Monday, July 30, 2012

KKKT IRINGA WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA SENSA




Washarika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, usharika wa Iringa Mjini wametakiwa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa mabadiliko ya uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kufanikisha uundwaji wa Katiba hiyo kwa kujumuisha mapendekezo ya watu wengi zaidi.

Wito huo umetolewa na mgeni rasmi Dkt. Christine Ishengoma katika harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa kanisa kuu la mtaa wa Wilolesi iliyofantik Katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzanaia, Usharika wa Iringa Mjini leo.

Dkt. Christine ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, amesema “ndugu zangu Washarika natoa rai kwenu kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha na kuwaeleza waumini wengine na wananchi kwa ujumla ili washiriki katika mchakato huu kwa kutoa elimu na hamasa”. Amesema “napenda kutoa wito kwenu wote kuwa huru kutoa maoni yenu Tume itakapopita katika maeneo na kukusanya maoni yenu”. 

Amesema kuwa baadhi ya wananchi wanalalamika kuwa Katiba ya sasa inamapungufu kadhaa, hivyo huu ndio wakati wao wa kutoa maoni yao ili hayo mapungufu yaweze kufanyiwa kazi na kuingia katika Katiba mpya. Amesema hili litafanikiwa pale tu, washarika na wananchi watakapojitokeza kwa wingi kutoa maoni yao pindi tume ya kukusanya maoni itakapopita katika maeneo yao. Amewataka kuwa makini katika kusikiliza tarehe na sehemu ambazo mikutano hiyo itakuwa ikifanyika ili waweze kuwasilisha maoni yao kwa tume hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa amewataka wananchi kuwa huru katika kutoa maoni yao na kuwahakikishia kuwa ukusanyaji wa maoni hayo hauhusiani na itikadi yoyote. Amesema ili Katiba hiyo mpya iwe ya mafanikio ni lazima maoni ya wananchi wengi yaweze kukusanywa na mafanikio hayo yanatokana tu, na wananchi kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao kwa tume hiyo.  
=30=

No comments:

Post a Comment