Saturday, September 24, 2011

MKUU WA MKOA WA RUVUMA AKABIDHIWA RASMI OFISI

  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe Said Thabit Mwambungu akisalimiana na watumishi wa ofisi yake mara baada ya kuwasili kwa mara ya kwanza kuanza kazi ya kuuongoza mkoa huo. Kulia kwake ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa, Dtk Anselm Tarimo


 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Said Thabit Mwambungu akisaini kitabu cha wageni katika ofisi yake mpya mara baada ya kuripoti kuanza kazi ya kuongoza shughuli za Serikali mkoani Ruvuma. Kushoto ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Dkt Christine Gabriel Ishengoma ambaye sasa ameahamia Mkoa wa Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Said Thabit  Mwambungu akipokea hati ya Makabidhiano ya ofisi kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Dkt Christine Gabriel Ishengoma tukio hilo lilishuhudiwa na wakuu wa sehemu na vitengo wote.

Picha zote kwa hisani ya Revocatus A. Kasimba, Msemaji wa Mkoa wa Ruvuma

Thursday, September 22, 2011

OFISI YA MKUU WA MKOA WATAKIWA KUDUMISHA MAWASILIANO

Wafanyakazi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa wametakiwa kudumisha mawasiliano baina yao ili kuweza kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na uwepo wa nyufa za kimawasiliano.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akiongea na wafanyakazi wa ofisi yake kwa lengo la kufahamiana na kuboresha utendaji wa kazi.

Dkt. Ishengoma amesema “mawasiliano baina yetu ni nyenzo muhimu sana na kama kutakuwa na ufa wa kimawasiliano hatuwezi kwenda mbali katika utendaji wetu”.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye pia ni mtaalamu wa tasnia ya mbinu za mawasiliano ameitaka timu ya wataalamu wa ofisi yake kuendeleza utamaduni uliojengeka wa kuandaa taarifa na kuziwasilisha taifani kwa wakati ili kuendelea kulijenga jina zuri la Mkoa wa Iringa.

Aidha, amesisitiza usimamizi madhubuti wa fedha za Serikali kuu na Halmashauri. Amesema katika kuzisimamia Halmashauri “si kwa kukaa ofisini tu bali kwa kuzitembelea Halmashauri na kuwafikia walio vijijini”.

Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wafanyazi katika ofiisi yake kushirikiana katika kazi na kutokupigana vikumbo ili kufanikisha utendaji kazi.   
  
Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kuongea na wafanyakazi, Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka amesema kuwa una jukumu la kuziwezesha na kuzijengea uwezo Serikali za Mitaa, kufikisha huduma bora za kiuchumi na kijamii na kuhakikisha amani, usalama na mshikamano unakuwepo.

Wednesday, September 21, 2011

RS WATAKIWA KUZIPENDA KAZI ZAO

Wafanyakazi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa wametakiwa kuzipenda kazi zao na kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kufikia mafanikio ya kiuchumi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akiongea na wafanyakazi wa ofisi yake kwa ajili ya kujitambulisha na kufahamiana na wafanyakazi wake.

Dkt. Ishengoma amesema “napenda kila mmoja apende kazi yake na asitamani kazi ya mwenzake na mambo yatajipa yenyewe hasa akiifanya kwa bidii”.

Aidha, amewataka wafanyakazi hao kuitumia fursa iliyopo Mkoani hapa ya wingi wa vyuo na vyuo vikuu kujiendeleza kitaaluma. Amesema “elimu haina mwisho na wafanyakazi wasisite kujiendeleza kielimu kwa sababu hakuna atakayekusukuma kujiendeleza”. Amesisitiza kuwa kila jambo jema chini ya jua linatokana na malengo madhubuti na kuwataka wafanyakazi hao kutokuridhika na kile walichonacho na kutamani kuendelea zaidi.

Aidha, amewataka wafanyakazi hao kuwa na wivu wa maendeleo. Amesema kinachomsaidia mwanadamu ni nia ya dhati ya kufanikiwa katika njia zilizo za halali.

Awali Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka alitoa pongezi kwa uteuzi wa Dkt. Ishengoma kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Aidha, aliahidi kwa niaba ya wafanyakazi wote kutoa ushirikiano unaostahili kwa Mkuu huyo wa Mkoa ili kuufanya Mkoa wa Iringa uzidi kusonga mbele katika kuimarisha ustawi wa wananchi.

Ikumbukwe kuwa Dkt. Ishengoma aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa akitokea Mkoa wa Ruvuma alipokuwa pia Mkuu wa Mkoa.

Tuesday, September 20, 2011

RC IRINGA AHAIDI USHIRIKIANO KUKUZA PATO LA MWANANCHI


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma ameahidi kushirikiana na viongozi wa Mkoa huo ili kuinua pato la mwananchi wa chini kwa minajili ya kumuinua kiuchumi.

Kauli hiyo ameitoa ofisini kwake wakati akipokea taarifa ya makabidhiano ya Mkoa wa Iringa iliyowasilishwa kwake na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka.

Amesema “ni matumaini yangu kuwa tutakuwa bega kwa bega ili kuhakikisha mwananchi wa chini anainua uchumi wake yeye mwenyewe hasa kwa kuongeza pato lake”.

Dkt. Ishengoma ameitaja changamoto nyingine inayoukabili Mkoa wa Iringa kuwa ni ile ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI. Amesema Mkoa unachangamoto mahususi ya kuhakikisha inateremsha kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI kutoka asilimia 15.7 ya sasa  hadi kufikia angalau asilimia tano. Amesema kuwa japokuwa dawa ya ugonjwa huo bado haijapatikana ila wananchi wenyewe wanayo dawa ikiwa ni pamoja na kubadili tabia.

Aidha, amewataka viongozi wa Mkoa kuangalia maeneo yanayohitaji kufikishiwa zaidi elimu ya maambukizi ya UKIMWI ili kuweza kuinusuru jamii na janga hilo. Amesema kuwa ugonjwa huo ni lazima jitihada za kuudhibiti zifanyike ili kupunguza idadi ya yatima na wajane wanaotokana na matokeo ya ugonjwa huo.

Awali akiwasilisha taarifa ya makabidhiano ya Mkoa wa Iringa, Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka amesema kuwa katika mwaka 2005 pato la Mkoa wa Iringa lilikuwa ni shilingi 867,482,000,000 huku Mkoa ukishika nafasi ya tano kitaifa. Aidha, pato la mkazi lilikuwa ni shinlingi 558,444 na Mkoa ulishika nafasi ya pili kitaifa.

Amesema katika mwaka 2010/2011 pato la Mkoa lilifikia Shilingi  1, 469, 720, 000,000 na pato la mkazi lilikuwa limeongeka kufikia Tshs 859,875 ambalo ni ongezeko la Shilingi 301,431 (54%).

Mpaka amesisitiza kuwa pato la Mkoa linaonekana ni kubwa lakini kwa kiasi kikubwa huchangiwa na mashamba makubwa ya chai, viwanda vya chai, misitu na viwanda vya mbao.

Upande wa Maambukizi ya UKIMWI Katibu Tawala huyo amesema kuwa Mwaka  2003/2004 maambukizi yalikuwa 13.4% na Mwaka 2010/11 maambukizi yamefikia 15.7%. Aidha, hadi Desemba, 2010/11 wananchi 74,632 wenye Virusi vya UKIMWI walioandikishwa kwenye Mpango wa Dawa za kupunguza makali.

Mkoa umekamilisha Mpango wa miaka minne 4 wa kupambana na tatizo la UKIMWI. Mpango huu ni kuanzia Oktoba 1998 hadi Septemba 2012.

MKUU WA MKOA WA IRINGA AWASILI RASMI MKOANI IRINGA

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (mwenye suti nyekundu) akizungumza na watumishi waliojitokeza kumlaki

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (mwenye suti nyekundu) akizungumza na watumishi waliojitokeza kumlaki kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka


 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma (mwenye suti nyekundu) akiwasalimia wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa nje ya jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa 

Mhandisi David Mwakalalile ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Kenneth Komba, Afisa Michezo ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Bibi. Hawa Kalolo ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Avelina Ngonyani, Mwangalizi wa Ofisi ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Neema G. Mwaipopo, Afisa Tawala ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Dennis Gondwe, Afisa Habari ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Bibi. Laurencia Mwanga, Katibu Muhtasi ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake


 Joseph Mnyikambi Afisa Elimu Mkoa ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

 Bw. Adam Swai, Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Uchumi na Sekta za Uzalishaji ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

  Bw. Theophil Likangaga, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Huduma za Jamii ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

  Bw. Vicent James, Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Miundombinu  ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake


 Bw. Barnabas Ndunguru, Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu ni miongoni mwa watumishi waliopata bahati ya kusalimiana ana kwa ana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma siku ya kwanza ya kuripoti kwake

HATIMAE DIMOSO AWAPELEKA MATOMBO

Menrad Dimosso akitoa shukrani zake kwa ujumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na zawadi waliyompatia katika sherehe ya harusi yake iliyofanyika katika ukumbi wa NESTO ZANGIRA- MATOMBO.

 Menrad Dimosso akitoa shukrani zake kwa Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Mipango na Uratibu, Nuhu Mwasumilwe baada ya kukabidhi zawadi ya Mkoa katika sherehe ya harusi yake iliyofanyika katika ukumbi wa NESTO ZANGIRA- MATOMBO.

Bwana harusi Menrad Dimosso na mkewe wakila keki kwa staili walioichagua wao 

 Hiyo ilikuwa miondoko ya KWAITO likiwa ni ombi mahususi la Sam Nyagawa

Mwenyekiti wa Kamati ya Harusi ya Menrad Dimosso Bi. NINA

Baadhi ya watumishi wa RS Iringa waliopata fursa ya kuwa mashuhuda

 Baadhi ya watumishi wa RS Iringa waliopata fursa ya kuwa mashuhuda

Mke wa Menrad Dimosso akirekebisha koti la MZEE baada ya kumvika ndani ya ukumbu wa NESTO ZANGIRA 

 Mke wa Menrad Dimosso akiingia ukumbini

Menrad Dimosso akiingia ukumbini

Monday, September 19, 2011

 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mteule Mhe. Dkt. Christine Ishengoma anatarajiwa kuwasili kesho katika kituo chake kipya cha kazi (Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa) .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa watu wote na kubandikwa katika mbao za matangazo katika Ofisi hiyo kutoka Sehemu ya Utawala inasema kuwa mteule huyo atawasili majira ya saa tano asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki.

Aidha, watumishi wote katika Ofisi hiyo wametakiwa kujitokeza muda huo ili kumlaki.

Mtandao wa www.dennisgondwe.blogspot.com unamtakia kila la kheri katika kituo chake kipya ukiamini KAZI KWANZA KATIKA KUIJENGA IRINGA YENYE NEEMA TELE


Tuesday, September 13, 2011

MKAGUZI NA MDHIBITI WA HESABU ZA SERIKALI MKOANI RUVUMA

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Ludovick Utouh akitoa mada wakati wa mkutano wake na viongozi wa serikali mkoani Ruvuma katika ukumbi wa Songea Club.Walio mstari wa mbele ni wakuu wa wilaya za Namtumbo,Mbinga na Songea


Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimaliwatu Humphrey Paya akichangia mada wakati wa mkutano kati ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali uliofanyika leo katika ukumbi wa Songea club Manispaa ya Songea.
CAG AZIAGIZA SEKRETARIATI ZA MIKOA KUSIMAMIA FEDHA ZA UMMA KATIKA HALMASHAURI
Na. Revocatus Kassimba, Ruvuma
Sekretariati za mikoa hapa nchini zimeagizwa kuzingatia Sheria,kanuni na taratibu za utumiaji wa fedha za serikali ili kuhakikisha Halmashauri zinapunguza hoja za ukaguzi wa Hesabu.
Agizo hilo limetolewa leo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG)  Bw.Ludovick Utouh alipokuwa akiongea katika mkutano na viongozi wa serikali mkoani Ruvuma katika ukumbi wa Songea club.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) Bw.Ludovick Utouh akiongea katika mkutano na viongozi wa serikali mkoani Ruvuma katika ukumbi wa Songea club.Kushoto ni Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanali Mstaafu Edmund Mjengwa na kulia ni kaimu Katibu Tawala Mkoa Dkt Anselm Tarimo
Bw Utouh amesema kuwa licha ya udhaifu wa  usimamizi wa sekeretariati za mikoa uliopo  kuhusu Sheria kutokuweka wazi wazi mahusiano ya utendaji kazi kati ya Sekretariati za Mikoa na Halmashauri ni budi fedha za serikali zikasimamiwa kikamilifu na Maafisa Masuhuli wa Serikali katika mikoa
Aliongeza kusema licha ya Sekretariati za Mikoa kutokuwa na vitendea kazi na bajeti ya kutosha kwa ajili ya usimamizi wa Halmashauri hazimaanishi kuacha jukumu lake la kusimamia utekelezaji wa shughuli za Maendeleo katika halmashauri kwani fedha nyingi za serikali hupelekwa huko kusaidia wananchi.
“Wananchi wetu wengi wako vijijini na ndiko miradi mingi ya Maendeleo inakoelekezwa na serikali na kugharimia fedha nyingi hivyo ukaguzi na ufuatiliaji ni muhimu ukapewa kipaumbele na mikoa yote” alisema Bw Utouh
Aibainisha wazi kuwa Miradi mingi ya maendeleo inatekelezwa kwenye ngazi za uongozi za vijiji kulingana na sera ya D by D hivyo ufuatiliaji na tathmini ya thamani ya fedha ni muhimu hasa vijijini.
Bw .Utoh ametaja sababu zinazopelekea halmashauri nyingi hapa nchini kupata hati zisizoridhisha  kutokana na fedha za serikali kutumika vibaya kuwa ni sheria za serikali za Mitaa kuwa za zamani hivyo kukinzana na Sheria zingine.
Aidha alitaja sababu zingine kuwa ni utaratibu wa kutuma fedha kwenye halmashauri kutokuwa na maelezo ya wazi na pia mfumo kutokuwa na utaratibu wa adhabu kwa wasiofikia Malengo yaliyowekwa.
Bw.Utouh amesema kuwa ukaguzi umebaini ya kuwa katika Mikoa mingi hapa nchini hakuna uhusiano mzuri wa utendaji kazi kati ya Sekretariati ya Mkoa, Halmashauri na Uongozi wa Vijiji hasa inapohusu usimamizi wa fedha na raslimali za umma.
Ili kutekelezan kwa makini usimamizi wa mapato na matumizi ya serikali  mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za serikali amewataka viongozi wa kisiasa kufuatilia taarifa zote za miradi ya Maendeleo na kuhoji matumizi ili uadhirifu wa fedha za umma ukome
Hata hivyo Bw Utouh ameaagiza wakurugenzi wa Halmashauri nchini kuwawezesha  waweka Hazina na Wahasibu wafundishwe juu ya viwango vya uhasibu vya kimataifa ili Kuboresha kazi zao itakazosaidia kupatikana kwa taarifa sahihi za Hesabu za Halmashauri .

Saturday, September 10, 2011

Reaction of World Leaders 

"On September the eleventh, enemies of freedom committed an act of war against our country. Americans have known wars but for the past 136 years, they have been wars on foreign soil, except for one Sunday in 1941.  Americans have known the casualties of war but not at the center of a great city on a peaceful morning. Americans have known surprise attacks but never before on thousands of civilians. All of this was brought upon us in a single day and night fell on a different world, a world where freedom itself is under attack.... 
We are not deceived by their pretenses to piety. We have seen their kind before. They are the heirs of all the murderous ideologies of the 20th century. By sacrificing human life to serve their radical visions - by abandoning every value except the will to power - they follow in the path of fascism, and Nazism, and totalitarianism. And they will follow that path all the way, to where it ends: in history's unmarked grave of discarded lies.... The course of this conflict is not known, yet its outcome is certain. Freedom and fear, justice and cruelty, have always been at war, and we know that God is not neutral between them.  This is not, however, just America's fight. And what is at stake is not just America's freedom. This is the world's fight. This is civilization's fight. This is the fight of all who believe in progress and pluralism, tolerance and freedom....Great harm has been done to us. We have suffered great loss. And in our grief and anger we have found our mission and our moment. Freedom and fear are at war. The advance of human freedom - the great achievement of our time, and the great hope of every time - now depends on us. Our nation - this generation - will lift a dark threat of violence from our people and our future. We will rally the world to this cause, by our efforts and by our courage. We will not tire, we will not falter, and we will not fail... I will not forget this wound to our country, or those who inflicted it. I will not yield - I will not rest - I will not relent in waging this struggle for the freedom and security of the American people." -President George W. Bush


 " I was stricken by news and television pictures coming from the United States this morning. It is impossible
 to fully comprehend the evil that would have conjured up such a cowardly and depraved assault upon
 thousands of innocent people.  There can be no cause or grievance that could ever justify such unspeakable
 violence.  Indeed, such an attack is an assault not only on the targets but an offense against the freedom and
 rights of all civilized nations. "  - Prime Minister Jean Chrétien, Canada 
 "There can be no doubt that these attacks are deliberate acts of terrorism, carefully planned and coordinated
 and as such I condemn them utterly. Terrorism must be fought resolutely wherever it appears."  - United
 Nations Secretary-General Kofi Annan


 Queen Elizabeth II said she was watching developments in "growing disbelief and total shock."
 "this terrible tragedy.... the entire  international community should unite in the struggle against terrorism 
 this is a blatant challenge to humanity." - President Vladimir Putin, Russia
 "France is deeply upset to learn of the monstrous attacks that have just struck the United States....  In these
 terrible circumstances, all French people stand by the American people. We express our friendship and
 solidarity in this tragedy." - President Jacques Chirac, France
 "Our hearts are with you and we are ready to provide any assistance at any time....This is a war between good
 and evil and between humanity and the bloodthirsty."  -Prime Minister Ariel Sharon, Israel
 "It was with horror that I learned of the abominable terrorist attacks on the World Trade Center in New 
 York
and the Pentagon in Washington in which so many innocent people have lost their lives. My
 government staunchly condemns these acts of terrorism. The German people are at the side of the United 
 States of America
in this difficult hour. I wish to express my deep-felt condolences and complete solidarity 
 to you and  the American people. Our thoughts and prayers go out to the victims and their families." 
 -Chancellor Gerhard Schroeder, Germany
 "There have been the most terrible, shocking events taking place in the United States of America within the last couple of hours.... We can only imagine the terror and carnage there and the many, many innocent people who have lost their lives .... perpetrated by fanatics who are utterly indifferent to the sanctity of human life, and we, the democracies of this world, are going to have to come together to fight it and eradicate this evil completely from our world." -Prime Minister Tony Blair, United Kingdom 
 "An attack on one is an attack on all" -NATO Secretary-General Lord Robertson after the alliance's 19 
 ambassadors decided to invoke Article 5 of the NATO charter for the first time in the alliance's history.
"this outrageous and vicious act of violence against the United States is unforgivable." -Prime Minister
 Junichiro Koizumi, Japan
 "Irrespective of the conflict with America it is a human duty to show sympathy with the American people, 
 and be with them at these horrifying and awesome events which are bound to awaken human 
 conscience." - Moammar Gadhafi, Libyan Leader
 "We want from here to express our solidarity and our support to all the victims of these acts of terrorism
 and  their family members. We reiterate our complete, emphatic rejection of all forms of violence and all
 forms of terrorism." - President Vicente Fox, Mexico
 "I send my condolences, and  the condolences of the Palestinian people to American President Bush and
 his government and to the American people for this terrible act....We completely condemn this serious 
operation.... We were completely shocked.... It's unbelievable, unbelievable, unbelievable."  -Palestinian 
Authority President Yasser Arafat 
 "Egypt firmly and strongly condemns such attacks on civilians and soldiers that led to the deaths of a 
 large number of innocent victims." -President Hosni Mubarak, Egypt
 "I wish to express, on behalf of the Chinese Government and people, our deepest sympathy and solicitude
 to you and, through you, to the Government and people of the United States. I wish also to extend
 our condolences to the families of the victims. The Chinese Government has consistently condemned and 
 rejected all forms of terrorist violence." -President Jiang Zemin, China
  Mohammad Khatami, President of Iran, said he felt "deep regret and sympathy with the victims." and said
 "it is an international duty to try to undermine terrorism."
 "these monstrous criminals  have demonstrated a vile and brutal affront against humanity." -Prime Minister 
 Silvio Berlusconi, Italy
 "Cuba laments and expresses its profound sadness for the loss of so many innocent lives and expresses our
 absolute rejection of acts of terrorism, wherever they may come from."  -Foreign Minister Felipe Perez
 Roque, Cuba
 "I hurry to express to you and your fellow citizens my profound sorrow and my closeness in prayer for the
 nation at this dark and tragic moment." -Pope John Paul II, Vatican City
 "no doubt this is a result of injustice the U.S practices against the weak in the world." - Sheikh Ahmed Yassin, 
 Spiritual Leader of Hamas
 "It is premature to level allegations against a person who is not in a position to carry out such attacks,
  it was a well-organized plan and Osama has no such facilities."" -Mullah Abul Salam Zaeef,
  Taliban's Ambassador to Pakistan

 "And just as your beautiful skyscrapers were destroyed and caused your grief, beautiful buildings and 
 precious homes crumbled over their owners in Lebanon, Palestine, and Iraq by American weapons....
 Americans should feel the pain they have inflicted on other peoples of the world, so as when they suffer, they will find the right solution and the right path. " - President Saddam Hussein, Iraq
North Korea called the attacks "tragic," adding that it "is opposed to all forms of terrorism." 
 "No, we did not do this, and we are not with you." -Ayatollah Khamenei, Iranian Supreme Religious Leader
 "This place may be bombed, and we will be killed. We love death. The U.S. loves life. That is the big 
 difference between us." -Osama bin Laden, to a visiting reporter 26 Nov 2001.
source of news is www.worldstatesmen.org

Wednesday, September 7, 2011

SHEREHE YA HARUSI YA BW N BIBI. SAMWELI S. NYAGAWA

 Wenyewe sasa Bw n Bibi. Samweli S. Nyagawa wakiingia ukumbini

Keki ya uhakika shukrani kwa mpambaji 

Mama Harry...! Mama Harry...! Mama Harry...! 

Mwenyewe Neema G. Mwaipopo kama sio wa nchi hii vile!

Bw na Bibi. Jonas Kilima na mtoto wao wakiwa katika tabasamu ukumbini 

Mr n Mrs. Dr. E. Mpuya ambaye pia ni Mkuu wa Kazi wa Bw. Samwel Nyagawa 

Mama Chota na ujumbe wake katika ukumbi wa RUCO kushuhudia sherehe ya harusi ya Sam 


Familia ya Mama Mdemu ikiingia ukumbini 

Mr n Mrs. Prof. S. Nyagawa wakiingia ukumbi wa chuo cha RUCO katika sherehe ya harusi ya kijana wao wa mwisho Samwel Nyagawa 

Bibi. Modesta Kaweni na Bibi Kiula katika sherehe ya harusi ya Sam

Bibi. Kiula, Bibi. Ambrose na Bibi. Chambala wamejiachia katika sherehe ya Harusi ya kijana wao Samwel S. Nyagawa 

Mr n Mrs. Bahati F. Golyama wakijinafasi katika sherehe ya Harusi ya Bw n Bibi. Samwel S. Nyagawa