Friday, November 25, 2011

RC MWAMBUNGU AKEMEA KASI NDOGO YA WAKANADARASI WA BARABARA

Na. Revocatus A. Kassimba, RS SONGEA
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu amekemea kitendo cha mkandarasi wa ujenzi wa barabara kutoka Namtumbo kwenda  Tunduru unaofanywa na kampuni ya M/S Progressive Higleig JV  kutoka India kuwa na kasi inayotia shaka
Amesema hayo wakati akifungua Kikao cha bodi ya barabara mkoa wa Ruvuma kilichofanyika leo katika ukumbi wa Songea Club mjini Songea
Alisema mradi wa ujenzi wa barabara ya Namtumbo hadi Tunduru ni sehemu ya mpango wa serikali kuhakikisha kuwa ukanda wa Maendeleo ya Mtwara unaunganishwa kwa lami kutoka bandari ya Mtwara hadi bandari ya Mbambabay
Aliongeza kuwa mradi huo unahusisha ujenzi wa barabara kwa iwango cha lami yenye urefu wa kilometa 193 ambapo kazi ya ujenzi ilipaswa kuanza Machi mwaka huu na utakamilika Mei 2013 lakini hadi sasa hata vifaa muhimu kwa kazi hiyo havijaletwa.
“Hadi mimi nakwenda kutembelea mradi husika hivi karibuni ndio mkandarasi anaanza kutoka usingizini kwa kuanza kusafisha msitu   hii haikubaliki hata kidogo kwani watu hawa kuachiwa kufanya uzembe huu” alisema Mkuu wa mkoa
Mwambungu alisisitiza ya kwamba hafurahishwi hata kidogo na kazi ya mkandarasi Progressive kwani kuna uwezekano mkubwa wa kazi kutokamilika kwa wakati yaani miezi 27 hivyo akaeleza kuwa anawasiliana na wizara ya ujenzi kuona hatua za kuchukua dhidi mkandarasi
Akielezea mafanikio ya serikali katika Kuboresha Miundombinu Mwambungu alisema kuwa lengo la serikali ni kuunganisha maeneo yote kwa barabara yenye kiwango cha lami
 Alisema kwa mkoa wa Ruvuma kazi ilianza mwaka jana kwa miradi ya ujenzi wa barabara kutoka Mbinga –Peramiho (km 78) unaendelea,Songea –Namtumbo (km 67) kazi inaendelea na Namtumbo-Tunduru (km 193) kazi imeanza hivi karibuni
Aidha kwa upande wake Meneja wa TANROADS mkoa wa Ruvuma Mhandisi  Ibrahim Kisimbo alikiambia Kikao kuwa mradi huo wa Namtumbo  hadi Tunduru unakadiliwa  kugharimu shilingi bilioni 180 ambazo ni ufadhili wa  Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDP),shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na serikali ya Tanzania
Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa amekemea tabia ya Halmashauri za wilaya na Manispaa mkoani kutekeleza miradi ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha chini kwa kigezo cha fedha kidogo kuwa halikubaliki
“Fanyeni kazi zenu kwa kuhakikisha ubora wa miradi unaendana na thamani ya fedha iliyotolewa “ na kuongeza kuwa wakumbuke kuwa wakaguzi wakuu wa kazi za ujenzi wa barabara ni wananchi hivyo tusiwaangushe kwa kusimamia miradi yenye ubora hafifu alisema Mkuu wa mkoa
Mkoa wa Ruvuma una mtandao wa barabara kiasi cha kilometa 5,485.59 ambapo kilometa 219.93 ni za lami na zilizobaki ni za changalawe na udongo

Wednesday, November 23, 2011

RC AKEMEA UKATAJI MITI OVYO

Mkuu wa Mkoa wa Iringa ameagiza kuacha tabia ya kukata miti ovyo ili kuunusuru Mkoa na kugeuka jangwa kama baadhi ya maeneo ambayo yanakubwa na ukame wa mara kwa mara na kusababisha upungufu wa chakula.
Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma wakati akiongea na wananchi wa Kata ya Idodi iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa alipofanya ziara ya kuhamasisha shughuli za kilimo na elimu.
Dk. Ishengoma amesema kuwa katika kipindi cha kuandaa mashamba wananchi wamekuwa na tabia ya kukata miti katika mashamba yao. Amesema “msikate miti yote sababu miti hii ndiyo inayotengeneza mvua hivyo, tukiendelea kukata miti hiyo ukame hautaisha bali utazidi kuongezeka katika eneo kubwa zaidi”.
Kutokana na ukame wa mara kwa mara unaosababisha upungufu wa chakula, Serikali imeweka mikakati ya kukabiliana na upungufu wa chakula ikiwa ni pamoja na kuanzisha kilimo cha mtama amesema Dk. Ishengoma.
Amesema ni vizuri wananchi wakabadili mawazo ya kutegemea mazao ya mahindi na mpunga pekee na kufikiria kilimo cha zao la mtama.
Akiongelea vocha za pembejeo za kilimo, amesema kuwa wananchi waliopata vocha hizo wazitumie vizuri ili kuweza kunufaika nazo na kufikiwa kwa malengo ya serikali ya kuwainua wananchi kiuchumi kupitia kilimo. Amesema wananchi wanawajibu wa kufahamu kuwa seti moja ya vocha za pembejeo inahusisha mbolea ya kupandia, mbegu bora na mbolea ya kukuzia.
Aidha, alitahadharisha kwa mawakala wasiowaaminifu kuwa lazima wafuate utaratibu uliowekwa katika usambazaji na matumizi ya vocha hizo na hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wakala yeyote atakayekiuka utaratibu uliowekwa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa anafanya ziara ya kuhamasisha kilimo na elimu baada ya msimu wa kilimo kuanza wakati baadhi ya sehemu katika Tarafa ya Idodi ni miongoni mwa maeneo yaliyokubwa na ukame na kusababisha upungufu mkubwa wa chakula. 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa anafanya ziara ya kuhamasisha kilimo na elimu baada ya msimu wa kilimo kuanza wakati baadhi ya sehemu katika Tarafa ya Idodi ni miongoni mwa maeneo yaliyokubwa na ukame na kusababisha upungufu mkubwa wa chakula. 

RC AHIMIZA MAZAO YANAYOSTAHIMILI UKAME


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma amewataka wananchi wa Tarafa ya Idodi kufikiria kilimo cha mazao yanayostahimili ukame ili kukabiliana na tatizo la njaa linalowakabili wananchi wa Tarafa hiyo mara kwa mara.
Dk. Christine anayefanya ziara maalumu ya kuhamasisha shughuli za kilimo na elimu katika Mkoa wa Iringa, siku yake ya kwanza ya ziara aliyoifanya katika Kata ya Nzihi, Tungamalenga na Mahuninga amesisitiza kilimo cha zao la mtama pamoja na mazao mengine. Amesema “si lazima kulima mahindi na mpunga tu kama zao la chakula, bali tubadilishe kidogo fikra ili tuweze kulima mazao yanayostahimili ukame na tuanze na zao la mtama”.
Amesema pamoja na jitihada za Serikali ya Mkoa kuhimiza kilimo cha zao la mtama lakini mkulima mmoja mmoja ni vizuri akalima pia muhogo na viazi vitamu kwa kujihakikishia uhakika na hifadhi ya chakula.
Amesema kuwa matarajio ni kila kaya kulima angalau ekari mbili za mtama. Amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, itazigawa hizo mbegu bure kwa wakulima na kuwakumbusha wakulima kuwa wamebakiwa na kazi moja tu ya kulima baada ya kuondolewa gharama za kununua mbegu ya mtama. Vilevile, amesisitiza kuwa serikali itakuwa makini katika kuzigawa mbegu hizo kwa kuangalia eneo lililolimwa ili kuepukana na baadhi ya wakulima kuzitumia kwa matumizi mengine tofauti na makusudio yaliyokusudiwa na serikali.
Aidha, amewataka wananchi kujihusisha na ufugaji wa wanyama wadogo wadogo kama kuku, bata na mbuzi ili uweze kuwasidia katika kukidhi mahitaji ya kawaida ya nyumbani. Amesema “ufugaji wa wanyama wadogowadogo unasaidia sana hasa akina mama kuweza kukidhi mahitaji ya familia”.
Akiongelea ufugaji wa ng’ombe ameshauri kuwa yatumike madume bora ili kupata maziwa mengi. Vilevile ameshauri kutumia njia ya uhamilishaji ili kupunguza gharama za ufugaji wa madume mengi ya ng’ombe na uhifadhi wa mazingira.
Kuhusu elimu, Mkuu wa Mkoa ameagiza watoto wote watakaofaulu wapelekwe shule ili kukuza kuwango cha elimu katika Mkoa. Amesema “kila mmoja lazima aone fahari kumpeleka mwanae shule na hasa watoto wa kike ili kuachana na tamaduni za kale zilizokuwa zikimfanya mtoto wa kike kukosa elimu”.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa anafanya ziara ya kuhamasisha kilimo na elimu baada ya msimu wa kilimo kuanza wakati baadhi ya sehemu katika Tarafa ya Idodi ni miongoni mwa maeneo yaliyokubwa na ukame na kusababisha upungufu mkubwa wa chakula. 
=30=

Thursday, November 17, 2011

MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU

 Vijana wa JKT Mafinga wakiwa katika shughuli zakijamii


 Wanafahamika kama wazee wa White hakuna kuchafuka


 Wanafahamika kama wazee wa White hakuna kuchafuka




 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi y Mkuu wa Mkoa wa Iringa

















 Viongozi waandamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa akifuatilia kwa makini yanayojiri katika uwanja wa Samora siku ya pili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru

 watumishi wakisikiliza Hotuba ya Katibu Tawala Mkoa wa Iringa katika Uwanja wa Samora siku ya pili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru kwa Mkoa wa Iringa


 watumishi wakisikiliza Hotuba ya Katibu Tawala Mkoa wa Iringa katika Uwanja wa Samora siku ya pili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru kwa Mkoa wa Iringa


 watumishi wakisikiliza Hotuba ya Katibu Tawala Mkoa wa Iringa katika Uwanja wa Samora siku ya pili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru kwa Mkoa wa Iringa



 Kundi la sanaa lijulikanalo kama Makhrikhri kutoka Makete

 Kundi la sanaa lijulikanalo kama Makhrikhri kutoka Makete

 
Katibu Tawala Msaidizi, Sehemu ya Utawala, Bw. Barnabas Ndunguru akipata maelezo kutoka banda la maonesho la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa 

 Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka akikagua madanda ya maonesho


 Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka akisaini kitabu cha wageni katika kanda la CCM 

 Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka akipata kipimo katika banda la Hospitali ya Mkoa katika siku ya pili ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru

 Viongozi ngazi ya Mkoa wakijiandaa kuupokea Mwenge wa Uhuru wilayani Wanging'ombe

 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dk. Christine Ishengoma akikumbatiana na Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa Bi. Mtumwa Khalfan

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Abbas Kandoro akijiandaa kumkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Iringa 


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma akipokea Mwenge wa Uhuru

Wednesday, November 16, 2011



 

Afisa Utumishi, Gasto Andongwisye (kushoto) na Afisa Ushirika, Shabaan Lubatilla (kulia) walitoa maelekezo katika banda la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa



Baadhi ya maafisa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakiweka mambo yao sawa katika banda la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa


 Baadhi ya maafisa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakiweka mambo yao sawa katika banda la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

 
 Watumishi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika banda la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

 Mkuiu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma akiwasili katika uwanja wa Samora



 Maandamano yakiingia uwanja wa Samora





























Saturday, November 5, 2011

...CLUB RAS IRINGA YAAGWA

Mwenyekiti wa Kamati ya michezo ya Mkoa wa Iringa ameitaka timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa (Club ya RAS Iringa) kuhakikisha inafanya vizuri katika michuano ya shirikisko la michezo na wizara, mikoa, idara na wakala wa serikali kuu (SHIMIWI) na kurudi na kombe la ubingwa.

Mwenyekiti wa kamati ya michezo mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka (kushoto) akimkabidhi viatu vya michezo Mwenyekiti wa Club ya RAS Iringa Dr. Oscar Gabone tayari kwenda Tanga kushiriki mashindano ya SHIMIWI

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo wa Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka leo wakati akiiaga timu hiyo maarufu kama Ras Iringa inayojiwinda na michuano ya SHIMIWI inayotarajiwa kuanza kurindima jijini Tanga leo tarehe 5.11. 2011.

Mpaka amesema kuwa michezo ni furaha, upendo na afya hivyo ni jukumu lenu wanamichezo kuhakikisha michezo inatumika katika kudumisha furaha, upendo na afya.

Amesema hayo yakizingatiwa ni dhahiri kuwa timu hiyo itafanya vizuri na pamoja na kurudu na kombe la ushindi pia ameigaziza kurudi na ushindi wa nidhamu.
Akiongea kwa kujiamini, Mpaka ambaye pia ni Katibu Tawala Mkoa wa Iringa na aliyeanzia kazi katika Mkoa wa Tanga kwa nafasi hiyo aliyonayo kwa sasa amesema ninajivunia timu ya wanamichezo iliyojiandaa kiushindani na yenye wachezaji walioshiba vilivyo.

Amesema “SHIMIWI tunaenda kushindana pia kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo” na kuwataka wanamichezo kushindana huku wakitafakari mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika miaka hiyo 50.

Awali akimkaribisha Mwenyekiti wa Michezo Mkoa wa Iringa, Mwenyekiti wa SHIMIWI Club ya RAS Iringa, Dk. Oscar Gabone amesema kuwa wanamichezo hao wameiva na kutokana na ari waliyonayo wanaona kama wanachelewa kuanza michuano hiyo ikiwa ni pamoja na kukabidhiwa ushindi wake.

Akitoa shukrani kwa niaba ya timu hiyo, Afisa Michezo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kenneth Komba, amemshukuru Katibu Tawala Mkoa wa Iringa kwa utayari wake kuwasaidia wanamichezo na michezo kwa ujumla katika Mkoa wa Iringa. Paamoja na kuahidi kurudi na kombe pia alimhakikishia kuendelea kuwa wamoja.

Michezo hiyo inatarajiwa kufunguliwa na Waziri ,wenye dhamana ya michezo nchini, Dk. Emmanuel Nchimbi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ametoa salamu za Iddi El Hajji kwa watoto wa makao ya watoto ya Tosamaganga akiwatakia heri katika sherehe hiyo.

Salaam hizo zimetolewa na katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka kwa niaba ya Rais, Dk. Kikwete katika kituo cha makao ya kulelea watoto ya Tosamaganga.
 Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka (kulia) akikabidhi zawadi ya mbuzi kutoka kwa Rais Kikwete kwa kituo cha makao ya watoto cha Tosamaganga




 Baadhi ya watoto wqanaolelewa katika kituo cha makao ya watoto Tosamaganga


Gertrude amesema “nimekuja hapa kufanya mambo makubwa mawili: jambo la kwanza nimekuja kuwafikishia salamu za Iddi El Hajji kutoka kwa Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anawatakia heri na fanaka kwa iddi El Hajji”.

Gertrude amesema Mhe. Rais amefarijika sana kushiriki na watoto hao katika kusherehekea sikukuu hiyo ya Iddi El Hajji “alipenda kuwa nanyi hapa, lakini kutokana na majukumu kuwa mengi ametuma salamu za kuwatakia heri na fanaka kwa Iddi El Hajji”. Vilevile, amesema kuwa Mhe. Rais anawatakia watoto wote kusherehekea sikukuu ya Iddi El hajji kwa furaha, amani na kudumisha upendo.

Katibu Tawala Mkoa amelitaja jambo la pili kuwa ni zawadi alizotoa mhe. Rais. “ili muweze kusherehekea vizuri sikukuu hii, Mhe. Rais ametoa zawadi kwenu akiamini mtasherehekea pamoja nae kwa furaha”.

Zawadi alizotoa Rais Kikwete ni mchele kilo 150, mbuzi watatu na mafuta ya chakula lita 40 vyote vikiwa na thamani ya shilingi 555,000.

Akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Tinna Sekambo amesema Halmashauri yake inavituo vine vinavyotoa huduma ya kulea watoto na kusema kuwa kituo hiki cha Makao ya watoto Tosamaganga ndicho kikubwa na kuushukuru uongozi wa kitaifa kwa kuutambua mchango wa kituo hicho na kuweza kuungana nao katika malezi ya watoto.

Akitoa shukrani zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, msimamizi wa kituo hicho Sr Hellen Kihwele amesema “namshukuru sana Rais. Kikwete kwa kutukumbuka mara kwa mara hali inayoonesha upendo wake kwetu sote”.

Sr. Hellen ameyataja matarajio ya baadae ya kituo hicho kuwa ni kukamilisha jingo la shule ya chekechea ambalo halijamalizika kutokana na ukosefu wa fedha na kuiomba jamii iweze kusaidia kukamilisha ujenzi huo.

Thursday, November 3, 2011

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA WAZIRI MKUU 

TAWALA ZA MIKOA ZA SERIKALI ZA MITAA






OFISI YA MKUU WA MKOA WA IRINGA



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU KIMKOA NA MAPOKEZI YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU TAREHE 7-11/11/2011


IMETOLEWA NA;    
MHE. DR. CHRISTINE G. ISHENGOMA (Mb.)
          MKUU WA MKOA WA IRINGA



Sanduku la Posta: 858, IRINGA
Simu: 255 026 2702715/2702021/2702191
Fax:   255 026 2702082
Barua pepe: rasiringa@pmoralg.go.tz


Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa:
Tarehe 7 hadi 9 Novemba, 2011 tutakuwa na maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru kimkoa ambayo yatafanyika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Hayati Samora uliopo katika Manispaa ya Iringa. Maadhimisho haya ni maalum kwa ajili ya kufanya tathmini ya shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kijamii tulizofanya kimkoa kwa kipindi cha miaka 50.

Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa:
Wakati wa maadhimisho haya ambapo kutakuwa na maonesho mbalimbali ya shughuli za maendeleo tunazofanya hapa Mkoani, burudani ya ngoma, sanaa, michezo na hotuba mbalimbali za viongozi katika ngazi za Vijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa tunapaswa kufanya tathmini kuona wapi tumetoka, wapi tulipo na wapi tunakwenda. Hii itatusaidia kujiwekea malengo mapya ambayo yataongeza kasi ya maendeleo katika Mkoa wetu kama kauli mbiu ya Maadhimisho haya inavyosema “TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE”.

Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa;
Maadhimisho haya ya miaka 50 ya UHURU yanakwenda sambamba na mapokezi ya Mwenge wa Uhuru ambao utapokelewa hapa Mkoani Iringa tarehe 09 Novemba, 2011 katika Tarafa ya Wanging’ombe iliyopo katika Wilaya ya Njombe (Mwenge utapokelewa toka Mkoa wa Mbeya) na tutaukabidhi Mkoa wa Ruvuma tarehe 11 Novemba, 2011.

Ukiwa hapa Mkoani, Mwenge wa Uhuru utafungua miradi minne  (4), kuweka mawe ya msingi miradi minne (4) kuzinduliwa mradi mmoja (1) jumla miradi tisa (9) yenye jumla ya thamani ya Tshs. Tshs. 486,833,845/=  Pamoja na kufungua miradi hiyo kutakuwa na mikesha ya Mwenge katika viwanja vya Samora katika Manispaa ya Iringa tarehe 9 na Uwanja wa Sabasaba tarehe 10 katika Halmashauri ya Mji wa Njombe.
Wakiwa Manispaa ya Iringa, wakimbiza Mwenge watapata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya shughuli mbalimbali ya miaka 50 ya Uhuru.
TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE.

Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa:
Shughuli hizi mbili ni za kihistoria, kwa sababu kila mmoja wetu atapata fursa ya kushuhudia mafanikio tuliyofikia. Hivyo, ninawaomba mjitokeze kwa wingi kuanzia tarehe 7 hadi 11 Novemba, 2011 kwenye maonesho tutakayofanya katika uwanja wa Samora na kwenye mapokezi ya Mwenge wa Uhuru ili tuweze kwa pamoja kuiandika historia ya Mkoa wetu vizuri kwa manufaa yetu wenyewe na vizazi vijavyo.


ASANTENI KWA KUNISIKILIZA

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE.

Wednesday, November 2, 2011

KWANZA JAMII LIPEWE USHIRIKIANO

Serikali Mkoani Iringa imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya habari vya Mkoani hapa na nje ya Mkoa ili kuhakikisha uhuru wa upatikanaji habari unashamiri na wananchi wanapata habari zinazohusu maendeleo yao.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma akizundua gazeti la Kwanza Jamii-Iringa  

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma akiongea na mmoja wa wajumbe wa bodi wa gazeti la Kwanza Jamii Maggid Mjengwa

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma wakati akizindua gazeti la Kwanza Jamii-Iringa katika sherehe za uzinduzi zilizofanyika katika uwanja wa shule ya sekondari Mwembetogwa katika Manispaa ya Iringa.

Dk. Ishengoma amesema “ieleweke kuwa serikali imekuwa na ushirikiano mkubwa na mzuri na vyombo vya habari, mara nyingi Mhe. Rais amehimiza ushirikiano huo kwa watendaji wengine, huku akiwataka wananchi kuvitumia vyombo hivyo kwa manufaa ya taifa”.

Aidha, amewataka wananchi wa Mkoa wa Iringa kujitokeza na kutoa ushirikiano wao kwa gazeti hilo kwa manufaa ya maendeleo ya Mkoa wa Iringa. Amewataka kuwa wadau kwa kununua nakala na kutoa matangazo yao ili kulifanya gazeti hilo kuwa endelevu.

Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi wa Mkoa wa Iringa, kulitumia gazeti hilo kama jukwaa la kusemea na kuwaunganisha na viongozi wao kwa manufaa ya maendeleo ya wana Iringa.