Monday, December 21, 2015

RC IRINGA AWATAKIA HERI MAJERUHI WA AJALI YA BASI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza amewatakia heri na kupona haraka majeruhi wote wa ajali ya basi ili waweze kuungana na familia zao na kuendelea na majukumu yao.

Kauli hiyo aliitoa muda mfupi baada ya kufanya ziara ya kustukiza katika hospitali ya rufaa ya Iringa kujionea jinsi majeruhi wa ajali ya basi la kampuni ya New Force wanavyohudumiwa hospitalini hapo.

Masenza akiyeambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Iringa alisema kuwa ajali hiyo imemuhuzunisha yeye binafsi na mkoa kwa ujumla. Alisema kuwa anawaombea kwa Mungu majeruhi wote kupata nafuu na kupona kabisa ili waweze kuendelea na majukumu yao ya ujenzi wa Taifa.

Akiongelea hali ya huduma hospitali hapo, Masenza alisema kuwa ameridhishwa na jinsi majeruhi wa ajali hiyo walivyopokelewa na kutibiwa hospitalini hapo. Aidha, aliwataka madaktari na wauguzi kuendelea kuonesha moyo wa huruma na uwajibikaji wanapowahudumia majeruhi wa ajali hiyo. Aidha, aliwahakikishia majeruhi hao kuwa serikali ipo pamoja nao kuhakikisha wanapata huduma bora ili wapone haraka na kuendelea na majukumu yao.

Ajali hiyo ilitokea kwa basi kugongana na lori ilitokea tarehe 18 Disemba, 2015 mchana baada ya tairi la lori lori namba T 616 DES la kampuni ya Ranfad Ltd kupasuka kupasuka na lori kukosa muelekeo na kuligonga basi la kampuni ya New Force namba T 483 CTF na kusababisha vifo vya abiria 12 na majeruhi 28. Miongoni mwa majeruhi hao, watatu ni raia wa Kongo DRC na mmoja raia wa Afrika Kusini.

=30=