Tuesday, January 7, 2014

HALMASHAURI ZA MKOA WA IRINGA ZAPONGEZWA KUVULA MALENGO YA BRN




Halmashauri za Mkoa wa Iringa zimepongezwa kwa kazi nzuri katika sekta ya elimu hadi kufanikisha kuvuka lengo la Matokeo Makubwa Sasa (BRN) na kuuwezesha Mkoa kushika nafasi ya tatu kitaifa katika Mtihani wa darasa la saba kitaifa. 

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wanafunzi wa kujunga na kidato cha kwanza Mkoa wa Iringa, Bibi. Wamoja Ayubu katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao cha Kamati ya Uchaguzi wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2013 Mkoa wa Iringa kilchofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Bibi. Ayubu amesema “kiwango cha ufaulu ni kizuri sana na Mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya tatu kati ya mikoa 25 ya Tanzania bara. Pia kiwango cha ufaulu kimepanda kwa Halmashauri zote. Kwa hiyo, nachukua nasafi hii kuzipongeza Halamshauri zote kwa kuvuka lengo la matokeo makubwa sasa ambalo ni asilimia 60 kwa mwaka 2013”.

Akiwasilisha taarifa ya mwelekeo wa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2013 Mkoa wa Irnga, Afsa Elimu Mkoa wa Iringa, Mwalimu Joseph Mnyikambi amesema kuwa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi ulifanyika tarehe 11-12 Septemba, 2013. Amesema kuwa shule za msingi 449 kati ya shule 482 ndizo likukuwa na watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi. 

Akiongelea mahudhurio siku za mitihani, Mwalimu Mnyikambi amesema kuwa mahudhurio yameongezeka kutoka asilimia 98.3 ya mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 99 mwaka 2013 likiwa ni ongezeko la asilimia 0.7. Amesema kuwa kiwango cha kumaliza elimu ya msingi kimeongezeka kutoka asilimia 82 (2012) hadi kufikia asilimia 84 (2013) likiwa ni ongezeko la asilimia 2. Aidha, wanafunzi ambao hawakufanya mtihani mwaka 2013 ni asilimia 1 ukilinganisha na asilimia 1.2 mwaka 2012 kutokana na sababu za utoro, vifo, ugonjwa na mimba.

Akiongelea hali ya ufaulu kwa kila Halmashauri katika Mkoa wa Iringa, Afisa Elimu Mkoa amesema kuwa Iringa Manispaa asilimia 81.9 (1), Mufindi asilimia 63.9 (2), Iringa asilimia 62.2 (3) na Kilolo asilimia 60.3 (4).

Amezitaja shule 10 bora katika Mkoa wa Iringa kuwa ni Sipto (1), Ummu Salaama (2), Ukombozi (3), St. Dominic Savio  (4), Star (5), Wilolesi (6), St. Charles (7) zote za Manispaa ya Iringa. Nyingine ni Brooke Bond (8), Southern Highland (9) Mufindi na Mapinduzi (10) Manispaa ya Iringa.
=30=

No comments:

Post a Comment