Thursday, November 7, 2013

COASTAL YALALA 1-0 KWA JKT RUVU





MZUNGUKO wa kwanza wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara umekamilika leo baada ya Coastal Union kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya maafande wa JKT Ruvu, kwenye uwanja wa Chamazi jijini Dar es Salaam.

Kipindi cha kwanza kilianza kwa Wagosi kusuasua na kuwapa nafasi Ruvu kuutawala mchezo ambapo ndani ya dakika ya kwanz awalikosa bao na kupata kona.
Hali iliendelea hivyo kwa wachezaji wa Wagosi kupoteza mwelekeo ambapo katika dakika ya tisa Ruvu walikosa bao la wazi baada ya beki  Wagosi Juma Nyoso alichelewa kufika baada ya Ruvu kupiga krosi na mchezaji wao kuingia nao lakini golikipa wa Wagosi Shaaban Kado alikuwa makini langoni.
Ilipofika dakika ya 34 Ruvu waligongeana pasi ndani ya box la Wagosi, ambapo kutokana na walinzi kukosa umakini Bakari Kondo wa Ruvu aliipatia bao la kuongoza timu yake.
baada ya hali kuwa hivyo kocha Joseph Lazaro wa Wagosi alifanya mabadiliko na kuwatoa Hamad aliyeumia na kumuingiza Marcus Ndeheli. Halafu akamtoa Othman Tamim na kumuingiza Abdi Banda.
Aidha timu zilienda mapumziko Ruvu JKT wakiwa mbele kwa bao moja.
Kipindi cha pili, mchezo ulianza kwa Coastal Union  kutawala uwanja, na kuonyesha nguvu ya kutaka kukomboa bao lililopatikana kipindi cha kwanza.
Baadaye alitolewa Suleiman Kassim ‘Selembe’ na kuingia Daniel Lyanga. Lakini hakuna kilichobadilika mpaka daika tisini.
Mwamuzi wa leo Hasheem Abdallah kutoka Dar es Salaam, alimaliza mchezo akiwa anazomewa na mashabiki wachache wa Coastal Union waliojitokeza leo wakimshutumu kuchezesha hovyo.
Kwa hali hiyo Coastal Union itaendelea kushikilia nafasi ya saba ikiwa na point 16.

@Habari na picha kwa hisani ya mtandao wa Coastal Union