Monday, July 30, 2012

KKKT IRINGA WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA SENSA




Washarika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, usharika wa Iringa Mjini wametakiwa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa mabadiliko ya uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kufanikisha uundwaji wa Katiba hiyo kwa kujumuisha mapendekezo ya watu wengi zaidi.

Wito huo umetolewa na mgeni rasmi Dkt. Christine Ishengoma katika harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa kanisa kuu la mtaa wa Wilolesi iliyofantik Katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzanaia, Usharika wa Iringa Mjini leo.

Dkt. Christine ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, amesema “ndugu zangu Washarika natoa rai kwenu kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha na kuwaeleza waumini wengine na wananchi kwa ujumla ili washiriki katika mchakato huu kwa kutoa elimu na hamasa”. Amesema “napenda kutoa wito kwenu wote kuwa huru kutoa maoni yenu Tume itakapopita katika maeneo na kukusanya maoni yenu”. 

Amesema kuwa baadhi ya wananchi wanalalamika kuwa Katiba ya sasa inamapungufu kadhaa, hivyo huu ndio wakati wao wa kutoa maoni yao ili hayo mapungufu yaweze kufanyiwa kazi na kuingia katika Katiba mpya. Amesema hili litafanikiwa pale tu, washarika na wananchi watakapojitokeza kwa wingi kutoa maoni yao pindi tume ya kukusanya maoni itakapopita katika maeneo yao. Amewataka kuwa makini katika kusikiliza tarehe na sehemu ambazo mikutano hiyo itakuwa ikifanyika ili waweze kuwasilisha maoni yao kwa tume hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka wananchi kuwa huru katika kutoa maoni yao na kuwahakikishia kuwa ukusanyaji wa maoni hayo hauhusiani na itikadi yoyote. Amesema ili Katiba hiyo mpya iwe ya mafanikio ni lazima maoni ya wananchi wengi yaweze kukusanywa na mafanikio hayo yanatokana tu, na wananchi kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao kwa tume hiyo.  
=30=

TAASISI ZA DINI ZATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO ILI KUFANIKISHA SENSA




Serikali Mkoani Iringa imeomba ushirikiano kutoka kwa viongozi wa dini katika kuhakikisha kuwa elimu ya kutosha na hamasa vinatolewa ili uelewa huo uwafikie waumini na wananchi wengi kwa ujumla.

Ombi hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akiendesha zoezi la harambee ya ujenzi wa kanisa kuu la mtaa wa Wilolesi mjini hapa katika ibada ya kwanza iliyofanyika katika kanisa kuu, usharika wa Iringa Mjini.

Dkt. Christine amesema kuwa Tanzania itafanya Sensa ya Watu na Makazi tarehe 26 Agosti, mwaka huu na kuendelea kwa takriban siku saba. Amesema “Sensa ya Watu na Makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua na kusambaza takwimu za kidemografia, kiuchumi na kijamii kuhusiana na Watu wote na Makazi yao katika nchi kwa kipindi maalum”. Amesema kuwa Sensa hiyo ni zoezi lenye lengo la kupata idadi ya watu wote katika nchi, kwa umri na jinsi, mahali wanapoishi, hali yao ya elimu, hali ya ajira, hali ya vizazi na vifo na hali ya makazi. 

Akiongelea malengo ya Sensa hiyo, Mkuu wa Mkoa amesema “Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 inalenga kutathmini utekelezaji wa Mipango yetu mikubwa ya Maendeleo ambayo imekuwa ikitekelezwa katika kipindi kilichopita. Mipango hiyo ni pamoja na Mkakati wa Kupunguza Umasikini na Kukuza Uchumi Tanzania na Mpango wa Kupunguza Umasikini Zanzibar”.

Akiongelea nafasi ya kanisa katika kufanikisha Sensa hiyo, Dkt. Christine amesema “napenda kuongelea nafasi ya Kanisa katika kuhakikisha Sensa ya Watu na Makazi inafanikiwa. Ni kweli kuwa Kanisa linalo jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa zoezi hili linafanikiwa kwa sababu takwimu hizo ndizo zitakazoiwezesha Serikali kutambua hali halisi na mahitaji halisi ya huduma zilipo katika maeneo yenu hivyo kuingizwa katika Mipango ya Maendeleo ya Taifa”. Amesema “kwa msingi huo, ninawaomba sana kuwahamasisha waumini na wananchi kwa ujumla ili wahesabiwe na wahesabiwe mara moja tu, ili takwimu zitakazokusanywa ziwe sahihi”.

Ameyataja mambo muhimu ya kutiliwa mkazo wakati wa kuwahamasisha washarika na wananchi kwa jumla kuwa ni tarehe ya Sensa, umuhimu wa Sensa na yatakayojiri wakati wa zoezi la kuhesabu watu. Sensa hiyo ya Watu na makazi inaongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Sensa kwa maendeleo, jiandae kuhesabiwa’.

Tuesday, July 24, 2012

PROF. J.A. MILLS AFARIKI DUNIA



Taarifa kutoka afisi ya rais zinasema kuwa alifariki ghafla baada ya kupelekwa hospitali siku ya Jumatatu usiku.
Prof. John Attah Mills
Kifo cha rais wa taifa la pili duniani kwa ukuzaji wa cocoa kimekuja wakati alikuwa anajiandaa kupogania tena urais.Msaidizi wake pia amethibitisha kufariki kwa kiongozi huyo.

Rais Prof. John Attah Mills ambaye husafiri mara kwa mara kwenda ng'ambo kwa matibabu alifariki muda mfupi baada y kupelekwa katika hospitali moja mjini Accra , Ghana.

Ni hivi majuzi tu rais huyo alisafiri hadi Marekani kwa kile kilichosemekana kwa ni uchunguzi wa kawaida wa afya yake.

Kwa muujibu wa katiba ya Ghana, Makamu wa Rais  John Dramani Mahama anatarajiwa kushikilia hatamu za uongozi hadi uchaguzi wa urais utakapofanywa.

Ghana ilikuwa inatarajiwa kwenda katika uchaguzi mkuu mwezi Disemba mwaka huu ambapo Prof. John Attah Mills alikuwa ametangaza nia yake ya kutetea uadhifa wake.

Wakati wa uongozi wake, uchumi wa Ghana uliimarika na demokrasia kupanuka zaidi.

" Ni kwa masikitiko makuu na kwa moyo mzito... Tunatangaza kifo cha ghafla cha rais wa jamhuri ya Ghana " taarifa iliyotumiwa shirika la Reuters kutoka ofisi ya rais ilisema.

Taarifa hiyo ilisema kuwa Rais Prof. Mills mwenye umri wa miaka 68 alifariki saa chache tu baada ya kupelekwa hospitali.

Hata hivyo hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa.
Lakini msaidizi wake mmoja ambaye hakutaka kutajwa, alisema kuwa Rais Prof. John Attah Millis alisikika siku ya Jumatatu akilalamika kwa anaumwa.

Hali yake ilizorota na hatimae kufariki mapema siku ya Jumanne.
Prof. Mills , anajulikana kwa kuanzisha uchimbaji wa mafuta nchi Ghana.

Chanzo: BBC SWAHILI



 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA



MKOA WA IRINGA:
Simu Na.  026 2702191   
Fax    Na. 026 2700310
 
  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,
   S. L. P. 858,

   IRINGA



YAH: MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA TAREHE 25 JULAI, 2012.


Wafanyakazi wote wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa na Wananchi wa Manispaa ya Iringa kwa ujumla mnatangaziwa kuwa Tarehe 25 Julai, 2012 kutafanyika Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa katika Uwanja wa Bustani ya Manispaa ya Iringa saa 2:00 Asubuhi.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa atakuwa Mgeni Rasmi katika Maadhimisho hayo.
Unatakiwa kuhudhuria katika Maadhimisho hayo muhimu kwa Kudumisha Historia ya Ukombozi wa Nchi yetu.



Imetolewa na:
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa
S.L.P 858
IRINGA


Thursday, July 19, 2012

SPEECH BY HIS EXCELLENCY, DR JAKAYA MRISHO KIKWETE, THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, ON THE OCCASION OF THE OFFICIAL OPENING OF THE ALMA SECRETARIAT OFFICE IN DAR ES SALAAM, 18TH JULY, 2012





Your Excellency, Ellen Johnson Sirleaf, the President of
       the Republic of Liberia;
Honorable Hussein Ali Mwinyi (MP), Minister of
     Health and Social Welfare;
Dr. Rufaro Chatora, Representative of the World
      Health Organization in Tanzania;
Members of the Diplomatic Corps;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen;

Once again it is my pleasure to welcome you, Madame President, to Tanzania. We thank you very much for accepting my invitation to visit us and agreeing to launch the African Leaders Malaria Alliance (ALMA) offices.

Ladies and Gentlemen;
As many of you know, Africa is the continent most affected by malaria. The disease accounts for 85 percent of malaria cases and 89 percent of malaria deaths worldwide, the majority being children under five years of age and pregnant women. Malaria also retards economic growth of the continent and over-burdens the already overstretched health care services in most African countries.  In fact, malaria has been estimated to cost Africa at least US Dollars 12 billion every year.  Despite these devastating effects of malaria, the scourge can be prevented, controlled and eventually eliminated in Africa.

It is for this reason that in September, 2009, some African leaders gathered at the United Nations Headquarters in New York, United States of America and decided to form an alliance to intensify the fight against malaria and ultimately end malaria-related deaths in Africa.  We formed a coalition to mobilize and coordinate our collective efforts as well as mobilize international support from nations, international organizations as well as institutions and persons of goodwill in the fight against malaria.  We formed the African Leaders Malaria Alliance, in short ALMA.   I was privileged and honoured to be the first Chairman of ALMA until January, 2012 when I handed over to my dear sister Her Excellency President Ellen Johnson Sirleaf of the Republic of Liberia who is our chief guest at this event today.

Your Excellency;
Since its inception, ALMA has been very instrumental in enhancing global partnership and mobilizing substantial resources to fight the scourge of malaria in Africa. As a result, many African countries have been able to scale up malaria interventions and reduce malaria related deaths and the social burden of the disease it engenders. One of the landmark achievements was the adoption of the ALMA Scorecard for Accountability and Action in September, 2011.  In fact, this new innovative way of tracking progress on key malaria indicators establishes transparency and accountability framework for rapid response to emerging issues and consolidates national data from multiple sources.

I would like to take this opportunity to thank all the African leaders for their commitment and efforts to fight malaria; and to all our partners for their immense contribution and support towards our noble goal of eradicating malaria-related deaths by 2015. I know our target is ambitious but doable if we scale up interventions on the fight against malaria. I commend our very able ALMA Secretariat, under the leadership of Madam Joy Phumaphi, for the good work of building the institution and coordinating our efforts. Without the dedicated services rendered by staff of the Secretariat, we would not be here today celebrating one of our achievements. Thank you very much Madame Joy, Saleemah, Dr. Halima, Melanie, Kwame, Samson and Mary for your wonderful service to our dear continent.

 And above all, ladies and gentlemen, I want to sincerely thank President Ellen Johnson Sirleaf for her leadership in steering the affairs of ALMA. Within a very short time, her vibrancy and visionary leadership have proven to be an asset in the fight against malaria in Africa. I am sure by the time her tenure ends, Africa will leap several steps forward in the fight against malaria. Tanzania will continue to support you and the work of ALMA until we attain our lofty objective.

Your Excellency;
Invited guests;     
Ladies and Gentlemen;

On behalf of the government of the United Republic of Tanzania, it is now my pleasure to hand-over new offices of the ALMA Secretariat here in Dar es Salaam. These offices are available to ALMA as a contribution of the government and the people of the United Republic of Tanzania to ALMA in recognition of its efforts in fighting Malaria in the continent.    
Finally, it is now my singular honor and privilege to welcome you Madame President to the podium to deliver your remarks and then launch the ALMA Secretariat offices here in Dar es Salaam.
Madam, welcome!

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete together with  the Liberian  Presdent Ellen Sirleaf Johnson pose for a group photograph with some dignitaries who attended the official opening ceremony of the ALMA offices in Dar es Salaam this morning.The ALMA offices are located at the institute of Medical Research NIMRI Headquarters  along Luthuli Avenue in Dar es Salaam.



Saturday, July 14, 2012

DR. ASHA-ROSE MIGIRO: “FURSA YENYE TIJA: TAFAKURI YA UTUMISHI WANGU KAMA NAIBU KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA”




Hakika kila chenye mwanzo hakikosi mwisho, na kila mwisho wa jambo moja huwa mwanzo wa jingine. Ingawa huenda ni mapema sana kwangu kutoa tafakuri kamili ya muhula wangu katika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, hapana shaka kabisa kuwa nafasi hiyo imenipa uzoefu maridhawa. Namshukuru Katibu Mkuu BAN Ki-moon kwa kunipa fursa hii, kuniamini na kwa ushirikiano mkubwa wakati wote wa utumishi wangu.


Kukitumikia chombo hiki cha kimataifa kwa muda wa miaka mitano na nusu mfululizo ni heshima ya pekee ambayo daima nitaienzi kama kilele kimojawapo cha maisha yangu ya utumishi wa umma. Kila siku niliyoitumia katika Umoja huo ilikuwa ni darasa la kusukuma mbele mipaka ya ujuzi na elimu. Nimepata kufahamu mengi zaidi kuhusu Shirika lenyewe; kuhusu dunia na watu wake, lakini pia kufahamu ukomo wa uwezo wa Umoja wa Mataifa katika kushughulikia changamoto mbali mbali zinazoikabili dunia yetu.

Dr. Asha-Rose Migiro

Utumishi wangu katika Umoja wa mataifa ulikuwa fursa adhimu iliyonipa uzoefu wa pekee. Kazi hii imeujaza moyo wangu na unyenyekevu wa dhati kwani niliingia Umoja wa Mataifa wakati ambapo dunia inachagizwa na madhila makubwa makubwa yakiwemo maradhi, umaskini wa kupindukia, kutokuwapo kwa usawa wa kijinsia, kuongezeka kwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto; na changamoto nyingine nyingi. Kwa muktadha huu ilikuwa fursa ya pekee kuchangia juhudi za pamoja za kuimarisha Umoja wa Mataifa katika kutekeleza majukumu yake katika kipindi cha mazingira magumu ya kimataifa yaliyojaa changamoto za kipekee kabisa.


Daima nitaendelea kushukuru na kuthamini kwa dhati jinsi Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Serikali na Watanzania wenzangu walivyonitia moyo na kunienzi katika kipindi chote nilichokuwa Umoja wa Mataifa. Familia yangu, ndugu na marafiki walikuwa karibu nami kwa dua na kunitia nguvu wakati wote wa utumishi wangu. Nawashukuru sana.


Hapana shaka kazi yangu katika Umoja wa Mataifa imeniwezesha kufahamiana kwa karibu na viongozi wengi wa kimataifa na pia watu mbali mbali waliopata mafanikio makubwa duniani. Nimeweza kufahamu kwa undani thamani ya michango yao katika kujenga amani na ustawi wa dunia.


Zaidi ya yote, sitasahau hisia nilizopata kila nilipokutana na watu wanyonge waliokuwa wanahitaji msaada wa Umoja wa Mataifa. Nitakumbuka daima tabasamu ya mwanamke mmoja niliyekutana naye katika moja ya ziara zangu barani Afrika nilipotembelea zahanati mojawapo kati ya kadhaa zinazofadhiliwa na Umoja wa Mataifa. Mama huyo mwenye watoto sita, alikuwa amekikumbatia kitoto chake kimoja kilichokuwa nyonde nyonde; lakini alikuwa na tabasamu iliyojaa faraja na matumaini kwa kuwa alikuwa amefanikiwa kupata bure dawa za kunusuru maisha ya mwanawe.


Maendeleo

Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa iliasisiwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 1997 kwa madhumuni ya kuongeza ufanisi wa utendaji wa Sekretariati na kuimarisha uongozi wa Umoja Mataifa katika medani za uchumi na maendeleo ya jamii. Majukumu ya Naibu Katibu Mkuu yaliongezeka kadri Shirika lilivyokuwa linapanua shughuli zake. Hatimaye Naibu Katibu Mkuu akakabidhiwa jukumu la kuoanisha na kuratibu idara zote zilizo chini ya mwavuli wa Umoja wa Mataifa. Jukumu hili lilikuwa na manufaa makubwa, hususan tulipoingia katika utekelezaji wa dhana ya “Huduma ya Pamoja ” (Delivering as One - DaO) ili kuleta ufanisi zaidi katika kazi zetu hususan za maendeleo.


Kwa bahati nzuri, ninamaliza kipindi changu kukiwa na maendeleo mazuri yanayotokana na jitihada za kimataifa za kupambana na umaskini. Takwimu za kuaminika za hivi karibuni zinatuambia kuwa juhudi zetu za kupunguza idadi ya watu maskini duniani kufikia angalau nusu ya viwango vya sasa zimeanza kuzaa matunda. Taarifa hii ni ya kutia moyo licha ya ukweli kwamba dunia inapitia dhahama kubwa ya kiuchumi kuliko wakati mwingine wowote katika miaka ya hivi karibuni. Pamoja na majukumu mengine,nguvu zetu tulizielekeza zaidi kwenye kufanikisha malengo ya maendeleo ya milenia na malengo mengine ya maendeleo yaliyokubaliwa kimataifa. Nilihamasika sana na dhamira waliyoionesha wadau na washirika wetu wa maendeleo: serikali, mashirika ya kiraia na mashirika ya biashara. Kwani wote kwa pamoja waliyatumia malengo hayo kama kilingo cha msingi katika kutokomeza umaskini.


Katika kufanikisha utekelezaji madhubuti wa malengo ya maendeleo ya milenia nilipewa jukumu la kukamilisha ahadi ya Katibu Mkuu aliyoitoa kwa nchi wanachama ya kuunda Mfumo Kamilifu wa Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs Integrated Implementation Framework ). Ninaona fahari kwamba naondoka Umoja wa Mataifa mfumo huu ukiwa umekamilika ambapo Katibu Mkuu aliuzindua mwezi Juni mwaka huu. Kwa mara ya kwanza mfumo huu umeweka utaratibu ambao utauwezesha Umoja wa Mataifa na wadau wote kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa ahadi za kisera na kifedha. Hapana shaka utaratibu huu utaongeza uwajibikaji wa wadau na upimaji sahihi wa hatua za maendeleo.

Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) Barani Afrika


Kwa mwelekeo huo huo, Katibu Mkuu alizindua Jopo la Viongozi la Kuhimiza Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia Barani Afrika (MDG Africa Steering Group) mwezi September 2007. Kikundi hiki kinajumuisha taasisi zote kuu duniani zilizo mstari wa mbele katika kuchochea kasi ya maendeleo ya Afrika. Nilipata bahati ya kukiongoza kikosi-kazi (MDG Africa Working Group) kilichokuwa mhimili wa Jopo hilo la viongozi. Baada ya miaka mitano ya majadiliano ya kina, Jopo hilo likiongozwa na Katibu Mkuu limetoa mapendekezo kamambe ya utekelezaji. Endapo mapendekezo haya yatazingatiwa basi yatakuwa nyenzo muhimu ya kuweka sera na mikakati madhubuti itakayosaidia maendeleo katika nchi husika na duniani kwa ujumla. Napenda kutoa mwito kwa wadau wote kuyapa umuhimu mapendekezo haya.


Ninafahamu kwamba tathmini kamili ya mafanikio ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia imepangwa kufanyika Septemba mwaka 2013. Hata hivyo tayari tunaweza kusema kuwa Malengo haya yameleta mabadiliko chanya katika maisha ya watu wa kawaida sehemu nyingi duniani, hususan barani Afrika. Ni dhahiri kuwa jamii nyingi zimenufaika na utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya milenia sio kwa kufanyiwa hisani bali kwa wao wenyewe kuwa na mikakati maalum ya kupiga hatua madhubuti za kujiletea maendeleo stahimilivu na yaliyolenga kuleta usawa baina ya watu.




Mkutano wa Rio + 20


Ni jambo la kutia moyo kwamba maendeleo shirikishi na yenye kuleta usawa ni baadhi ya masuala muhimu yaliyojadiliwa katika mkutano wa Rio +20 uliomalizika hivi karibuni. Suala hili litachukua nafasi kubwa pia katika kuandaa mfumo wa maendeleo unaotarajiwa baada ya mwaka 2015, mwaka uliokusudiwa kufikia malengo ya maendeleo ya milenia. Nilipokabidhiwa jukumu la kuratibu maandilizi ya ushiriki wetu kwenye mkutano wa Rio+20 nilitiwa moyo na nia ya dhati ya mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kubuni mkakati wa pamoja wa kutekeleza maazimio ya Rio+20. Napenda kuzishukuru nchi wanachama kwa kufikia makubaliano katika masuala mengi yaliyojadiliwa Rio licha ya changamoto nyingi zinazotokana na mtikisiko wa uchumi duniani. Ninafurahi kwamba maazimio ya mkutano huu yatachangia upatikanaji wa maendeleo stahimilivu, shirikishi na yenye kuleta usawa na hususan kuhakikisha kunakuwa na mustakabali mzuri kwa wanawake na wasichana.

Uwezeshaji wa wanawake na usawa wa kijinsia


Tukirejea kwenye suala hili, hata baada ya Mkutano wa Rio + 20 tutawajibika kuendelea na juhudi za uwezeshaji wa wanawake na kuleta usawa wa kijinsia. Wakati wa utumishi wangu Umoja wa Mataifa tumefanya bidii kubwa na kutumia muda mwingi kushughulikia suala hii. Tumetumia hadhi na ushawishi wa ofisi yetu kupaza sauti za wanawake na wasichana na kukuza ushiriki wao katika jamii. Tumeendesha kampeni za kupiga vita ukatili kwa wanawake na wasichana. Tumezihimiza mamlaka katika ngazi za kitaifa na kimataifa kutunga sera na sheria zinazozingatia haki za wanawake na usawa wa kijinsia, na tumetaka wapewe fursa kushika nafasi za uongozi katika jamii. Ndiyo maana kwa upande wetu hatukuweka koleo chini hadi pale tulipokamilisha uanzishwaji wa idara inayojulikana kwa kifupi kama “UN Women” mnamo Julai 2010. Hii ni idara ya Umoja wa Mataifa iliyoundwa kwa madhumuni ya kuongoza masuala ya wanawake na usawa wa kijinsia kwa umakini na ufanisi zaidi kuliko hapo awali. Tumefanya jitihada hizi kwa kuamini kuwa hakuna uamuzi wowote ule, uwe mdogo au mkubwa, unaofanywa na Umoja wa Mataifa bila ya kuzingatia maendeleo na ustawi wa wanawake na wasichana.


Huduma ya Pamoja


Kwa upande mwingine ninapenda kuwapongeza kwa dhati wenzangu wote waliomo katika utumishi wa Umoja wa Mataifa,wake kwa waume,walioutumia ujuzi na weledi wao wote kuchangia maendeleo ya nchi na jamii tunazozihudumia. Natoa shukrani za pekee kwa wale wote waliopo kwenye ofisi na vituo vya Umoja wa Mataifa nje ya Makao Makuu na ambao wanafanya kazi katika mazingira magumu na yenye changamo nyingi. Hao wote wanadhihirisha umuhimu wa kuwapo kwa Shirika hili kama chombo cha kuhimiza maendeleo katika ngazi zote za kitaifa, kikanda na kimataifa. Katika kutekeleza dhana ya “Huduma ya Pamoja” (Delivering as One) Waratibu Wakaazi wa Umoja wa Mataifa wamekuwa na mchango muhimu sana.Uratibu wao umeongeza ubora na wepesi wa utoaji huduma kwa nchi wanamowakilisha Shirika. Hatuna budi kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha dhana ya “Huduma ya Pamoja”. Ni dhahiri kwamba uwezo wa nchi mwanachama kumiliki mchakato wa maendeleo yake unakuwa imara zaidi pale ambapo kuna mtiririko mzuri wa huduma za Umoja wa Mataifa na fursa za kukuza ushirikiano endelevu na wadau wengine wa maendeleo. Wakati uamuzi rasmi kuhusu maendeleo ya dhana hii ukisubiri kukamilika kwa majadiliano ya nchi wanachama, ninaamini kwa dhati kuwa utaratibu wa kutoa “Huduma ya Pamoja” kupitia mpango mmoja uliokubaliwa na wote ni mwelekeo sahihi na wenye tija.

Nchini mwetu Tanzania, mashirika ya Umoja wa Mataifa yamekuwa yakifanya kazi kwa ushirikiano wa karibu sana toka mwaka 2011 kupitia mpango mmoja uitwao “Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kusaidia Maendeleo” (United Nations Development Plan – UNDAP). Mpango huu unakwenda sambamba na mwaka wa fedha wa Serikali yaani Julai 1 hadi Juni 30 na kwa mantiki hiyo kuuwezesha kuzingatia vipaumbele vya Serikali. Kupitia mpango huu Umoja wa Mataifa umejiwekea utaratibu wa kujipima na kujitathmini ambao unatoa fursa kwa hatua za haraka kuchukuliwa inapobidi. Utaratibu huu unapatikana kwenye tovuti. Kwa upande wa uendeshaji, mfumo huu wa utendaji kazi kwa pamoja umetuwezesha kutekeleza majukumu mengi kwa kutumia raslimali chache ambapo“ziada” iliyopatikana imeelekezwa kwenye shughuli nyingine za maendeleo.


Afya ya Jamii


Katika eneo la afya, ambamo wanawake na watoto ndiyo wanaathirika zaidi, hatua muhimu zinachukuliwa kupunguza vifo nakuhakikisha kwamba kila mwanamke na kila mtoto anakingwa na maradhi, hususan kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Tukiwa Nairobi Aprili mwaka 2011, Katibu Mkuu Ban Ki-moon, Michel Sidibe, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI (UNAIDS) pamoja nami tulishuhudia mfano hai wa jitihada za Umoja wa Mataifa. Tulipata fursa ya kukutana na mwanamke aliyeathirika na virusi ambaye alijaaliwa kupata mapacha watatu waliozaliwa bila ya maambukizi. Nikiwa mjumbe wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa iliyoshughulikia taarifa na uwajibikaji katika masuala ya afya ya mama na mtoto (Commission on Information and Accountability on Women's and Children's Health) ambayo iliendeshwa kwa umahiri na Rais Kikwete wa Tanzania na Waziri Mkuu Harper wa Canada, nina imani kwamba jumuiya ya kimataifa hivi sasa imepata mfumo madhubuti utakaohakikisha kwamba kunakuwa na ufuatiliaji, usimamizi na uwajibikaji kuhusu afya ya mama na mtoto. Hakuna shaka kwamba mfumo huu utafikia hatua ya utekelezwaji siku za hivi karibuni.


Hali kadhalika, kazi nzuri imekuwa ikifanywa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Mpango wa Uzazi Duniani (UNFPA), Babatunde Osotimehin, na Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ya kuboresha afya ya mama na mtoto. Matokeo ya jitihada za wenzangu hawa yalikuwa chachu ya utekelezaji wa majukumu ya Naibu Katibu Mkuu katika nyanja zote za maendeleo. Ama kwa hakika matunda ya kazi zao yanaimarisha imani yangu kuwa Umoja wa Mataifa ni Shirika lenye umuhimu mkubwa; na kwamba mchango wetu, japo mdogo, unasaidia sana katika kufikia malengo ya maendeleo ya milenia. Nilijawa na imani kama hiyo nikiwa katika ziara nyingine za kikazi. Kwa mfano nikiwa Montevideo, Uruguay, Novemba 2011, pamoja na wenzangu Michelle Bachelet, Helen Clark na Alicia Barcena, tulisimama kidete kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya kupiga vita vitendo vya ukatili kwa wanawake.


Nilipozuru Haiti mwezi Aprili2010, miezi michache baada ya tetemeko ambalo lilikuwa kubwa kuliko yote yaliyowahi kutokea nchini humo kwa kipindi cha takriban karne moja, nilikutana na watu ambao walikuwa wameathirika vibaya sana: waliopoteza familia nzima, waliopata ulemavu wa maisha, waliopoteza mali zao zote! Lakini bado watu hawa walikuwa na nyuso za matumaini wakitarajia mchango wa Umoja wa Mataifa na wa wadau wengine wa jumuiya ya kimataifa. Mnamo Novemba 2010 tulizuru Laos, ambako Umoja wa Mataifa unashirikiana kwa karibu na Serikali na wadau wengine wengi katika utoaji wa misaada muhimu ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuisaidia Laos kupambana na janga la mabaki ya mabomu ya“cluster munitions”.


Hii ni mifano michache tu inayojibu hoja za wakosoaji wa Umoja wa Mataifa.Ujumbe wangu kwao ni huu: wanyonge na wenye kutaabika sehemu zote duniani ni mashuhuda na watetezi wakubwa wa Umoja wa Mataifa. Kwa wanyonge na wahitaji walio wengi Shirika hili ni nguzo ya kutumainiwa katika jitihada zao za kila siku za kujiletea maisha yenye utu na heshima.

Mageuzi katika menejimenti na usimamizi wa mabadiliko


Ukweli huu haumaanishi kuwa Umoja wa Mataifa hauna kasoro au upungufu. La hasha! Ndiyo maana wakati wa utumishi wangu tulijielekeza kikamilifu kwenye kuboresha masuala ya utawala, uendeshaji na namna tunavyofanya kazi. Ni wazi kwamba hivi sasa Umoja wa Mataifa umebadilika kutoka chombo cha huduma za mikutano na kuwa mtendaji mwenye majukumu muhimu nje ya kumbi za mikutano. Kwa ushirikiano na msaada maridhawa wa wafanyakazi wenzangu, tulijikita katika kuhamasisha mabadiliko ya kiutendaji katika Umoja wa Mataifa, ikiwa ni pamoja na kujenga desturi ya uwajibikaji, uadilifu na kufanya kazi kwa tija zaidi huku tukitumia rasilmali chache.


Ilitubidi pia kuweka mifumo thabiti ya kusimamia mabadiliko yaliyokuwa yakijitokeza. Katika kufanya hivyo tulitambua wazi kwamba hakukuwa na njia ya mkato wala njia mbadala ya kuliimarisha Shirika letu na kulifanya liwe la kisasa zaidi katika kutekeleza majukumu yake.Tulihakikisha kwamba utendaji kazi wetu unakwenda sambamba na changamoto zilizopo, lakini pia tulizingatia ufinyu wa bajeti, misimamo tofauti na wakati mwingine inayaokinzana ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa. Katika hali hii ilitulazimu kuwa wabunifu zaidi ili kuleta muafaka baina ya nchi wanachama na kuhakikisha kwamba raslimali chache zilizopo zinatoa tija kubwa zaidi.


Wafanyakazi ndiyo rasilmali kubwa kupita zote. Hivyo kila tulipoendelea na jitihada za kuboresha Shirika ilitubidi kuwekeza vilivyo kwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa kwa kuwapatia fursa za mafunzo na msingi imara wa maendeleo yao kazini. Ni jambo lililo dhahiri kuwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wanatekeleza majukumu yao katika mazingira hatarishi na yenye kubadilika mara kwa mara. Tunafahamu, tena kwa uchungu mkubwa, kuwa Bendera ya Umoja wa Mataifa - “bendera ya bluu” - hivi sasa si kinga tena. Haituhakikishii usalama kwani wengi wa watumishi wetu mahiri wamekuwa wahanga wa matukio ya kikatili ya ugaidi. Nilishuhudia tukio la aina hii huko Abuja, Nigeria, ambako watumishi wenzetu walipoteza maisha kutokana na shambulio la kigaidi la tarehe 26 Agosti 2011. Na mara nyingi wenzetu wanapotangulia mbele ya haki, wapendwa wao wanaachwa katika hali ngumu ya maisha. Ni faraja kubwa kwangu kuwa miongoni mwa masuala ambayo tuliyasimamia kabla ya kumaliza utumishi wangu ni kuanzisha mchakato wa kubaini namna bora ya kuwasaidia wahanga wa majanga hayo pamoja na familia zao.



Utawala wa sheria


Mojawapo ya majukumu ya Umoja wa Mataifa ni kukuza sera zinazolenga kulinda haki za binadamu na kuendeleza utawala wa sheria katika ngazi za kitaifa na kimataifa. Leo hii, nchi nyingi zimelipa kipaumbele suala la kuimarisha utawala wa sheria, hususan kufuatia umuhimu wake katika ajenda za ujenzi wa amani (peace-building) na maendeleo stahimilivu. Kwa mantiki hiyo, nilifurahi nilipopata fursa ya kusimamia ujenzi wa mfumo madhubuti wa sera na mwongozo wa utekelezaji wa shughuli za utawala wa sheria nikishirikiana na nchi wanachama. Kwa upande wao nchi wanachama zimepanga kufanya mkutano wa ngazi ya juu wakati wa kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwezi Septemba 2012. Nia kubwa ni kuendeleza jitihada katika suala hili ili kukuza heshima ya watu wote duniani na kujenga amani kati ya mataifa.
Hitimisho


Japokuwa muda wangu wa utumishi katika Umoja wa Mataifa umefikia tamati, naamini hakuna tamati katika utekelezaji wa malengo, misingi na maadili ya Umoja wa Mataifa. Ili mradi bado kuna umaskini duniani na mahitaji ya chakula; bado kuna changamoto ya kutunza utu na heshima ya binadamu na haja ya kuimarisha amani duniani basi hakika nitaendelea kuunga mkono jitihada, misingi na malengo ya Umoja wa Mataifa popote pale nitakapokuwa. Kwani ni dhahiri kwamba njia bora ya kukabiliana na changamoto kubwa zilizo mbele yetu ni kujenga ubia na ushirikiano wa karibu baina ya serikali, asasi za kiraia, wafanyabiashara, mashirika ya hisani, taasisi za kitaaluma na watu binafsi.


Aidha, ninaaamini kuwa vijana, kizazi ambacho kina kila sababu ya kuwa na kiu ya kuishi kwenye dunia yenye utu, usawa, haki na amani, watauchukulia Umoja wa Mataifa kuwa mbia wa kuaminika katika kujenga mustakabali wao.



Asha-Rose Migiro

Friday, July 13, 2012

SIKU YA UGAWAJ WA BAISKELI ZA RAIS KIKWETE


Wakina Mama watatu wa Mkoa wa Iringa


 Mkuu wa Wilaya ya Mufindi (kushoto) na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa (kulia)


 Baadhi ya Baiskeli walizokabidhiwa Waganikazi wa Mkoa wa Iringa 



Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi Gertrude Mpaka akishikana mkono na Mganikazi baada ya kukabidhiwa Baiskeli yake 

Thursday, July 12, 2012



WAGANI KAZI KUWEZESHWA IRINGA


Serikali Mkoani Iringa ameahidi kuendeleza ushirikiano uliopo na wapani kazi ili kuwawezesha kutekeleza wajibu wao wa kukuza kilimo katika maeneo waliyopo na kupunguza umasikini.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Christine Ishengoma wakati akigawa baisketi 373 zenye thamani ya shilingi milioni 54 kwa wagani kazi walioshiriki mafunzo ya ugani kazi mwaka 2009, tukio lililofayika katika uwanja wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa leo.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Dr. Christine Ishengoma 
akikabidhi baiskeli kwa Mganikazi

Dkt. Christine amesema kuwa Serikali ya Mkoa inatambua umuhimu wa Wagani kazi katika kukuza sekta ya Kilimo Mkoani Iringa na kuwakumbusha kuwa Wagani kazi ndiyo mabwana na mabibi shamba katika maeneo yao. Amesema kuwa kutokana na umuhimu huo kwa wakulima, Serikali itaendelea kuwasaidia Wagami kazi hao kwa kuwapatia mafunzo ya mara kwa amra na mbinu bora za kilimo cha kisasa pamoja na kuwapatia nyenzo za kufanyia kazi ili kuleta mapinduzi katika Kilimo Kwanza.

Amesema lengo la kuwakabidhi baiskeli hizo kuwawezesha Wagani kazi hao kuwafikia wakulima wengi kwa urahisi na haraka zaidi. Amesema “nawakabidhi baiskeli hizi ili mkafanye kazi iliyokusudiwa”. Amesema kuwa nilazima wakafanye kazi kwa nguvu zaidi kwa sababu watapimwa kutokana na kazi walizozifanya.

Akiongelea pembejeo za kilimo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema kuwa utaratibu utaendelea uleule isipokuwa sasa mawakala watatoka juu ambao watasambaza pembejeo hizo wenyewe kwa wakulima na kuwataka wakuu wa Wilaya kusimamia vizuri zoezi hilo ili pembejeo ziweze kuwafikia walengwa.

Katika Taarifa fupi ya utendaji kazi wa Wagani kazi Mkoani Iringa iliyowasilishwa na Shenal Nyoni, Afisa Kilimo Mkuu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, imesema kuwa mwanzoni wa mwaka 2000 Mkoa w Iringa ulikuwa unakabiliwa na tatizo la uhaba wa wataalam wa kilimo na mifugo katika ngazi ya Kijiji na Kata baada ya Serikali kusimama katika kuajiri wataalamu katika Sekta ya Kilimo pamoja na Sekta nyingine.

Amesema kutokana na hilo Mkoa wa Iringa ulibuni utaratibu wa kuwa na Wagani kazi ambao watasaidia kutoa huduma za ugani kwa kushirikiana na wataalam wa kilimo na mifugo vijijini.

Nyoni amesema kuwa mafunzo kwa Wagani kazi yalifanyika katika kila Halmashauri kwa muda wa wiki mbili na Wagani kazi 406 walipatiwa mafunzo kwa lengo la kufundisha Wagani kazi 50 katika kila Halmashauri. Amesema kuwa Wagani kazi hao walifundishwa juu ya kanuni za kilimo na ufugaji bora na fursa ya kujifunza kwa vitendo.

Akionglea mgawanyo wa baiskeli hizo katika mabano, Afisa Kilimo huyo amesema kuwa Manispaa ya Iringa (22), Wilaya ya Iringa (58), Wilaya ya Kilolo (50), Wilaya ya Mufindi (50), Wilaya ya Njombe (50), Njombe Mji (44), Wilaya ya Ludea (49), Wilaya ya Makete (50)  


Ikumbukwe kuwa baiskeli hizo ni ahadi aliyoitoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipofungua mafunzo ya wiki mbili kwa ajili ya Wagani kazi katika Mkoa wa Iringa mwaka 2009. 



Viongozo wa Mkoa wa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na Waganikazi muda mfupi baada ya kukabidhiwa baiskeli zao





=30=