Wednesday, May 4, 2011

PONGEZI KWA VYOMBO VYA HABARI IRINGA



Vyombo vya habari vya Mkoa wa Iringa vimepongezwa kwa jitihada kubwa vinazozifanya za kuhamasisha michezo Mkoani hapa hususani mpira wa miguu.
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Bibi. Gertrude Mpaka wakati akipokea shilingi 1,500,000 fedha taslimu zikiwa ni ufadhili wa kampuni ya bia Tanzania (TBL) kwa timu ya Mkoa wa Iringa katika mashindano ya Kili Taifa Cup mwaka 2011 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa leo.
Mwakilisi wa TBL Mkoani Iringa, Masumbuko John Changwe (katikati) akimkabidhi 
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Gertrude Mpaka (kulia) Tshs. 1,500,000 za ufadhili
wa timu ya Mkoa wa Iringa, kushoto ni Afisa Michezo Mkoa Keneth Komba
akishuhudia tukio hilo.

Akitoa shukrani hizo Bibi. Mpaka amesema “nawashukuru sana kampuni ya bia Tanzania kwa mchango wenu wa fedha na vyombo vya habari kwa jitihada kubwa za kuhamasisha michezo na kuutangaza Mkoa wa Iringa”.
Katibu Tawala Mkoa wa Iringa ambaye ndie Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Mkoa amewaasa wanamichezo wanaouwakilisha Mkoa wa Iringa katika mashindano ya Kili Taifa Cup kuzingatia nidhamu ya hali ya juu ili waweze kuuletea Mkoa ushindi na heshima kubwa.
Bibi. Mpaka amesema kuwa Serikali inathamini sana michezo na kukuza vipaji vya wanamichezo nchini na kutokana na umuhimu huo ndio maana Serikali imerudisha michezo ya UMITASHUMTA na UMISETA shuleni.
Awali akitoa maelezo kabla ya kukabidhi fedha za ufadhili wa TBL, mwakilishi wa TBL Mkoani Iringa, Masumbuko John Changwe amesema kuwa kampuni ya bia nchini inamalengo ya kuinua vipaji vya wanamichezo vijana nchini na kuwapatia ajira kupitia michezo.
Aidha, amekemea vikali vitendo visivyo vya kimichezo vya kuwapiga waamuzi na matumizi ya lugha ya matusi kwa wanamichezo. Vilevile amesisitiza kuwepo kwa mfumo mzuri wa kupata timu ya Mkoa iliyo bora kwa kuwashirikisha wadau wote ili timu ya Mkoa iwe na sura ya kimkoa.       
 Nae Katibu wa chama cha mpira wa miguu mkoani hapa Eliud Mvella amesemakuwa changamoto iliyopo ni udhamini ambapo amesema kuwa chama chake kipo mbioni kufanya maongezi na kampuni ya bia Tanzania ili waongeze wigo wa fedha katika udhamini wao.
Timu ya mpira wa miguu ya Mkoa wa Iringa itaondoka kesho tarehe 5 Mkoani hapa kuelekea kuelekea Mkoani Mbeya ambapo inajiwinda kufungua dimba na timu ya Mkoa wa Mbeya hapo tarehe 7 Mei, 2011.

MATUKIO YA MEI DEI KATIKA PICHA

Mgeni rasmi akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala Mkoa,Alhaji Adam Swai



Mgen rasmi akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala Msaidizi,
Sehemu ya Menejimenti ya Serikali za Mitaa, Sifael Kivamba


Mgeni rasmi akisalimiana na Mkuu wa Itifaki, Bahati Golyama

 Mgeni rami akisalimiana na Katibu Tawala Wilaya ya Iringa, Gideon Mwinami


 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Alhaji Mwamwindi akisalimiana na
Katibu Tawala Wilaya ya Iringa, Gideon Mwinami

 Baadhi ya Wafanyakazi Hodari wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Neema Mwaipopo na Vicent James

Waandamanaji katika MEI DEI

...Zingatieni kanuni za kazi
Waajiri wametakiwa kuzingatia misingi na kanuni za kazi ili kuweza kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza kwa kukiukwaji huo mahala pa kazi.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evarista Kalalu katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani- Mei Mosi iliyofanyika kimkoa Wilayani Mufindi leo.


Kaimu Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa (kushoto), Mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika maadhimisho ya Meimosi, Evarista Kalalu (katikati) na kuu wa Wilaya ya Ludewa, Georgina Budala (kulia)

Kaimu Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa (kushoto), Mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa katika maadhimisho ya Meimosi, Evarista Kalalu (katikati) na kuu wa Wilaya ya Ludewa, Georgina Budala (kulia)

Kalalu amesema “ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima mahala pa kazi waajiri wote wafanye kazi kwa kufuata misingi ya Sheria na Kanuni za kazi”. Mfanyakazi anawajibu wa kuipenda kazi yake lakini kero za kikazi zinapokuwa nyingi humfanya mfanyakazi kuichukia na ufanisi wa kazi yake kupungua. “Naomba sana tujitahidi kupunguza kero kwa wafanyakazi wetu na ikibidi tuwape motisha ambazo zitawafanya wafanye kazi kwa bidii” amesisitiza Kalalu.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Mufindi amewata waajiri kuwa makini wanaposhughulikia utatuzi wa kezo za wananchi kuzingatia makundi yote husika. Amesema kutokufanya hivyo kunaweza kujenga mianya ya kutengeneza makundi baina ya wafanyakazi na badala ya kutatua kezo husika kujikuta wanatengeneza kero na migogoro mingine ambayo ingeweza kuepukika.
  
Aidha, amewataka waajiri kutenga  muda wa kukaa na waajiriwa wao ili kujadili masuala mbalimbali ya kazi na matatizo yanayojitokeza ili yamalizwe kwa njia ya mazungumzo.

Awali akisoma risala ya wafanyakazi wa Mkoa wa Iringa, Mratibu wa TUCTA Mkoa, Khatibu Juma Baweni amesema kuwa wafanyakazi wanawajibu wa kufanya kazi kwa bidii na kuongeza tija katika jitihada za kuongeza pato la taifa. Amesema “kila mtu akitimiza wajbu wake hapatakuwa na malalamiko baina ya wafanyakazi na waajiri” amesisitiza Baweni. Aidha, amesisitiza kilio cha wafanyakazi dhidi ya kupanda kwa bei ya umeme, mafuta na bidhaa nyingine jambo lisiloenda sanjali na upandaji wa mishahara ya wafanyakazi jambo linalomdidimiza mfanyakazi kiuchumi.

Maadhimisho haya ya siku ya wafanyakazi duniani maarufu kama Mei Mosi ni kumbukumbu ya mapambano ya wafanyakazi ya kujikomboa yaliyoanzia Ulaya na Marekani ya Kaskazini katika karne ya 18 na 19 kutoka katika ukandamizaji na unyonyaji wa waajili kutokana na ukuaji wa viwanda.