kwenye teknolojia yetu kutokana na utafiti na maendeleo”. 

Aidha, amesema kuwa kwa sasa hatua za makusudi zinafanywa na Serikali kuhakikisha kuwa uhamishaji teknolojia unaenda kwa kasi na unakuwa endelevu ikiwa ni pamoja na kupitia mikutano na majadiliano ya ushirikiano wa manufaa kwa wote.  

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Uratibu na Bunge amesema kuwa lengo la majadiliano hayo ni kutoa fursa kwa viongozi wa Serikali ngazi zote kukutana na jumuiya mbalimbali za wananchi ili kujadiliana na kupata maoni kutoka kwa wananchi yatakayopelekwa kwa viongozi tofauti na utaratibu uliozoeleka wa viongozi kutoa maagizo. Akiongelea umuhimu wa ushirikishwaji wa wananchi, amesema kuwa uzoefu unaonesha kuwa wananchi wanaposhirikishwa kikamilifu katika kutoa maoni na wakawa na uelewa mzuri wa masuala yaliyoamuliwa, utekelezaji wake kuwa rahisi. Amesema kuwa ushirikishwaji huo utasaidia katika kutekeleza Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025 na Mipango ya Maendeleo ya miaka mitano.

Katika salamu za Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma amesema kuwa majadiliano hayo yanamanufaa makubwa sana kwa mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya hivyo ni fursa nzuri kwa wadau hao wa maendeleo kujadili na kuainisha fursa za ushirikiano zilizopo na zinazohitajika kuboreshwa kwa manufaa ya wote. Amesema kuwa katika mkoa wa Iringa utaendelea kuboresha mazingira ya utoaji huduma katika kuharakisha mageuzi ya kiuchumi na kijamii katika mkoa. 

Majadiliano ya kikanda ya ushirikiano wa manufaa kwa wote yanafanyika katika kanda nane za Tanznaia Bara na mbili za Zanzibar. Katika kanda ya nyanda za juu kusini majadiliano hayo yamefanyika katika mkoa wa Iringa na kujumuisha mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya.

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma akiusindikiza ujumbe wa Waziri Lukuvi
 
=30=

SERIKALI KUKUZA MIFUMO YA TEKNOLOJIA NCHINI



Serikali itaendelea kuwekeza katika kukuza mifumo ya kiteknolojia kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya watanzania na dunia kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi wakati akifungua majadiliano ya kikanda ya ushirikiano wa manufaa kwa wote, yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo kikuu cha Ruaha.

Lukuvi amesema “sote tunatarajia katika maendeleo ya nchi yetu na dunia kwa ujumla. Teknolojia huboresha tija kwa kubadilishana miundo ya mfumo wa uzalishaji kutoka mfumo mmoja na kuingia mifumo ambayo italeta ufanisi na manufaa zaidi katika shughuli za kiuchumi na kijamii”. Amesema “hapo awali Tanzania haikuwekeza sana katika mipango na kuweka utaratibu wa kuchagua, kujitwalia na kuhamisha teknolojia ambayo ingeingizwa kwenye teknolojia yetu kutokana na utafiti na maendeleo”. 

Aidha, amesema kuwa kwa sasa hatua za makusudi zinafanywa na Serikali kuhakikisha kuwa uhamishaji teknolojia unaenda kwa kasi na unakuwa endelevu ikiwa ni pamoja na kupitia mikutano na majadiliano ya ushirikiano wa manufaa kwa wote.  

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu- Sera, Uratibu na Bunge amesema kuwa lengo la majadiliano hayo ni kutoa fursa kwa viongozi wa Serikali ngazi zote kukutana na jumuiya mbalimbali za wananchi ili kujadiliana na kupata maoni kutoka kwa wananchi yatakayopelekwa kwa viongozi tofauti na utaratibu uliozoeleka wa viongozi kutoa maagizo. Akiongelea umuhimu wa ushirikishwaji wa wananchi, amesema kuwa uzoefu unaonesha kuwa wananchi wanaposhirikishwa kikamilifu katika kutoa maoni na wakawa na uelewa mzuri wa masuala yaliyoamuliwa, utekelezaji wake kuwa rahisi. Amesema kuwa ushirikishwaji huo utasaidia katika kutekeleza Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025 na Mipango ya Maendeleo ya miaka mitano.

Katika salamu za Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma amesema kuwa majadiliano hayo yanamanufaa makubwa sana kwa mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya hivyo ni fursa nzuri kwa wadau hao wa maendeleo kujadili na kuainisha fursa za ushirikiano zilizopo na zinazohitajika kuboreshwa kwa manufaa ya wote. Amesema kuwa katika mkoa wa Iringa utaendelea kuboresha mazingira ya utoaji huduma katika kuharakisha mageuzi ya kiuchumi na kijamii katika mkoa. 

Majadiliano ya kikanda ya ushirikiano wa manufaa kwa wote yanafanyika katika kanda nane za Tanznaia Bara na mbili za Zanzibar. Katika kanda ya nyanda za juu kusini majadiliano hayo yamefanyika katika mkoa wa Iringa na kujumuisha mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya.
=30=