Tuesday, January 7, 2014

MAPOKEZI YA RAIS KIKWETE MKOANI IRINGA KUONGOZA MAZISHI YA MAREHEMU DKT. MGIMWA





















SERIKALI IONGEZE SHULE ZA VIPAJI MAALUM



Serikali imeshauriwa kuandaa mkakati wa kitaifa wa kuongeza idadi ya shule za sekondari za bweni na vipaji maalum kutokana na idad ya wanafunzi kufaulu na kupanda kila mwaka ili kuwatendea haki na kulinda vipaji vya watoto.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Bibi. Evarista Kalalu wakati akichangia katika kikao cha uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mkoa wa Iringa kilchofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Bibi. Kalalu amesema ufaulu wa wanafunzi unapanda na kuongezeka lakini sekondari za bweni na vipaji maalum haziongezeki jambo linalosababisha kutokuwatendea haki wanafunzi wengi waliofaulu vizuri kukosa nafasi katika shule hizo. Ameshauri kuwa uwepo mkakati wa kitaifa wa kuongeza shule za bweni na vipaji maalum ili kuwapatia fursa watoto wengi zaidi.

Wakati huohuo, Mbunge wa Mufindi Kusini, Bw. Menrad Kigola ameshauli viwepo vyuo vikuu vya vipaji maalum nchini ili kulinda vipaji vya wanafunzi wanaomaliza shule za sekondari. “Tunazo shule za sekondari za vipaji maalum chakushangaza watoto wetu wanapomaliza sekondari wanajiunga na vyuo vikuu vya kawaida jambo linalochangia kupoteza vipaji vya watoto wetu. Umefika wakati wa serikali kuwa na vyuo vikuu vya vipaji maalum ili kulnda na kuendeleza vipaji vya watoto wetu” amesisitiza Bw. Kigola.  

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa kikao hicho ambae pia ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Bibi. Wamoja Ayubu amewataka wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa wanaripoti na kuanza masomo shule zitakapofunguliwa. Aidha, amewataka kuhakikisha vikao vya tathmini ya elimu na kuzipongeza shule zilizofanya vizuri katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013. 

Bibi. Ayubu amewata kuweka mikakati endelevu ili mwaka 2014 Mkoa wa Iringa ufikie asilimia 70 ambalo ni lengo la Matokeo Makubwa Sasa kwa mwaka huo. Vilevile, amewataka kuhakikisha Kata ambazo zimechukua wanafunzi wengi zaidi kuliko uwezo wa vyumba vya madarasa vilivyopo, kuhakikisha madarasa yanajengwa haraka ili kukidhi idadi ya wanafunzi stahili. Katika kuendeleza ubora wa elimu mkoani, Kaimu Katibu Tawala Mkoa amewataka wakurugenzi kuhakikisha usimamizi na ufuatiliaji unakuwa wa karibu zaidi na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara shuleni ili kuondoa tatizo la wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika.  
=30=

HALMASHAURI ZA MKOA WA IRINGA ZAPONGEZWA KUVULA MALENGO YA BRN




Halmashauri za Mkoa wa Iringa zimepongezwa kwa kazi nzuri katika sekta ya elimu hadi kufanikisha kuvuka lengo la Matokeo Makubwa Sasa (BRN) na kuuwezesha Mkoa kushika nafasi ya tatu kitaifa katika Mtihani wa darasa la saba kitaifa. 

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wanafunzi wa kujunga na kidato cha kwanza Mkoa wa Iringa, Bibi. Wamoja Ayubu katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Uchaguzi wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2013 Mkoa wa Iringa kilchofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Bibi. Ayubu amesema “kiwango cha ufaulu ni kizuri sana na Mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya tatu kati ya mikoa 25 ya Tanzania bara. Pia kiwango cha ufaulu kimepanda kwa Halmashauri zote. Kwa hiyo, nachukua nasafi hii kuzipongeza Halamshauri zote kwa kuvuka lengo la matokeo makubwa sasa ambalo ni asilimia 60 kwa mwaka 2013”.

Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013 Mkoa wa Irnga, Afsa Elimu Mkoa wa Iringa, Mwalimu Joseph Mnyikambi amesema kuwa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi ulifanyika tarehe 11-12 Septemba, 2013. Amesema kuwa shule za msingi 449 kati ya shule 482 ndizo likukuwa na watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi. 

Akiongelea mahudhurio siku za mitihani, Mwalimu Mnyikambi amesema kuwa mahudhurio yameongezeka kutoka asilimia 98.3 ya mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 99 mwaka 2013 likiwa ni ongezeko la asilimia 0.7. Amesema kuwa kiwango cha kumaliza elimu ya msingi kimeongezeka kutoka asilimia 82 (2012) hadi kufikia asilimia 84 (2013) likiwa ni ongezeko la asilimia 2. Aidha, wanafunzi ambao hawakufanya mtihani mwaka 2013 ni asilimia 1 ukilinganisha na asilimia 1.2 mwaka 2012 kutokana na sababu za utoro, vifo, ugonjwa na mimba.

Akiongelea hali ya ufaulu kwa kila Halmashauri katika Mkoa wa Iringa, Afisa Elimu Mkoa amesema kuwa Iringa Manispaa asilimia 81.9 (1), Mufindi asilimia 63.9 (2), Iringa asilimia 62.2 (3) na Kilolo asilimia 60.3 (4).

Amezitaja shule 10 bora katika Mkoa wa Iringa kuwa ni Sipto (1), Ummu Salaama (2), Ukombozi (3), St. Dominic Savio  (4), Star (5), Wilolesi (6), St. Charles (7) zote za Manispaa ya Iringa. Nyingine ni Brooke Bond (8), Southern Highland (9) Mufindi na Mapinduzi (10) Manispaa ya Iringa.
=30=